# | spa | swa |
---|
1 | Egipto: ¡Basboussa presidente! | Misri: Basboussa kwa Urais! |
2 | Foto tomada de la cuenta en Facebook de Bothaina Kamel. Participaba en una manifestación durante el Día Mundial en contra de la Corrupción | Makala hii ni sehemu ya habari maalumu tunazowaletea kuhusu Mapinduzi ya Misri ya Mwaka 2011. |
3 | “La ex presentadora de televisión y activista egipcia Bothaina Kamel anunció en su cuenta de Twitter la noche del viernes (ar), hora del Cairo, que quiere participar en las próximas elecciones presidenciales, con lo que se convierte en la primera mujer en anunciar su candidatura al más alto cargo de Egipto”, Manar Ammar. (en) | ” “Mtangazaji habari wa zamani wa televisheni ya Misri na mwanaharakati Bothaina Kamel alitangaza kwenye ukurasa wake wa twita usiku wa Ijumaa [ar] saa za Cairo kwamba ana mipango ya kugombea urais kwenye duru inayofuata ya uchaguzi, na kumfanya awe mwanamke wa kwanza kutangaza nia ya kutaka kuingia kwenye ofisi kuu nchini Misri”, Manar Ammar |
4 | Así fue como Manar Ammar informó la noticia de la postulación de Bothaina Kamel a las elecciones presidenciales egipcias. | Hivi ndivyo Manar Ammar alivyoripoti habari za Bothaina Kamel kugombea kwenye uchaguzi wa Urais wa Misri. |
5 | Bothaina tuitea con el nombre de @basboussa1, y recibió reacciones diversas de los usuarios de Twitter. | Kamel (@basboussa1) amepokea miitikio mchanganyiko kutoka kwa watumiaji wa twita. |
6 | Parece que Fares no podía creerlo, así que escribió si eran noticias confirmadas o rumores. | Mtumiaji wa Twita @FaresADLhakuweza kuamini habari hiyo, kwa hiyo akamwandikia Kamel akishangaa kama habari hizo zilikuwa zimethibitishwa ama zilikuwa ni uvumi tu: |
7 | @FaresADL: @basboussa1 ¿de verdad vas a postular a la presidencia? | @FaresADL: @basboussa1 ni kweli kabisa unagombea uraisi? |
8 | Fatma Emam, que es feminista, también escribió acerca de la noticia. | Fatma Eman, ambaye ni mtetezi wa usawa wa mwanamke aliandika kuhusu habari hizo: |
9 | @fatmaemam: Bothina Kamel la primera y única candidata para la presidencia en #Egipto, síganla en @basboussa1, en solidaridad. | @fatmaemam: Bothina Kamel mgombea mwanamke wa kwanza na wa pekee nchini #Egypt , mfuatilie hapa @basboussa1 , katika mshikamano #womenrights #jan25 |
10 | #WomenRights [#Derechosdelasmujeres] #Jan25 A Lara le parecieron buenas noticias, sea que esté convencida o no de votar por ella. | Picha iliyochukuliwa kwenye ukurasa wa facebook wa Bothaina Kamel; akishiriki maandamano wakati wa maadhimisho ya Siku ya Vita Dhidi ya Rushwa duniani |
11 | @FarawlaLawra: @basboussa1 estoy tan orgullosa de que postules - es un paso adelante para abrir la sociedad a iguales derechos (aun cuando mi voto no sea para ti). | Lara (@FarawlaLawra) aliiona habari hiyo kuwa nzuri, bila kujali ikiwa ameshawishika kumpigia kura ama la: @FarawlaLawra: @basboussa1 ninajisikia fahari na furaha unagombea -ni hatua moja mbele kuifungua jamii kuelekea kwenye haki sawa (hata kama ninaweza nisikupigie kura wewe) |
12 | Mahmoud Salem, conocido como SandMonkey, también escribió en demostración de apoyo. | Mahmoud Salem, anayefahamika pia kama @Sandmonkey, pia aliandika kumuunga mkono: |
13 | @Sandmonkey: @basboussa1 ana ma3aky ya rayessah 3ala fekra [Estoy contigo jefa, por cierto]. | @Sandmonkey: @basboussa1 ana ma3aky ya rayessah 3ala fekra. mpaka hapo kura yangu umepata |
14 | Hasta ahora tienes mi voto. En el siguiente video, Kamel anuncia sus planes de postular a la presidencia [ar]. | Katika video hii iliyopandishwa kwenye YouTube na mtumiaji moushebl1 tarehe 3 Aprili, 2011, Kamel anatangaza mipango yake ya kugombea Urais [ar]. |
15 | Algunas personas también comentaron en contra de su postulación a la presidencia. | Watu kadhaa walitoa maoni juu ya video hiyo hapo juu kupingana na nia yake ya kugombea Urais. |
16 | MyHamosa: Estoy en contra de que nos gobierne una mujer. | MyHamosa: Sikubaliani sisi kutawaliwa na mwanamke |
17 | Algeriangirls123: ¡no creo que siquiera vaya a tener el mínimo requerido de votos para entrar a las elecciones! | Algeriangirls123: Sidhani kama hata ataambulia kura za chini kabisa zinazotakiwa ili kuingia kwenye uchaguzi! |
18 | Finalmente, Radwa El-Shami cuestionó (en) la razón detrás de esta enorme cantidad de candidatos postulando a la presidencia en Egipto: | Radwa El-Shami alihoji sababu zilizo nyuma ya idadi kubwa ya wagombea wanaoutaka Urais nchini Misri: |
19 | El número está aumentando y seriamente estoy empezando a cuestionar las intenciones y motivos de cada persona que quiere ascender al trono de Egipto. | Idadi inaongezeka na nimeanza kujiuliza kwa makini dhamira na nia za kila mtu anayetaka kupanda kwenye kiti cha enzi cha Misri. |
20 | Parece como que no puedo servir a mi país a menos que esté en lo más alto de la jerarquía, a menos que sea presidente. | Inaonekana zaidi kana kwamba siwezi kuitumikia nchi yangu bila kushika nafsi za juu za utawala, bila ya kuwa rais. |
21 | Admito que también estoy cuestionando quién está anhelando poder y prestigio. | Ninakiri kwamba ninahoji pia wale wenye uchu wa madaraka na sifa binafsi. |
22 | Estoy preguntando por qué el señor Shafiq postula a la presidencia (¡al menos 10 millones de egipcios de 45 millones que tienen derecho a votar lo rechazaron como primer ministro!); por qué el doctor Amr Khaled está evaluando postular a la presidencia (todavía no confirmado); que piensa el bueno de Sheikh Hassan que hará por Egipto como su presidente (dicen que postula a la presidencia); por qué el señor Mortada Mansour imagina que puede ser presidente (¿va a gobernarnos con amenazas y a gritos?); por qué la señorita Bothaina Kamel quiere ser presidenta (¿feminismo?); por qué algunos están convenciendo al señor Naguib Sawiris a ser parte de esto (noticias de acá y de allá, pero personalmente dijo que Baradei es su figura favorita); y también pregunto cuál es la posición del doctor AlBaradei luego que las masas aceptaran las pobres enmiendas constitucionales por las que se niega a ser el presidente. | Ninahoji kwa nini Bw. Shafiq anagombea urais (wakati kiasi cha wa-Misri milioni 10 kati ya milioni 45 wenye sifa na haki ya kupiga kura walimkataa kama waziri mkuu!); kwa nini Dk. Amr Khaled anafikiria kugombea urais (bado haijathibitishwa); Jema gani Sheikh Hassan anafikiria kuwa itaifanyia Misri kama rais (kuna uvumi kuwa naye anawania urais); kwa nini Bw. Martada Mansour anajidhania kuwa anaweza kuwa rais (je atatutawala kwa vitisho na kupayuka?); kwa nini Bi. Bothaina Kamel anataka kuwa rais (ni harakati za usawa wa mwanawake?); kwa nini wapo watu wanamshawishi Bw. Naguib Sawiris kuwa sehemu ya harakati za uraisi (habari kutoka hapa na pale, lakini yeye mwenyewe alisema Baradei ni mtu anayempenda); na ninauliza pia ni upi msimamo wa Dk. AlBaradei baada ya umma kukubali mabadiliko yenye kilema ya katiba ambapo yeye aligoma kuwa rais? |
23 | Después Radwa continuó: | Halafu Radwa aliendelea: |
24 | No sé si soy solamente yo quien percibe pesimistamente la situación como absurda, y esta es la razón por la que escribo. | Sijui kama mimi ni mtu pekee ninayeikatia tamaa hali hii na kuiona kama kituko, na hii ndiyo sababu ninaandika. Ninapazia sauti kuguswa kwangu kwa sababu ninahitaji uhakikisho. |
25 | Estoy expresando mis preocupaciones porque necesito una tranquilidad. | Ninaomba maoni yenye weledi na ujuzi; Ninatafuta mtu atakayeongea kwa mantiki. |
26 | Estoy pidiendo una intuitiva opinión bien informada; busco a alguien que hable coherencias. | Makala hii ni sehemu ya habari maalumu tunazowaletea kuhusu Mapinduzi ya Misri ya Mwaka 2011.. |