# | mlg | swa |
---|
1 | Madagasikara: Manova olona ny mipetraka Andafy | Madagascar: Kuishi ughaibuni hubadili uhusiano |
2 | | Katika makala iliyochapishwa mwezi Machi, wachumi William Easterly na Yaw Nyarko wanaeleza kwamba katika nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara, kiasi cha fedha kinachotumwa na wahamiaji wanaotoka bara hilo ni wastani wa asilimia 81 ya misaada ya fedha kutoka nchi za kigeni kwa kila nchi. |
3 | News2dago no mitantara ny fitotongan'ny fifandraisana ananany tamin'ny namana tena akaiky azy tany ampianarana satria nifindra nankany Firantsa io namany io: | Dhima ya waMadagascar walio nchi za mbali kwa maendeleo ya nchi yao imewahi kujadiliwa hapo kabla katika ulimwengu wa wanablogu wa Madagascar. |
4 | | Hivi karibuni wanablogu walijadili athari ya kuishi ughaibuni kwa mienendo ya WaMadagascar na jinsi mabadiliko hayo yanavyoathiri uhusiano na marafiki na ndugu zao walio nyumbani. |
5 | “Nisy ranamana izay niray dabilio tamiko ary tena akama be mihitsy izy io tany @ taona 1992 tany ho any izahay no nihaona farany rehefa azo moa ny Bacc dia nanam-bitana ranamana ka lasa tany frantsa nanohy ny fianarany. | News2dago anasimulia ni kwa namna gani alipoteza urafiki wa karibu aliokuwa na rafiki yake mmoja wa tangu enzi za shule. Anaeleza kwamba uhusiano wao ulififia polepole mara tu baada ya rafiki yake kuondoka kwenda zake Ufaransa: |
6 | Ny tena moa dia teto @ tanana ihany safidy moa io tsy misy omena tsiny mihitsy. | Nilikuwa na uhusiano mzuri na rafiki yangu tangu tulipokuwa madarasa ya juu ya sekondari. Tuliketi dawati moja. |
7 | Nivadika teny ihany ny volana sy ny taona tsy dia henoheno intsony ranamana taty aorina fa misy inona ary olona sendra nahalala azy no niteny tamiko oe nanam-bady izy! | Mara ya mwisho kumtia machoni ilikuwa mwaka 1992 wakati wa mahafali ya kumaliza elimu ya sekondari na kutunukiwa cheti. Rafiki yangu alipata bahati ya kuendelea na masomo ya juu nchini Ufaransa. |
8 | Ny tena moa manoratra email ihany fa tsy misy valiny intsony e!” | Mimi nilichagua kubaki nyumbani, ulikuwa uamuzi binafsi, hakuna wa kumlaumu kwa hili. |
9 | Nampian'i News2dago moa fa afaka nianatra ho any Firantsa ihany koa ny tenany tamin'ny taona 2005 fa rehefa nieritreritra lalina izy dia naleony ihany nijanona. | Miaka ilipita na mawasiliano na rafiki yangu, ambayo mwanzoni nilipata mara kwa mara, polepole yalianza kufifia. Siku moja nilipata taarifa kutoka kwa mtu tuliyefahamiana naye kwamba rafiki yangu yule alikuwa amekwishafunga ndoa. |
10 | Nambarany ary ny antony: Very be dia be ny fifaneraserana any Firantsa, samy maka ho azy ny olona any, tsy misy namana ilalaovana belaoty intsony, naleony nananganany tetikasa teto an-toerana ihany ny vola tokony nandehanana tany. | Niliendelea kumwandikia barua-pepe lakini pasipo kupata jibu lolote. News2dago anaongeza kwamba yeye pia alipata fursa ya kusafiri kwenda Ufaransa mwaka 2005, lakini baada ya kutafakari vyema aliamua kubaki nyumbani. |
11 | | Anataja baadhi ya sababu za kufanya hivyo: udugu hupotea miongoni mwa WaMadagascar mara baada ya kufika Ufaransa, kila mmoja anakuwa na lwake, hakuna kukutana ili kucheza mchezo wa karata, pia alitumia pesa ambazo zingemuwezesha kwenda ughaibuni ili kuusimamisha mradi anaoufanya sasa. |
12 | “Izay no tsara kokoa toy izay tahaka an-dry zalahy manana dipilaoma maro dia maro.” | “Ni afadhali kufanya hivi kuliko kushughulika na watu walio ughaibuni na vyeti vyao vya mbwembwe vya elimu.” |
13 | Hoy manko izy: | Anaongeza: |
14 | “Ny namana taloha ary ity toa mody fanina izany satria niantso azy efa in-3 aho t@ izany fotoana izany dia noraisiny t@ voalohany nandeha ny resaka ary natsidiko ny teny hoe “hibôsy kely any @ lisany any lesy aho raha sitram-po ny Tompo a”, “hay ve hoy ranamana”, “miantso anla ihany aho rehefa tena tapa-kevitra e”. | Kuna kipindi nilimpigia simu ili tupige soga na kujikumbusha mambo ya zamani. Nilimwambia kwamba Mungu akipenda, huenda nitakuja huko kufanya kazi na kuwa mmoja wenu. |
15 | Nanomboka teo dia lasa messagerie vocal foana ny finday-n'ilay ranamana” | “Kweli?” aliniuliza. Tangu nilipomweleza hayo, kila nikimpigia nakutana na ujumbe wa kunitaka kuacha ujumbe wa sauti. |
16 | Mifandraika amin'izany ihany dia nolazain'i news2dago fa nisy zanaky ny mpiray tampo taminy vavy iray nitodi-doha teto Madagasikara fa hatao mariazy amin'ny namany izay Malagasy ihany koa nifanena taminy tany. | Katika habari inayohusiana na hiyo, news2dago alisema kwamba mpwa wake alirejea Madagascar kutokea Ufaransa ili kufunga ndoa na Mmadagascar mwenzake aliyekutana naye ughaibuni. |
17 | Efa niomanany avokoa ny zava-drehetra, hatramin'ny nitondra mpaka sary matihanina avy any Firantsa. | Walihakikisha kwamba harusi nzima imepangwa vema, hata walileta mpiga picha mtaalamu kutoka Ufaransa. |
18 | Niangavy ny hampiasa ny aterinetony tao an-tranony izy ireo hikarakaran'izy ireo ny fiovana rivotra nankany Mahajangà, ary dia tsy nandalo nanao veloma akory izy ireo rehefa niverina nankany Firantsa indray. | Walimwomba watumie kifaa chake cha kuunganisha intaneti ili kupanga fungate lao katika eneo la Mahajanga mara baada ya harusi. Pamoja na hayo yote hawakuona ulazima wa kuaga walipokuwa wanaondoka kurudi zao Ufaransa. |
19 | Tena manova olona tokoa ny miaina any andafy. | Ama kwa hakika kuishi ughaibuni hubadilisha watu. |
20 | Raha namaly ity tantara ity moa Ravatorano dia nilaza fa tsy ny mpiray firenena monina any andafy ihany no manana izany tsy firaharahiana na mody fanina amin'ny namana izany. | Akieleza kuguswa na taarifa hiyo, Ravatorano anaamini kwamba tabia ya kujifanya kutojali au kuwapuuza marafiki wa zamani haipo tu miongoni mwa raia wa nchi moja ughaibuni. |
21 | Na izany aza dia nolazainy fa fanajana kely indrindra ny manaja ny olona izay nanampy anao. | Hata hivyo, anaamini kwamba ni jambo stahiki kuonyesha heshima kwa watu waliokusaidia. |
22 | Namazivazy i Simp hoe: ” Mamindrà fo azy fa olombelona ihany izy… Ny soa atao levenambola hoy izy ary ny ratsy atao loza mihantona. | Simp alidakia kishabiki: “Wasameheni kwani wao ni binadamu tu … matendo mema ndiyo mbegu za bahati njema na matendo maovu ni kama jambia la hukumu la Damocles.” |
23 | ” lehilahytsyresy indray no manome ny anton'izay mety hanadinoana ilay fisakaizana akaiky izay (mg): | lehilahytsyresy anajaribu kutoa maelezo ya sababu kwa nini watu wanatelekeza urafiki wa kweli kwa ajili ya urafiki wa kutumiana (mg): |
24 | “Rehefa voaporitra mafy ao anaty fiaraha-monina gejain'ny concurrence ady-saritaka isan'andro isan' andro izy, dia normal raha toa ka raiki-tapisaka ao an-tsainy koa izay fomba fisainana “namana-raha-misy-patsa” izay, mba hahafahany mi-survivre. | “Wamadagaska wanapobinywa na ukweli wa maisha ya ughaibuni,, ushindani mkali na maisha yaliyojaa madhila mengi kila siku, kwa hiyo ni jambo la kawaida kwamba mtazamo wa “ni rafiki ikiwa ni tajiri” utawale, maana mtazamo huu ni muhimu ili mtu upate kuishi. |
25 | Rehefa avy eo koa anefa, dia tsy afaka intsony ilay toetra ka na dia ny havana koa aza, dia lasa anaovana “havako-raha-misy-patsa”. | Kwa bahati mbaya, tabia hiyo huwaingia mno watu kiasi kwamba mtazamo huo huutumia hata dhidi ya ndugu zao, na hatimaye anakuwa ndugu wa kweli endapo tu ni “mtu aliye nazo”. |