# | spa | swa |
---|
1 | Egipto: Huelga de Empleados del IslamOnline | Misri: Wafanyakazi wa IslamOnline Wagoma |
2 | Luego que la administración Qatarí anunciara que 250 empleados del ampliamente leído sitio de noticias IslamOnline (IOL) podrían ser despedidos, cientos de empleados, editores y periodistas tomaron las instalaciones a modo de protesta. | Baada ya uongozi mpya wa Qatari kutangaza kuwa wafanyakazi 250 watapunguzwa kazi katika mtandao wa habari unaosomwa sana wa IslamOnline (IOL), mamia ya wafanyakazi, wahariri, na waandishi wa habari walianza mgomo wa kuonyesha hasira yao. |
3 | La situación se intensificó rápidamente cuando la administración amenazó con llamar a la seguridad estatal para romper la toma, pero los empleados confirmaron que continuarían con la huelga hasta que sus demandas sean satisfechas. | Hali ilizidi kuwa mbaya kwa kasi sana pale uongozi ulipotishia kuita vikosi vya usalama ili kuvunjilia mbali mgomo huo baridi, lakini wafanyakazi walithibitisha kwamba walikuwa imara na kuwa wangeendelea na mgomo wao mpaka matakwa yao yatimizwe. |
4 | Es destacable que esta huelga es, tal vez, la primera vez en que los huelguistas utilizan eficiente y efectivamente los nuevos medios para llamar toda la atención necesaria para sostener su causa, utilizando desde contínuas actualizaciones de Twitter hasta transmisiones en vivo. | Pengine ni jambo linalostahili kutajwa kwamba huenda mgomo huu ni wa kwanza wa aina yake unaotumia kwa ufanisi na vizuri zaidi njia za kisasa za upashanaji habari ili kuvuta usikivu na uungwaji mkono, kuanzia na Twita inayoendelea mpaka mmiminiko wa habari wa hapo kwa hapo. |
5 | Nadia El Awady, una ex-periodista del IOL, siguió de cerca los hechos y publicó en su blog una declaración emitida por los empleados en huelga del IslamOnline: | Nadia El Awady, aliyekuwa mwandishi wa habari wa IOL, alikuwa akifuatilia kwa karibu hali ya mambo na alituma kwenye blogu yake tamko lililotolewa na wafanyakazi wa Islamonline: |
6 | La situación se ha intensificado miserablemente dentro de las oficinas centrales del IOL en El Cairo, luego que la administración Qatarí enviara abogados para hacerse cargo del edificio, con todas sus posesiones y documentos, e investigara a 250 empleados que enviaron una declaración a Sheikh Qaradawy, Presidente del periódico, quejándose por las injustas acciones de la nueva administración. | Hali imezidi kuwa mbaya ndani ya Makao Makuu ya IOL huko Cairo, baada ya kuwa menejimenti ya Qatari kutuma wanasheria kulishika jengo na mali zake zote pamoja na nyaraka, na kuwachunguza wafanyakazi 250 waliotuma tamko lao kwa Shehe Qaradawy, ambaye ni mwenyekiti wa Bodi, wakilalamikia vitendo visivyo vya haki vilivyofanywa na menejimenti mpya. |
7 | Algunas fuentes afirman que la razón oculta detrás de estas investigaciones a empleados es despedirlos, y de este modo quitarles sus derechos financieros. | Baadhi ya vyanzo vilidokeza kuwa sababu iliyojificha ya kuwachunguza wafanyakazi hawa ni kuwafukuza kazi kisha kuwapiga marufuku kudai haki zao zozote za kifedha. |
8 | Fuentes bien informadas dentro de la institución afirman que el objetivo de la investigación a los empleados es despedirlos arbitrariamente y luego confiscarles sus derechos financieros. | Watu walio vyanzo vya habari na walio na uhakika wa kile wanachokieleza ambao wamo ndani ya taasisi hiyo wanasema kwamba lengo la uchunguzi dhidi ya wafanyakazi ni kuwaondoa mara moja na kuwanyika madai yao mbalimbali ya fedha waliyo nayo. |
9 | Mientras que Tadamon Masr menciona [Ar] que la disputa puede deberse a que la nueva administración Qatarí pretende mudar las instalaciones centrales desde El Cairo a Doha, AbdelMoniem es escéptico [Ar] y se pregunta si no se trata de extremistas que quieren silenciar las voces moderadas de los sitios como Islam Online. | Kwa upande wake Tadamon Masr alieleza [Ar] kwamba mgogoro huo huenda umetokana na lengo la uongozi mpya wa Qatari kutaka kuhamisha makao makuu ya IOL kutoka Cairo kwenda Doha. AbdelMoniem alikuwa na wasiwasi [Ar] na alijiuliza kama ilikuwa ni njama za wenye siasa kali kutaka kunyamazisha sauti zinazotaka maelewano zaidi zilizo katika tovuti kama ile ya IslamOnline. |
10 | Zeinobia expresó una opinión similar a la de AbdelMoniem, al decir: | Zeinobia alitoa maoni yanayotaka kufanana na hayo kwa AbdelMoniem akisema: |
11 | Se dice que la nueva administración Qatari es muy conservadora y cree que el sitio web debe apegarse a los temas religiosos y remover otras secciones. | Inasemekana kwamba Uongozi mpya wa Qatari ni ule wenye msimamo wa kihafidhina unaoamini kwamba uendeshaji wa tovuti hiyo hauna budi kushikilia mitazamo ya kidini yenye msimamo wa kihafidhina na kuondolea mbali vipengele vingine. |
12 | En Twitter, Mohammed, otro ex periodista de IOL, comenzó a difundir las noticias al decir: | Kupitia Twita, mwandishi mwingine wa habari wa zamani wa IOL, Mohammed, alikuja na taarifa inayosema: |
13 | @MohammedY: Para los periodistas en Egipto y el mundo Árabe: Periodistas @#IslamOnline están siendo intimidados por la nueva administración para silenciar las malas prácticas de la compañía. | @MohammedY: Kwa waandishi walio Misri na ulimwengu wa Kiarabu: Waandishi wa habari wanaofanya kazi katika Islamonline wanatendewa vibaya na uongozi wao mpya ili kuwanyamazisha kutoa matamko dhidi ya vitendo vibaya vya uendeshaji kampuni. |
14 | @MohammedY: Cuando los trabajadores firmaron un petitorio afirmando sus problemas, la administración los puso bajo investigación. | @MohammedY: Kwa hiyo, pale wafanyakazi wanapotia saini maelezo kuhusu matatizo yanayowakabii, basi uongozi unawaweka wafanyakazi chini ya uchunguzi. |
15 | ¿Qué m****a pasa en #IslamOnline ? | Hivi jambo hili limesababishwa nini hapo Islamonline? |
16 | Abdullah El Shamy y Muhammad Ghafari, quienes se encuentran entre los huelguistas, realizaron emisiones en vivo, actualizaron contínuamente sus cuentas de Twitter y publicaron fotos del lugar. | Abdullah El Shamy na Muhammad Ghafari, ambao ni miongoni mwa wanaogoma, walikuwa wakishughulikia taarifa zinazoingia moja kwa moja, kwa hiyo walikuwa wakituma taarifa hizo moja kwa moja kwenye akaunti zao za Twita na kutuma picha za eneo hilo la kazi. |
17 | @Ghafari : Para quienes están involucrados, actualizaciones En Vivo sobre la huelga de empleados del #IslamOnline aquí: http://www.ustream.tv/channel/iol-on-air | @Ghafari: Kwa wale wanaoguswa na hali hii, ili kupata taarifa mpya kuhusu mgomo wa wafanyakazi wa Islamonline, tafadhali bofya hapa: http://www.ustream.tv/channel/iol-on-air |
18 | Ghafari no se olvidó de mencionar el rol vital que están tomando las mujeres en la huelga: | Ghafari hakusahau kueleza jinsi gani wanawake wanavyoshiriki katika kuupa mgomo huo nguvu: |
19 | No es necesario mencionar el rol vital que las mujeres tuvieron en esta toma, ¡incluso componiendo canciones! | @Ghafari #IslamOnline #mgomo #wanawake Hakuna sababu ya kueleza jinsi wanawake wanavyosaidia kuutia nguvu mgomo huu, zaidi ya hilo wanatunga nyimbo za hamasa pia! |
20 | Nadia El Awady actualizó durante todo el día a través de sus amigos en Twitter, donde mencionó: | Nadia El Awady vilevile alikuwa akiwapa taarifa rafiki zake kupitia Twita karibu kila dakika, alieleza: |
21 | @NadiaE : Las empleadas mujeres de #Islamonline hablan de pasar la noche en bolsas de dormir en su oficina para continuar con la huelga | @NadiaE: Mfanyakazi wa kike pale Islamonline analeza nia yake ya kulala ofisini kutumia begi la kulalia ili kuendeleza mgomo. |
22 | @NadiaE : el empleado de #islamonline @mos3abof pide a la audiencia hacer copias de seguridad del contenido del sitio web [la junta directiva de qatar está tomando el control y los planes para el website no son claros] | @NadiaE: #mfanyakazi wa islamonline, @mos3abof, anatoa wito wa wafuatiliaji kutoa uungaji mkono kwa yale yanayochapishwa na tovuti [mipango ya Bodi ya Qatar na uchukuaji wake haileweki] |
23 | El blogger egipcio Ahmed Shokeir expresó una opinión que casi todo el mundo siente, comentando de qué manera las herramientas de los nuevos medios están siendo usadas de una manera diferente esta vez: | Mwanablogu wa Misri, Ahmed Shokeir, alitoa maoni kwamba karibu kila mtu aliona, akielezea kuhusu zana za vyombo vya habari vya kisasa, jinsi vinavyotumiwa tofauti katika wakati huu: |
24 | Pienso que la toma de IslamOnline debe ser la primera en transmitirse en vivo en la red. | @Shokeir Nafikiri kuwa mgomo wa Islamonline huenda ukawa wa kwanza kutumwa moja kwa moja mtandaoni. |
25 | Creo que será una herramienta efectiva y difundida en el futuro cercano. | Naamini njia hii itakuja kuwa yenye ufanisi na kuwa zana itakayotumiwa sana katika siku za hivi karibuni. |
26 | Es importante destacar que un rumor se diseminó porTwitter, diciendo que EL Qaradawi podría renunciar, en palabras de Mohammed: | Pia inafaa kutaja kwamba kuna uvumi kwenye Twita kwamba huenda El Qaradawi akajiuzulu nafasi yake, hiyo ni kwa mujibu wa Mohammed: |
27 | @MohammedY: la administración en Qatar del #IslamOnline evadió las llamadas de Al-Qaradawi porque él quiere tomar partido por los empleados (a través de Fathi en IOL) | @MohammedY : #Menejimenti ya IslamOnline huko Qatar imekuwa ikikataa kupokea simu kutoka kwa Al-Qaradawi kwa sababu inamtuhumu kwamba alitaka kujiunga upande wa wafanyakazi (kupitia Fathi katika IOL) |
28 | Y fue ratificado por otro Tweet de Nadia: | Na hiyo ilipata uungaji mkono kutoka kwa mwanaTwita mwingine, Nadia: |
29 | @NadiaE: Motaz Al-Khateeb, productor del show del Sheikh Al-Qaradawi en Aljazeera habló con la secretaria del Sheikh, quien dijo que aún considera la renuncia. | @NadiaE: Motaz Al-Khateeb, ambaye ni mtayarishaji wa kipindi cha televisheni cha Shehe Al-Qaradawi's katika Aljazeera alizungumza na katibu muhtasi wa Shehe huyo akimkariri akisema kuwa bado anafikiria kujiuzuru. |
30 | Antes de dormir, Ghafari concluyó sus actualizaciones diciendo que no levantarían la huelga a menos que sus demandas sean satisfechas: | Kabla ya kwenda kulala, Ghafari alihitimisha utoaji taarifa zake za kila mara kwa kusema kwamba hawatasimamisha mgomo wao mpaka matakwa yao yote yatimizwe: |
31 | La huelga de empleados continuará hasta la mañana, hasta que se garanticen nuestros derechos de manera oficial | @Ghafari: #Mgomo wa wafanyakazi wa IslamOnline utaendelea mpaka asubuhi, yaani mpaka uamuzi ufanyike unaothibitisha kwamba haki zetu zipo palepale. |
32 | Puede encontrar más fotografías aquí. | Picha zaidi zipo hapa. |