# | ind | swa |
---|
1 | Somalia: Apakah Pemerintah Merekrut Pemuda Kenya Untuk Berperang? | Somalia: Je Serikali Inawaandikisha Vijana Wa Kikenya Kwa Ajili Ya Vita? |
2 | Ini adalah rangkuman blog Somalia yang pertama kali di tahun 2009. | Huu ni muhtasari wa kwanza wa blogu za Kisomali mwaka 2009. |
3 | Ya, sudah setahun lebih saya mengambil cuti panjang dari aktivitas penulisan blog, namun sekarang saya kembali untuk selamanya. | Naam, ni zaidi ya mwaka mmoja tangu nilipochukua likizo ya muda mrefu kutoka kwenye shughuli za kublogu lakini sasa nimerudi, moja kwa moja. |
4 | Ini merupakan pos pertama dan akan ada pos-pos lainnya tentang blogosfer Somalia. | Hii ni makala ya kwanza na tarajieni makala zaidi zinazohusu ulimwengu wa blogu za Kisomali. |
5 | Narablog Royale Somalia menerangkan profil seorang dokter wanita muda Somalia di Mogadishu yang lulus tahun lalu, ia menulis: | Mwanablogu Royale Somalia anatoa wasifu wa daktari mdogo wa kike jijini Mogadishu ambaye alimaliza masomo mwaka jana, anaandika: |
6 | Pada Desember 2008, 20 murid Somali mengatasi segala rintangan dan lulus dari sekolah medis di Mogadishu-kelompok pertama yang berhasil dalam kurun waktu hampir dua dekade di negara Tanduk Afrika yang gagal ini. | Mwezi Desemba mwaka 2008, wanafunzi 20 walishinda vigezo vikubwa na kufuzu kutoka chuo cha uganga huko Mogadishu - kundi la kwanza kufanya hivyo katika takriban miongo miwili ndani ya nchi iliyoshindwa katika pembe ya Afrika. |
7 | Dr. Hafsa Abdurrahman Mohamed, 26, adalah salah seorang yang menerima diploma dari Universitas Benadir yang terletak di ibu kota. | Dr. Hafsa Abdurrahman Mohamed, 26, alikuwa ni mmoja wa waliopokea stashada kutoka katika Chuo Kikuu cha Benadir jijini humo. |
8 | Dalam tahap penyelesaian studinya, ia memutuskan bekerja untuk Ikatan Dokter Tanpa Perbatasan/Médecins Sans Frontières (MSF), mempraktikkan keahliannya demi memberikan perawatan medis gratis di Somalia. | Wakati anamaliza masomo yake aliamua kufanya kazi kwa Waganga Wasio na Mipaka/ Médecins Sans Frontières (MSF), kwa kutumia ujuzi wake ili kutoa huduma za bure za afya nchini Somalia. |
9 | The East African Philosopher mengomentari kunjungan Presiden Somalia Sharif Ahmed ke AS dan perubahan kebijakan pemerintah AS dalam menangani Sharif: | Mwanafalsafa wa Afrika ya Mashariki anatoa maoni juu ya ziara ya Rais Sharif Ahmed nchini Marekani na mabadiliko ya sera ya serikali ya Marekani katika mahusiano yake na Sharif: |
10 | Pada Desember 2006 Sheikh Sharif Sheikh Ahmed, yang sekarang menjabat sebagai Presiden boneka Pemerintahan Federal Transisi Somalia, menjadi buron tentara Ethiopia, CIA, dan Prajurit Komando AS. | Mwezi Desemba 2006, Sheikh Sharif Sheikh Ahmed, ambaye hivi sasa ni rais-kwa-jina-tu wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho la Somalia, alikuwa analikimbia jeshi la Ethiopia, CIA, pamoja na wanamgambo wa Marekani. |
11 | East African Philisophers melanjutkan: | Mwanafalsafa wa Afrika ya Mashariki anaendelea: |
12 | Minggu ini Sheikh Sharif berada di Minneapolis, MN (dan merupakan rumah seorang anggota kongres wanita yang sinting) untuk menghadiri rapat dengan para anggota Kongres, Pemerintah, dan perwakilan masing-masing kota/walikota. | Wiki hii Sheikh Sharif yuko Minneapolis, MN (na nyumbani kwa mbunge mwendawazimu wa kike wa bunge la chini la Marekani) anakutana na wabunge, Gavana na madiwani/Meya. |
13 | Beberapa bulan lalu ia rapat dengan Sekretaris Clinton di Nairobi dalam perjalanan Clinton ke Afrika. | Miezi miwili iliyopita alikuwa na mkutano na Katibu Clinton jijini Naorobi wakati wa ziara yake ya Afrika. |
14 | Status Sheikh Sharif sebagai teroris dan kemudian berubah menjadi presiden hanya dalam dua tahun. | Kutokea gaidi mpaka kuwa rais kwa Sheikh Sharif katika miaka miwili. |
15 | Hal seperti ini, kawan-kawan, pastilah yang pertama kali terjadi. | Jambo hilo, marafiki, ni lazima limetokea kwa mara ya kwanza. |
16 | Bagi saya ini menjelaskan lebih dari apapun hal-hal tentang kebijakan asing AS yang buruk. | Kwangu mimi hili linaongea vikubwa kuhusu sera mbaya ya nchi za nje ya Marekani zaidi ya jingine lolote. |
17 | The Kenya Somali Blog berkata pemerintahan Somalia sedang merekrut pemuda Somalia dari Kenya: | The Kenya Somali Blog anasema kuwa Serikali ya Somalia inawaandikisha vijana wa Kisomali kutoka Kenya: |
18 | Pemerintah Somalia yang didukung oleh PBB telah merekrut lebih dari 170 pemuda Kenya dan mantan tentara untuk membantu melawan para pemberontak di negara Tanduk Afrika yang gagal ini, menurut para pembaca lokal di daerah timur Kenya. | Serikali ya Somalia inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imewaandikisha zadi ya vijana 170 wa Kikenya na wanamgambo wa zamani ili wakasaidie kupigana na waasi katika nchi iliyoshindwa ya pembe ya Afrika, viongozi walio katika maeneo ya mashariki ya Kenya wamesema. |
19 | Mohamed Gabow, walikota Garissa, memberitahu Reuters pendaftaran etnis Kenya Somalia sedang dilaksanakan di sebuah rumah di desa, di pinggiran kota. | Mohamed Gabow, Meya wa Garissa, aliiambia Reuters kuwa uandikishaji huo wa vijana wa Kikenya wenye asili ya Kisomali ulikuwa unafanywa katika nyumba moja kwenye kijiji cha Bulla Iftin, kilichopo pembezoni mwa mji wake. |
20 | Perekrutan ini tidaklah rahasia. | Uandikishaji huo sio siri. |
21 | Mereka yang terlibat tidak takut. | Wanaohusika hawaogopi. |
22 | Mereka berkeliling ke seluruh desa untuk mengumumkan waktu pelatihan,” kata Gabow dalam suatu wawancara pada Kamis malam. | Wanakwenda vijijini kote kutangaza zoezi hilo,” Gabow alisema katika mahojiano siku ya Alhamis. |