# | nld | swa |
---|
1 | De paus in Kameroen (2): Over geestelijken, corruptie en politiek | Papa Nchini Kameruni (2): Wazee Wa Kanisa, Upotofu na Siasa |
2 | Het bezoek van het hoofd van de rooms-katholieke kerk aan Kameroen in maart 2009 was voor een aantal Kameroense bloggers reden om de aandacht te vestigen op de politieke gevolgen (als die er al zijn) van een pausbezoek aan een land als Kameroen. | Ziara ya kiongozi wa Kanisa La Katoliki nchini Kameruni mwezi huu wa Machi 2009 imepelekea baadhi ya wanablogu wa Kikameruni kuelekeza tochi zao kwenye matokeo ya kisiasa (kama yapo) yatakayotokana na ziara hiyo ya Papa nchini humo. |
3 | Neba Fuh van Voice of the Oppressed [en] is een van hen: | Neba Fuh anayeblogu kwenye Voice of The Oppressed ni mmoja wa wanablogu hao: |
4 | De vorige paus, Johannes Paulus II, heeft Kameroen twee keer eerder bezocht en het effect op de toch al verpauperde bevolking was slechts religieuze euforie die werd betaald uit hun eigen financiële bijdragen en uit de schatkist. | Mara mbili, Hayati Papa Yohane Paulo wa Pili alizuru Kameruni na matokeo ya ziara hizo kwa umma wa watu ambao ni masikini hayakuwa zaidi ya furaha ya kidini iliyowagharimu michango binafsi pamoja na ile ya hazina ya serikali. |
5 | De onbeantwoorde vragen over de onderdrukking door Biya werden niet beantwoord. | Maswali yasiyo na majibu kuhusu vitendo vya ukandamizaji vya (rais) Biya yalibaki bila ya majibu. |
6 | Aloysius Agendia, journalist en voormalig seminarist, lijkt in een artikel met de titel Pope Benedict XVI visit to AFRICA: Going beyond spiritual rhetoric [en] te suggereren dat de kerk daden van overheden en politici die het belang van het volk schaden aan de kaak moet stellen in plaats van zich te omhullen met diplomatie: | Aloysius Agendia, mwanahabari ambaye pia ni mseminari wa zamani katika makala aliyoipa kichwa cha Ziara ya Papa Benedikti wa XVI AFRIKA: zaidi ya kauli za kiroho inaonekana kwamba angependa Kanisa lipinge vitendo vya dola na vya wanasiasa ambavyo vinaharibu maslahi ya umma badala ya kuvivika majoho ya kidiplomasia: |
7 | We begrijpen dat de kerk en het Vaticaan als staat, en als religieus orgaan, maar met politieke connotaties, soms een diplomatieke aanpak moet kiezen. | Tunalielewa Kanisa na Vatikani kama dola, kadhalika kama chombo cha dini, japokuwa lina maana pia ya kisiasa, na wakati mwingine linapaswa kuwa na diplomasia katika mtazamo wake. |
8 | Naar mijn mening moet echte religie niet onverschillig zijn voor onrecht, onderdrukking, exploitatie, kolonialisme in al hun vormen en andere soorten corruptie. | Kwa maoni yangu, dini ya kweli haipaswi kufumbia macho maovu, ukandamizaji, unyonyaji, ukoloni katika mifumo yake yote pamoja na maovu mengine. |
9 | De katholieke kerk heeft veel gedaan en doet nog steeds veel, maar er moet nog veel meer worden gedaan. | Kanisa Katoliki limefanya mengi na linaendelea kufanya lakini mengi zaidi bado yanapaswa kufanywa. |
10 | Diplomatie is op zich goed, maar de kerk moet het niet te vaak gebruiken, ze moeten er geen doekjes om winden. | Hata hivyo, diplomasia hata kama ni nzuri katika namna yake, haitakiwi kutumika sana katika Kanisa kwa sababu, beleshi ni lazima liitwe beleshi. |
11 | In hun pogingen om brandende kwesties altijd maar weer “subtiel” uit te leggen, gaat de boodschap verloren of wordt de betekenis/het belang ernstig gebagatelliseerd. | Katika kujaribu kutumia mbinu “laini” ili kufafanua masuala mazito, ujumbe huweza kupotea au maana/na umuhimu, unaweza kuchujwa sana. |
12 | Kerkelijke leiders moeten ervoor kiezen om niet alleen om te gaan met machthebbers, met rijke en invloedrijke mensen. | Viongozi wa kanisa hawapaswi kuchagua kufanya karamu na wale walio madarakani, matajiri na wenye nguvu. |
13 | Ze hoeven niet zo nodig met de oppositie om te gaan, maar ze moeten naast de zwakken, de onderdrukten, de zieken enzovoort staan. | Siyo lazima wawe na pamoja na wapinzani, lakini, inawabidi wasimame pamoja na wanyonge, wanaokandamizwa, wagonjwa n.k |
14 | Hij is duidelijk over wat hij van de paus verwacht: | Anajua wazi ni nini anachotegemea kutoka kwa Papa: |
15 | Als een spirituele leider die hoop vertegenwoordigt, moet hij ons niet alleen maar vertellen om te wachten en te hopen. | Kama kiongozi wa kiroho anayewakilisha matumaini, hatakiwi kutuambia tuendelee kungoja na kutumaini. |
16 | We verwachten van hem dat hij moedig genoeg is om degenen die de hoop van Kameroeners en Afrikanen dwarsbomen ten minste te vertellen dat ze enig gevoel moeten hebben voor mensen en voor hun medeburgers. | Tunatumaini kuwa atakuwa na ujasiri wa kutosha kuwaaambia wale wanaokinza matumaini ya Wakameruni na Waafrika wawe angalau na hisia kwa wanaadamu wenzao au wananchi wenzao. |
17 | Aan de andere kant vraagt Voice of the Oppressed [en] zich af of de geestelijkheid in met name Kameroen ethisch genoeg is om verandering te eisen van de leiders van het land terwijl ze zelf geen lichtende voorbeelden zijn: | Kwenye upande mwingine, Voice of the Oppressed anajiuliza kama wazee wa kanisa hasa wale wa Kameruni wana maadili ya kutaka mabadiliko kutoka kwa wale wanaotawala nchi wakati wao wenyewe sio mifano angavu: |
18 | Wat kan een maatschappij, die al moreel verzwakt is, leren van een bisschop of priester die lukraak kinderen verwekt in zijn gemeenschap? | Ni somo gani ambalo jamii iliyopotoka kimaadili inaweza kujifunza kutoka kwa askofu au padri ambaye anazaa watoto kiholela katika jamii yake? |
19 | Wat kan die maatschappij leren van een priester die talloze ‘vriendinnen' in zijn gemeenschap heeft, met als excuus dat hij ook maar een mens is, net als iedereen? | Ni somo gani ambalo jamii inaweza kujifunza kutoka kwa padri mwenye wapenzi wa kike kadhaa kwenye jamii, kwa kisingizio kuwa ati “ni mwanaadamu” kama wanaadamu wengine? |
20 | Of van iemand die voor zijn vriendin een reis naar het buitenland betaalde, weg van zijn gemeenschap, zodat ze zijn kinderen kan baren, en die, als hij op vakantie gaat of studieverlof opneemt, in het buitenland wordt verwelkomd door ‘zijn vrouw' en ‘kinderen'? | Au anayedhamini safari ya rafiki huyo wa kike nje ya nchi, mbali na jamii, ili aweze kumzalia watoto, na pale anapochukua likizo au likizo ya masomo, anakaribishwa huko nje ya nchi na “mke” pamoja na “wanawe”? |
21 | Of van een schoolhoofd, tevens priester, die schoolgeld verduistert met behulp van nepfacturen en een nepboekhouding? | Au mkuu wa shule ambaye ni padri, ambaye anafuja fedha za shule kwa kutumia hundi na mahesabu ya kughushi? |
22 | Of van priesters die zich als roofdieren op kwetsbare kinderen storten die tot hun beschikking zijn gesteld? | Au padri ambaye amegeuka kuwa mwindaji wa watoto wasio na kinga ambao wamewekwa chini ya usimazi wake? |
23 | Volgens Aloysius Agendia moet paus Benedictus XVI iets doen aan de vermeende onberekenbaarheid van katholieke prelaten in Kameroen: | Kwa Aloysius Agendia Papa Benedikti wa XVI anapaswa aongelee mwenendo wa hovyo wa viongozi wa Kikatoliki nchini Kameruni: |
24 | De Heilige Vader moet hier bij zijn bezoek aan Kameroen en Afrika aandacht aan besteden. | Wakati Baba Mtakatifu anapozuru Kameruni na Afrika, ni lazima akumbuke hili. |
25 | Op de eerste plaats moet de katholieke kerk, en dan vooral de meeste van hun (herders) in Kameroen, nodig worden “gesaneerd” of “gereviseerd”. | Kwanza kabisa, Kanisa Katoliki na wengi wa (wachungaji) wake katika Kameruni wanahitaji “kurekebishwa” au “kukarabatiwa”. |
26 | Er moet iets worden gedaan aan de talloze verhalen over de promiscuïteit, de extravagantie en het lichtzinnige gedrag van sommigen van onze priesters, inclusief bisschoppen. Sommigen gaan zelfs zo ver dat ze kinderen verwekken, anderen plegen ontucht met hun studenten, met de vrouwen van anderen, met parochianen, enzovoort… | Habari nyingi zinazohusu uzinzi, ufujaji na tabia za utongozaji kwa baadhi ya mapadri wetu wakiwamo maaskofu, ambao wengine wanafika mbali hata kuzaa watoto, wengine wanafanya ngono na wanafunzi wao, wake za watu, wanaparokia n.k, ni lazima viongelewe… |
27 | Deze blogger vindt dat als dit soort corruptie binnen de rooms-katholieke kerk niet door de paus wordt aangepakt, het bezoek voor hem geen betekenis heeft: | Mwanablogu huyu anaamini kuwa kama masuala ya upotofu ndani ya Kanisa la Kikatoliki la Roma nchini Kameruni hatashughulikiwa na Papa, ziara hiyo haitakuwa na maana yoyote kwake: |
28 | Het verpanden van de kerk en haar bezittingen voor “leningen”, alsof Jezus Christus opnieuw wordt verkocht voor 950.000.000 CFA-frank [1,5 miljoen euro] zoals Judas deed voor 30 zilverlingen. | Kuliweka rehani Kanisa na mali zake kwa ajili ya kuchukua “mikopo”, kama vile kumuuza Yesu Kristu tena kwa Faranga 950.000.000 kama vile Yuda alivyofanya kwa vipande 30 vya fedha. |
29 | Dit volgt op het gebruik van een beroemde kathedraal in Kameroen als onderpand voor een lening die door een van hun bisschoppen is afgesloten. | Hii inatokana na kanisa linalojulikana sana nchini Kameruni kuwekwa kama dhamana kwa ajili ya mkopo aliochukua mmoja wa maaskofu wake. |
30 | De ernstige en afschuwelijke verduisteringszaken verdienen onder andere de aandacht van de paus. | Kuna kesi za kutisha za ufujaji ambazo zinabidi kutupiwa macho na Papa. |
31 | Als de paus deze zaken niet aan de orde stelt, ook al is het privé met zijn priesters, dan moet ik toegeven dat zijn missie naar Kameroen bij lange na niet aan de verwachtingen voldoet en, waarom niet, een kansloze zaak is. | Haya ni masuala ambayo ikiwa Papa atashindwa kuyashughulikia hata katika faragha na mapadri wake, basi ziara yake nchini Kameruni, ni lazima nikubali, kwamba itakuwa imeanguka chini ya matarajio. |
32 | Zal de paus het aandurven? | Je Papa atathubutu? |
33 | Dat zou wel eens het volgende punt van aandacht kunnen zijn in de Kameroense blogosfeer. | Hilo litakuwa ndio suala linafuatia kwenye ulimwengu wa blogu wa Kameruni. |
34 | Opmerking: Deel 1 van dit artikel staat hier. | Tafadhali Angalia: Sehemu ya kwanza ya makala hii inapatikana hapa. |