Sentence alignment for gv-spa-20120423-116967.xml (html) - gv-swa-20120430-2905.xml (html)

#spaswa
1Senegal: Ninguna tolerancia para el Presidente Wade después de la pacífica derrota electoralSenegali:Rais Wade Aandamwa Hata Baada ya Kukubali Kushindwa Uchaguzi
2Mientras que el mundo exterior parece unánime en sus elogios para el saliente presidente senegalés Abdoulaye Wade y la democracia después del resultado de la pacífica elección en marzo de 2012, la blogosfera senegalesa ha sido más crítica del historial del ex Presidente Wade.Wakati ulimwengu wa nje ya Senegali unaonekana kushabihiana katika kumwagia sifa kemkem rais wa Senegali anayeondoka Abdoulaye Wade pamoja na kupongeza demokrasia iliyochukua nafasi baada ya matokeo ya uchaguzi uliojidhihirisha kuwa wa amani mwezi Machi 2012, ulimwengu wa blogu nchini humo umekuwa mkosoaji mkubwa wa rekodi ya Rais Wade.
3Los bloggers no han olvidado a las víctimas de la violencia pre-electoral, la violación de la libertad de prensa, y múltiples ejemplos de mal gobierno durante la presidencia de Wade del 2000-2012.Wanablogu hawaonekani kusahau athari na waathirika wa ghasia za kuelekea uchaguzi, kuingiliwa kwa uhuru wa habari na mifano mingine mingi ya utawala mbovu katika kipindi chote cha urais wa Wade tangu 2000-2012.
4Abdoulaye Wade hablando en New York en el 2002.Abdoulaye Wade akiongea Mjini New York mwaka 2002.
5Tomada por Marcel Bieri de Swiss Image.Picha ya Marcel Bieri wa Swiss Image.
6Compartida por World Economic Forum en Flickr (CC-BY-SA 2.0)Iliwekwa kwenye habari za Mkutano wa Uchumi wa Dunia kwenye Flickr (CC-BY-SA 2.0)
7Fabienne Fatou Diop escribe que Wade no tuvo más remedio que admitir la derrota ante el ex primer ministro y retador Macky Sall, en su post, “Senegal, 25 de Marzo de 2012, ¡Honor para nuestro pueblo!”Fabienne Fatou Diop anaandika kwamba Wade hakuwa na uchaguzi mwingine isipokuwa kukubali kushindwa na Waziri Mkuu wa zamani na mshindani wake Macky Sall katika posti yake “Senegali, tarehe 25 Machi 2012, Heshima kwa watu wetu!”
8[fr]:[fr]:
9No, Abdoulaye Wade, no estaba siendo democrático al telefonear a Macky Sall.Hapana, Abdoulaye Wade hakuwa muumini wa demokrasia wakati alipompigia simu Macky Sall (kumpongeza).
10Él no tenía otra opción.Hakuwa amebakiwa na uchaguzi mwingine wowote.
11Le impusimos esa opción el 23 de junio, le impusimos aquella opción en las manifestaciones contra su tercera candidatura a la presidencia.Tulimlazimisha afikie uamuzi huo siku ya uchaguzi tarehe 23, tulimlazimisha afikie uamuzi huo pale tulipoandamana kumpinga alipoonyesha nia ya kugombea urais kwa mara ya tatu.
12Él demostró desprecio en su apogeo con la violación de nuestra Constitución, al no atender nuestra indignación y en la represión de nuestra única y la última libertad que queda, el derecho a manifestarse.Alionyesha upuuzi wa hali ya juu kwa kutokuheshimu Katiba yetu, katika kutokujali hasira yetu na katika kukandamiza haki pekee na uhuru uliobaki, yaani kuandamana.
13En su blog, Mr. Boombastic PlO recuerda “El “reinado macabro” de Wade [fr]:Katika blogu yake Bw. Boombastic PlO anakumbuka “jinamizi ya utawala” wa Wade [fr]:
14La elección de Macky Sall no es el primer traspaso de poder en Senegal, que siempre ha sido una democracia.Kuchaguliwa kwa Macky Sall si makabidhiano ya kwanza ya utawala nchini Senegali, ambayo siku zote yamekuwa ya kidemokrasia.
15El tiempo de Wade en la oficina seguirá siendo un paréntesis desafortunado en la historia política de Senegal, un momento en el que las libertades fueron aplastados por el asesinato … Los periodistas y los opositores políticos fueron encarcelados (como en el caso de los jóvenes Socialistas, Malick Noel Seck y Barthélémy Diaz), y sobre todo, una época marcada por los asesinatos durante la crisis pre-electoral.Muda wa Wade madarakani utaendelea kuwa doa kwenye historia ya siasa za Senegali, wakati ambao uhuru ulikandamizwa kwa mauaji…waandishi wa habari na wapinzani wa kisiasa waliwekwa kizuizini (mfano suala la vijana wa wenye mrengo wa kijamaa Malick Noel Seck na Barthélémy Diaz) na zaidi ya yote, utakuwa ni wakati uliotambulishwa kwa mauaji kufuatia ghasia za kuelekea uchaguzi.
16Bandera senegalesa en la Plaza del Obelisco.Bendera ya Senegali katika eneo liitwalo de l'obélisque.
17Por Nd1mbee en FlickR con su autorización.Imewekwa kwenye mtandao wa Flickr na Nd1mbee imetumiwa kwa ruhusa
18En “Adiós Wade” [fr] Wirriyamu escribe:Katika blogu ya “Adieu Wade,” [fr] Wirriyamuanaandika:
19Con los años, Abdoulaye Wade, tuvo muchas oportunidades de prestar la más mínima atención a los deseos de su pueblo … No aprovechó ninguna de esas oportunidades.Kwa miaka mingi (aliyokaa madarakani), Abdoulaye Wade alikuwa na fursa ya kujali matakwa ya watu wake…Hakutumia fursa yoyote kati ya hizo.
20Por el contrario, en aquellas ocasiones en que no respondió con desprecio (haciendo afirmaciones tales como “Tengo una mayoría”, “Estas personas son cobardes”, o “Nada va a pasar”), respondió con agresión.Badala yake, wakati huo wote kama kuna mahali hakuitikia kwa dharau (akitoa kauli kama “nina umma nyuma yangu”, “Watu hawa ni wajinga,” au “hakuna kitakachotokea”), aliitikia kwa hasira.
21Haby Ba, en una entrada titulada “El Presidente Macky Sall” [fr], afirmó que la candidatura polémica de Wade para un tercer mandato privó al país de una verdadera campaña electoral:Haby Ba, katika posti yenye kicha cha habari “Président Macky Sall”, [fr] anaeleza kwamba mkanganyiko wa uamuzi wake wa kugombea urais kwa mara ya tatu kwa hakika uliinyima nchi kampeni za kweli za uchaguzi:
22Este año, deberíamos haber tenido una campaña sobre las opciones sociales, ¿Qué podemos hacer para reconstruir el sistema educativo senegalés, que está claramente la deriva?Mwaka huu, tungekuwa na kampeni za uchaguzi ambazo zingejikita kwenye masuala ya msingi ya kijamii; (kama vile) tufanye nini kuujenga upya mfumo wa elimu ya Senegali, ambao ni bayana unadidimia?
23¿Cómo podemos construir la solidaridad nacional para que los más empobrecidos no sólo puede recibir una educación, sino también tener atención médica?Tunawezaje kujenga umoja wa kitaifa ili raia maskini kuliko wote si tu wapate elimu, bali pia wapate huduma za afya?
24Estas preguntas no fueron abordadas en lo absoluto debido a que estábamos centrados en la necesidad de velar por la transparencia del sistema electoral.Maswali haya hayakushughulikiwa kabisa kwa sababu tulimezwa na hitaji la kuhakikisha uwazi unakuwepo katika mfumo wa uchaguzi.
25Wirriyamu [fr] dijo:Wirriyamu [fr] anasema:
26Al final, al insistir en ser candidato a la presidencia, Wade potencialmente alteró el curso de la historia de Senegal.Mwisho, kwa kung'ang'ania kugombea urais, wade ameharibu mwenendo wa historia ya Senegali.
27Él no permitió que la batalla justa de ideas que implica cualquier elección digna de ese nombre, tuviera lugar.Hakuruhusu ushindani wa haki wa mawazo, ambayo ni msingi wa uchaguzi wowote wenye hadhi ya kuitwa uchaguzi.
28La oposición llegó a tener que organizarse en torno a un único proyecto: deshacerse de Wade.Upinzani uliishia kujikita kwenye mradi mmoja: kumng'oa Wade.
29De este modo, Senegal ha demostrado que sabe muy poco acerca de los proyectos y que ella no sabe qué es lo que guarda su futuro, sólo que este futuro no será con Wade…Katika kufanya hivyo, Senegali imeonyesha kwamba inajua kidogo mno mambo ya mipango na kwamba haijui majaliwa yake, isipokuwa (labda moja tu) kwamba mustakabali wa nchi hiyo hautafungamana na Wade…
30Los bloggers son unánimes en sus conclusiones y en su demanda a que se haga justicia.Wanablogu wanakubaliana katika mahitimisho yao na katika namna yao ya kudai haki itendeke.
31Según Fabienne Fatou Diop [fr]:Kwa mujibu wa Fabienne Fatou Diop [fr]:
32No queremos que las lesiones y las vidas perdidas durante las manifestaciones contra la tercera candidatura de Abdoulaye Wade para la presidencia, sean en vano.Hatutaki majeraha na maisha yaliyopotea wakati wa maandamano dhidi ya hatua ya Abdoulaye Wade kugombea urais kwa muhula wa tatu yawe ni bure.
33Exigimos que aquellos que llevaron a cabo y aquellos que ordenaron estos crímenes sean llevados ante la justicia.Tunadai kwamba wale waliohusika na ghasia hizo na wale walioamuru uhalifu huu ufanyike wafikishwe kwenye mikono ya sheria.
34Haby Ba dijo [fr]:Haby Ba anasema [fr]:
35Los políticos son tan ajenos al hecho de que sus acciones tienen consecuencias, incluidas las consecuencias penales, que siguen saqueando este país.Wanasiasa hawatambui ukweli kwamba matendo yao yana matokeo, hii ikiwa ni pamoja na adhabu kwa mujibu wa sheria, kwamba wanaendela kuifilisi nchi hii.
36Sólo el sistema de justicia puede impedir que vuelvan a caer en la espiral de siempre.Ni mfumo wa sheria tu unaweza kutulinda kurudi kwenye mzunguko wa zamani.
37Mr. BoOmbastic PlO escribió [fr]:Bw. BoOmbastic PlO anaandika [fr]:
38Las familias de las víctimas creen que Wade y sus hombres no deberían poder librarse de “esta injusticia y que una luz deberia encenderse por sus muertos”.Familia za waathirika zinaamini kwamba Wade na wafuasi wake hawapaswi kukwepa uvunjifu mkubwa wa haki na kwamba wanapaswa kujiandaa kwa vifo vyao”.
39En Twitter, @astouka ha iniciado una petición a favor de una auditoría del gobierno saliente en Senegal, así como la puesta en marcha de nuevas investigaciones judiciales [fr].Kwenye mtandao wa twita, @astouka ameanza kutafuta uungwaji mkono kwa ajili ya ukaguzi wa hesabu za serikali inayoondoka madarakani nchini Senegali, pamoja na kufumuliwa kwa mfumo wa sheria wa nchi hiyo. [fr].