# | spa | swa |
---|
1 | Kenia: Explosión estremece Nairobi, #NairobiBlast tendencia en Twitter | Kenya: Habari za Mlipuko Jijini Nairobi Zatawala Mijadala ya Twita |
2 | Una explosión golpeó [en] una de las principales avenidas de Nairobi, Moi Avenue, en la capital de Kenia la tarde del lunes 28 de mayo, Las investigaciones iniciales sugieren que la explosión fue el resultado de una falla eléctrica en la zona. | Mlipuko unaodhaniwa kuwa ni bomu umesababisha madhara katika moja ya barabara kuu za Nairobi, Moi avenue, katika mji mkuu huo wa Kenya mchana wa Jumatatu. Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba mlipuko huo ulitokana na hitilafu ya umeme kwenye eneo hilo. |
3 | El Comisionado de Policía de Kenia ha rechazado los rumores de ataques con bomba vinculados a Al-Shabaab. | Kamishna wa polisi wa nchi hiyo amekanusha tetesi kwamba mlipuko huo umetokana na shambulio la bomu linalohusishwa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab. |
4 | Kenia se ha visto golpeada por una serie de ataques con bombas y granadas [en] desde la incursión militar del país en Somalia en contra de Al Shabaab, llamada “Operación Linda Nchi” (“Operación defendamos el país” en suajili). | Kenya imekumbwa na mfululizo wa mabomu tangu majeshi ya nchi hiyo yaingie Somalia kupambana na kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab kwa kile kiichoitwa “Operesheni Linda Nchi”. |
5 | En Twitter, los cibernautas usan las etiquetas #NairobiBlast [explosión en Nairobi] y #MoiAvenueBlast [explosión en avenida Moi] para discutir la tragedia y distribuir información. | Kwenye mtandao wa twita, watumiaji wamekuwa wakijadili tukio hilo na kubadilishana taarifa kupitia alama ya #NairobiBlast na #MoiAvenueBlast. |
6 | Lugar de la explosión en Nairobi. | Eneo la mlipuko jijini Nairobi. |
7 | Foto distribuida en Twitpic por @JoeWMuchiri. | Picha imewekwa kwenye mtandao wa twitpic na @JoeWMuchiri |
8 | Por favor, quédense lejos: | Tafadhali kaa mbali: |
9 | @__RamzZy__: A menos que seas de la prensa, si no tienes nada que hacer cerca del lugar de los hechos, quédate lejos. | @__RamzZy__: Kama wewe si mwandishi wa habari, kama huna shughuli inayokulazimu kuwa karibu na eneo la tukio, kaa mbali. |
10 | Dejen que la policía y los equipos de rescate hagan su trabajo. | Waache polisi na timu za uokoaji kufanya kazi zao. |
11 | #MoiAvenueBlast | #MoiAvenueBlast |
12 | @cobbo3: Es peligroso que la gente se reúna en avenidas Moi y Kimathi luego de #MoiAvenueBlast. | @cobbo3: Ni hatari kwa watu kukusanyika kwenye mtaa wa Moi na Kimathi baada ya mlipuko huo. |
13 | Si es bomba terrorista, por lo general una segunda bomba está cerca para atacar a las multitudes. | Ikiwa mlipuko huo ni shambulio la kigaidi, mara nyingi bomu la pili laweza kulipuka kuangamiza maelfu |
14 | Responsabilidad de los medios: | Wajibu wa vyombo vya habari: |
15 | @jaydab: @mckenziecnn, estamos esperando ver y escuchar qué dirán acerca de #NairobiBlast. | @jaydab: @mckenziecnn, tunasubiri kuona na kusikia mtakachosema kuhusu mlipuko huu. |
16 | Informen tal como es y no exageren. | Tujuzeni hali ilivyo na sio kutia chumvi. |
17 | @CyrusNjoroge: Cuando los medios sociales aterrizaron en la ciudad, todos nos convertimos en ‘expertos'. | @CyrusNjoroge: Vyombo vya habari vya kiraia vilipotua mjini, sote tumekuwa “wataalam”. |
18 | Nunca esperamos los hechos. | Wala hatujisumbui kusubiri kusikia ukweli wa mambo. |
19 | #NairobiBlast | #Nairobiblast |
20 | @saddiqueshaban: Sinceramente espero que @MediaCouncilK esté viendo atentamente la conducta de los medios de comunicación en sus informes de #NairobiBlast. | @saddiqueshaban: Ninatarajia kwa dhati baraza la habari @MediaCouncilK linafuatilia kwa makini yanayofanywa na vyombo vya habari kipindi hiki wanaporipoti tukio hili #nairobiblast. |
21 | La resposabilidad es un imperativo. | Uwajibikaji ni kitu cha lazima |
22 | @Kevin2Tek: #NairobiBlast es ahora tendencia a nivel mundial. | @Kevin2Tek: Alama inayotumika kujadili tukio la mlipuko huo, #NairobiBlast, sasa inatawala gumzo la mtandao wa twita duniani kote. |
23 | Por favor, atentos con lo que tuitean, ¡no difundan pánico ni consientan mentiras! | Tafadhali kuwa makini na kile unachotuma kwenye mtandao huo, usisambaze hofu au kujadili uongo! |
24 | ¿Qué causó la explosión?: | Nini kimesababisha mlipuko?: |
25 | @iAMneshynsky: La gente debería dejar de llegar a conclusiones apresuradas y no decir que es un ataque de Al Shabaab… en este momento, podría ser cualquier cosa. | @iAMneshynsky: watu wasikimbilie kufanya mahitimisho na kuhisi ni shambulio la al shabaab…chochote kinawezekana katika tukio hilo #NairobiBlast |
26 | #NairobiBlast @careywinnie: Oh Dios, ¡¡espero que mis amigos de los puestos de películas estén bien y todos los demás!! | @careywinnie: Mungu wangu, ninadhani maafiki zangu wapenzi wa filamu wako salama na wote wanaoishi maeneo hayo!! |
27 | #NairobiBlast #moiavenue ¿Qué cuernos sucedió? | #NairobiBlast #moiavenue wtf happened? |
28 | @jowac50: RT #NairobiBlast Jefe de policía Mathew Iteere dice que la explosión la causó una falla eléctrica - Informes. | @jowac50: RT #NairobiBlast RT #NairobiBlast Mkuu wa Polisi Mathew Iteere anasema mlipuko ulisababishwa na hitilafu ya umeme -kwa mujibu wa taarifa mbalimbali |
29 | @Fionaakumu: Las palabras “estallidos” y “explosiones” deben ser reexaminadas. | @Fionaakumu: Maneno “mabomu” na “milipuko” yanaihitaji kuangaliwa upya. |
30 | ¿Desde cuándo se convirtieron en sinónimos? | Tangu lini maneno haya yakawa na maana inayofanana? |
31 | #MoiAvenueBlast | #MoiAvenueBlast |
32 | Irresponsabilidad del gobierno: | Kuokuwajibika kwa serikali: |
33 | @tonybkaranja: Realmente necesitamos un plan de manejo de desastres que no esté solamente en papel. #nairobiblast | @tonybkaranja: Tunahitaji sana mpango wa kudhibiti majanga ambao hautakuwa tu kwenye makaratasi #nairobiblast |
34 | @MisterAlbie: De nuevo nuestra falta de adecuada conciencia de los desastres y la falta de preparación nos muerde en la espalda. #Firehydrants [hidrante para incendios], etc. #MoiAvenueBlast | @MisterAlbie: Kwa mara nyingine tabia yetu ya kutokuwa na ufahamu sahihi na maandalizi dhidi ya matukio kama haya yanatugharimu #Firehydrants #MoiAvenueBlast |
35 | @TeamKonshens1: ¡¡Solamente muestra lo incompetentes que son nuestros equiops de respuesta a emergencias!! | @TeamKonshens1: Inaonyesha namna mwitikio wa vikosi vya Dharura ulivyo duni! |
36 | ¡Parece que estuviéramos en una película en televisión en vivo! | Inaonekana kama filamu kwenye runinga! |
37 | #NairobiBlast | #NairobiBlast |
38 | @iCabway: #MoiAvenueBlast nos recuerda por qué SE DEBE implementar la instalación de hidrantes en esta era complicada. | @iCabway: #MoiAvenueBlast tukio hili linatukumbusha ulazima wa kuwa na mfumo unaoaminika wa maji yakuzimia moto katika kizazi hiki chenye matatizo. |
39 | Las ciudades africanas no tienen esperanza en este respecto. | Miji ya ki-Afrika haina habari na umuhimu wa kuchukua tahadhari. |
40 | Saqueo en medio de la tragedia: | Wizi katikati ya Janga:: |
41 | @iAMneshynsky: Los saqueadores están haciendo lo que mejor saben en la Avenida Moi. #NairobiBlast | @iAMneshynsky:Wezi wanafanya kile wanachoweza kwenye mtaa wa Moi Avenue #NairobiBlast |
42 | @rmunene: Los kenianos están “sacando” zapatos y ropa de los puestos en la escena de la zona de la explosión. | @rmunene: Wa-Kenya wanasomba viatu na nguo kutoka kwenye maduka ya eneo la tukio. |
43 | #NairobiBlast #KTNLiveStream [transmisión en vivo de KTN] | #nairobiBlast #KTNLiveStream |
44 | Ineficiencia policial: | Udhaifu wa kiutendaji wa Polisi: |
45 | @ArybaStacks: No sé por qué la policía sigue dejando a la gente por toda la extensión de la avenida Moi… ¿Y si hay una segunda explosión? | @ArybaStacks: Sijui kwa nini polisi bado wanaruhusu watu kwenda eneo la tukio…itakuwaje kama kuna mlipuko mwingine? |
46 | #MoiAvenueBlast | #MoiAvenueBlast |
47 | @Mwanikih: Los policías están empeorando una situación mala al tratar de evacuar a la gente a la fuerza. | @Mwanikih: Polisi wanafanya hali hii ambayo tayari ni mbaya kuwa mbaya zaidi kwa kutumia nguvu kuwatawanya watu. |
48 | Ahora la gente está gritando “Mlikua wapi?” | Sasa hivi watu wanapiga kelele “Mlikuwa wapi?” |
49 | [¿dónde estabas?] #NairobiBlast | #NairobiBlast |
50 | La policía keniana dice [en] que 27 personas fueron heridas en la explosión y que están en tratamiento en diversos hospitales de la ciudad capital. | Jeshi la Polisi la Kenya limesema kwamba watu wapatao 27 wamejeruhiwa na mlipuko huo na wanaendelea na matibabu. |