# | spa | swa |
---|
1 | Ministro ugandés: Las mujeres que se visten de forma indecente piden que las violen | Waziri wa Uganda: Wanawake Wasiovaa Mavazi ya Heshima Wanaomba Kubakwa |
2 | Captura de pantalla de la petición que exige la dimisión del ministro. | Picha ya tamko linalomtaka waziri huyo ajiuzulu. |
3 | Según el ministro ugandés de la Juventud [en], Ronald Kibuule, las mujeres que visten indecentemente están pidiendo que las violen, y los sospechosos de haber violado a una de estas mujeres deberían ser puestos en libertad. | Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Vijana wa Uganda Ronald Kibuule, wanawake wanaovaa mawazi yasiyositiri miili yao wanaomba kubakwa, na watuhumiwa wanaodaiwa kuwabaka wanawake waliovaa namna hiyo waachiliwe huru. |
4 | También dijo que en casos de violación, la policía debería, en primer lugar, comprobar la indumentaria de la víctima, y si vestía de forma indecente, la debería acusar de incitación al delito. | Alisema vile vile kuwa katika kesi za ubakaji, polisi wawe wa kwanza kusimamia namna wanawake hao waathirika walivyovaa, na kama wamevaa hovyo, nao washitakiwe kwa kosa la kukaribisha uhalifu. |
5 | Kibuule hizo estos comentarios en el condado de Kajara, distrito de Ntungamo, el sábado 21 de setiembre de 2012, mientras asistía al almuerzo de la Cooperativa de Desarrollo y Sociedad de Ahorro de los Jóvenes de Kajara. | Kibuule alitoa matamshi hayo akiwa kwenye halmashauri [kaunti] ya Kajara, wilayani Ntungamo siku ya Jumamosi Septemba 21, 2013 wakati akihudhuria ufunguzi wa Chama cha Ushirika na Akiba cha Vijana wa Kajara. |
6 | Los comentarios aparecieron en el periódico ugandés Daily Monitor [en] el 24 de setiembre. | Kauli hiyo ilionekana kwenye gazeti la Uganda Daily Monitor la Septemba 24, 2013. |
7 | No obstante, el artículo no explicaba las circunstancias en las que Kibuule hizo los comentarios. | Makala hiyo, hata hivyo, haikueleza mukhtadha ambao Kibuule alitoa matamshi hayo. |
8 | El parlamento ha pedido la comparecencia [en] del ministro para que explique las declaraciones que hizo en Kajara. | Bunge limemtaka waziri huyo ajieleze bungeni ilikuwaje akatoa matamshi hayo juma lililopita. |
9 | Los internautas ugandeses reaccionaron con indignación a dichos comentarios utilizando la etiqueta #Kibuule [en] en Twitter. | Raia wa Uganda mtandaoni walijadili matamshi hayo kwa hasira wakitumia alama habari #Kibuule kwenye mtandao wa twitter. |
10 | Los que pedían su dimisión lanzaron las etiquetas #KibuuleMustGo [en] (Kibuule debe irse) y #KibuuleOut [en] (fuera Kibuule). | Wale waliomtaka ajiuzulu wanatumia alama habari #KibuuleMustGo [Kiluule Lazima Ang'oke] na #KibuuleOut [Kibuule Nje]. |
11 | En Change.org hay una petición [en] que pide su dimisión: | Tamko lililopo kwenye mtandao wa Change.org linamtaka ajiuzulu: |
12 | Con esas palabras, el Sr. Kibuule promueve la violación de mujeres según su indumentaria: exime a los violadores de sus delitos contra mujeres supuestamente ligeras de ropa y se asegura de que las víctimas de una violación tengan miedo de hacerlo público por temor a que el hecho de haber sido violadas les cause problemas legales. | Kwa manano haya, Bw. Kibuule anautangaza ubakaji wa wanawake kwa kigezo la mavazi yao; anawahurumia wabakaji kwa makosa yao ya jinai waliyoyafanya kwa wanawake wanaodaiwa kuvaa vibaya na; anahakikisha waathirika wa ubakaji wanapata hofu ya kujitokeza hadharani kwa kuogopa kushitakiwa kwa kubakwa. |
13 | Debería perder su puesto inmediatamente, ya que está claro que no representa el bienestar de sus electores. | Lazima aachane na msimamo huo haraka sana kwa kuwa ni wazi alichokisema hakiwakilishi ustawi wa wapiga kura wake. |
14 | Rosebell Kagumire (@RosebellK [en]), una periodista en línea ugandesa, escribió: | Rosebell Kagumire (@RosebellK), mwandishi wa Uganda mtandaoni, aliandika: |
15 | 4000 niñas son deshonradas en el norte de #uganda cada año, ¡apuesto a que #kibuule piensa que es porque iban provocativas! | Watoto 4000 kaskazini mwa Uganda wananajisiwa kila mwaka. Nina hakika Kibuule anadhani ni kwa sababu watoto hao walivaa vibaya! |
16 | ¡Idiotas en el poder! | Wajinga walio madarakani! |
17 | Linda (@LindaNEK [en]), una empresaria ugandesa, ridiculizó la autoridad moral del ministro: | Wandera Samuel (@wandyBlackstig) anatafakari mawazo haya ya Waziri yametokea wapi: |
18 | | Kibuule anakaa kwenye kochi|anabadilisha badilisha chaneli za runinga | anajikuna sehemu nyeti| anafikiri -> kwamba wasichana waliovaa vimini wabakwe |
19 | #Kibuule es moralmente incompetente para dar una opinión digna de tener en cuenta sobre temas morales, sobre todo considerando el hecho de que es polígamo @DailyMonitor | Linda (@LindaNEK), mfanyabiashara wa ki-Ganda, alikejeli mamlaka ya kimaadili aliyonayo waziri: Kibuule hana ubavu wa kimaadili kutoa matamshi hayo yanayohusiana na Maadili hasa sote tukijua jamaa ana wake wengi @DailyMonitor |
20 | El periodista deportivo Mark Namamanya (@mnamanya [en]) observó: | Mark Namamanya (@mnamanya), mwandishi wa michezo, aliona alibaini: |
21 | En muchas sociedades, el payaso de #Kibuule estaría hoy dando una conferencia de prensa para anunciar su dimisión. | Katika jamii nyingi, mtu anayefanya kituko kama Kibuule angekuwa anafanya mkutano na waandishi wa habari kutangaza kujiuzulu. |
22 | Por desgracia, Uganda no es una de ellas. | Inasikitisha, si moja ya jamii hizo nyingi |
23 | Gordon G Ananura (@NgabiranoIV [en]) se unió a los que ridiculizaban al ministro: | Gordon G Ananura (@NgabiranoIV) alijiunga na wale waliokuwa wakimkejeli waziri: |
24 | @eshbankwesiga @iDEASUG: Sabía que el ministro #Kibuule era un chiste | Nilijua kuwa Kibuule ni kichekesho |
25 | No obstante, algunos ugandeses, como Ibrahim Batambuze (@TheBigPapaa), apoyaron los argumentos del ministro: | Hata hivyo, baadhi ya wa-Ganda kama Ibrahim Batambuze (@TheBigPapaa) waliunga mkono matamshi ya waziri: |
26 | @Mr_Bata_ estoy completamente de acuerdo con usted. | Ninaungana na wewe kwa asilimia 100. |
27 | Si deja la puerta abierta y le roban, ¿a quién hay que culpar por su estupidez? #Kibuule | Kama unaacha milango yako wazi na anakuja jambazi anakuibia, unamlaumu nani kwa ujinga wako? |