# | spa | swa |
---|
1 | Trabajadores y fuerzas de seguridad se enfrentan al Norte de Mauritania | Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania |
2 | Foto de los enfrentamientos, publicada por Abo Bakr Ahmado en su cuenta de Facebook | Picha ya mapigano, iliyowekwa na Abo Bakr Ahmado kwenye ukurasa wake wa Facebook |
3 | La mañana del martes 28 de mayo de 2013, miles de trabajadores, que cobran sus remuneraciones en jornales diarios, iniciaron una gran protesta [ar] en Zuérate, la capital del estado Tris Zemmour en el Norte de Mauritania, exigiendo contratos y derechos apropiados, así como el fin del monopoio de los empresarios en la Empresa Minera Árabe (ARMICO, por su nombre en inglés). | Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara kwenye makampuni ya machimbo ya madini katika nchi za Kiarabu (ARMICO). |
4 | Los trabajadores se dirigieron a la sede administrativa del estado estado antes de que las unidades antidisturbios suprimieran la protesta. Los trabajadores respondieron ocupando el edificio del estado, las instalaciones de una de las empresas contratistas y los edificios de la radio estatal. | Wafanyakazii hao waliandamana kuelekea kwenye makao makuu ya utawala wa jimbo hilo, majengo ya mmoja wapo wa makampuni ya wakandarasi, pamoja na majengo ya kituo cha redio ya taifa. |
5 | El ejército [ar] intervenino para controlar la situación y detener las protestas de los trabajadores. | Jeshi [ar] liliingilia kati kudhibiti hali hiyo na kuyatawanya maandamano hayo. |
6 | El activista Magdy Ahmed tuiteó sobre el escape del gobiernador de Tris Zemmour luego de las protestas de los trabajadores [ar]: | Mwanaharakati Magdy Ahmed alitwiti kuhusu kutoroka kwa gavana wa Tiris Zemmour baada ya wafanyakazi kuandamana [ar]: |
7 | @mejdmr: El gobernador Ould Bahia, el vicegobernador y la policía huyeron tras presenciar el día de furia de los trabajadores cuando ocuparon la gobernación y las oficinas de la radio estatal. | @mejdmr: Gavana, Ould Bahia, naibu gavana na polisi walikimbia baada ya kushuhudia hasira ya wafanyakazi hao kwa siku moja walipovamia ofisi ya gavana na kituo cha redio ya taifa. |