# | spa | swa |
---|
1 | Mozambique: Ataque a un candidato presidencial | Msumbiji: Shambulio Dhidi Ya Mgombea Urais |
2 | Los bloggers de Mozambique Carlos Serra [pt] y Paulo Granjo [pt] respondieron al ataque que sufrió el político Daviz Simango, en la ciudad portuaria del norte de Mozambique Nacala. | Wanablogu wa Msumbiji Carlos Serra [kireno] na Paulo Granjo [kireno] waliandika kuhusu shambulio dhidi ya mwanasiasa Daviz Simango lililofanywa kwenye mji wa kaskazini wa bandari ya Nacala. |
3 | Además de las reacciones de la blogosfera, el partido de Simango (@mdmwiki), informó del ataque por Twiter. | Pamoja na maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu, chama cha Simango (@mdmwiki), pia kilitumia huduma ya Twita kuandika kuhusu shambulio hilo. |
4 | Simango es el alcalde de Beira, y fundó su nuevo partido MDM a principios de este año, después de salir del partido tradicional de la oposición RENAMO. | Simango ni Meya wa Beira, na alizindua chama chake kipya cha MDM mapema mwaka huu, baada ya kutofautiana na chama cha upinzani cha RENAMO. |
5 | Sólo días atrás, él y su partido confirmaron competir por la presidencia y comenzar la campaña para la elección del próximo Octubre. | Siku chache zilizopita, yeye pamoja na chama chake walithibitisha mipango yao ya kugombea urais na kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa mwezi Oktoba. |
6 | Simango se dirigía a una reunión de su partido cuando el coche recibió los disparos de individuos en la multitud que arrebataron las armas de la policía. | Simango alikuwa anaelekea kwenye mkutano wa chama wakati gari lake lilipotupiwa risasi watu waliokuwa ndani ya umati uliokusanyika ambao walipora silaha za askari polisi. |
7 | Él escapó sin ser herido, pero los medios de comunicación reportaron al menos tres personas heridas, incluyendo a un oficial de la policía. | Alinusurika bila ya kudhurika lakini taarifa za vyombo vya habari zinasema kwamba watu watatu walijeruhiwa, akiwemo polisi. |
8 | Los reportes iniciales de los medios de comunicación independientes de Mozambique sugieren que los asaltantes eran miembros del RENAMO. | Taarifa za mwanzo kutoka vyombo huru vya habari nchini nMsumbiji zinaashiria kwamba watu waliopiga risasi walikuwa ni wanachama wa RENAMO. |