# | spa | swa |
---|
1 | Reportero ciudadano de 14 años muere en Siria | Mwandishi Habari za Kiraia wa Miaka 14 Auawa Akiripoti Mapigano Nchini Syria |
2 | Omar Qatifaan, un niño de 14 años de edad, murió este 21 de mayo, mientras reporteaba encuentros entre el ejército sirio y el ejercito rebelde libre en un área al sur de Daraa al-Ballad, cerca de la frontera con Jordania. | Omar Qatifaan, Mwanaharakati wa Habari mwenye umri wa miaka 14, aliuawa Mei 21, 2013 wakati alipokuwa anaripoti mapigano kati ya Jeshi la Syria na waasi wanaopinga serikali ya nchi hiyo kusini mwa al-Ballad eneo la Syria karibu na mpaka na Jordan. |
3 | El proyecto mediático juvenil Syrian Documents [en] informó su muerte y el blog de noticias de Siria YALLA SOURIYA [en] lo denominó como un “Espíritu de Siria” | Nyaraka kuhusu Syria zilizotolewa na Mradi wa vyombo vya habari vya vijana ziliripoti kuhusu kifo chake, na blogu ya habari nchini humo YALLA SOURIYA ilimwita kijana huyo kuwa “Roho wa Syria”. |
4 | El conflicto en Siria, así como otras revueltas de la Primavera Árabe, han aumentado el número de ciudadanos reporteros que informan desde el terreno sobre el transcurso de la guerra entre las fuerzas a favor del gobierno y quienes se encuentran en contra. | Mgogoro wa Syria, kama vile Mapinduzi mengine yaliyozikumba nchi za Kiarabu, zimesababisha kuongezeka kwa waandishi wa habari za kiraia wanaoripoti kutoka katika kwenye uwanja wa vita kuhusu mgogoro unaoendelea kati ya majeshi yanayounga mkono serikali na yale ya waasi. |
5 | Muchos han sido detenidos, torturados y incluso asesinados mientras intentaban llevarle al mundo la historia de la revolución. | Wengi wamekuwa kizuizini, kuteswa, na hata kuuawa wakiwa katika jitihada za kuutangazia ulimwengu habari za mapinduzi. |
6 | Los niños han pagado un terrible precio durante este conflicto, con los miles asesinados durante los ataques hasta ahora. | Watoto pia wameumia kupindukia wakati wa vita, na maelfu wakiuawa wakati wa ghasia hadi wakati huu. |
7 | El activista de los medios Omar Qatifaan tenia 14 años cuando murió mientras cubría una batalla en Daraa, Siria. | Mwanaharakati wa Vyombo vya Habari Omar Qatifan alikuwa na umri wa miaka 14 alipouawa akiwa anaripoti habari za vita huko Daraa, Syria. |
8 | La foto es de la cuenta de twitter de @RevolutionSyria | Picha kutoka akaunti ya twita @RevolutionSyria |
9 | Otro activista mediático grabó un video de Qatifaan luego de su muerte. | Mwanaharakati mwingine wa vyombo vya habari alirekodi video ya Qatifaan mara tu alipouawa. |
10 | La secuencia fue publicada en YouTube por SyrianDaysOfRage [VIDEO EXPLÍCITO] | Video hiyo iliwekwa kwenye YouTube na SyrianDaysOfRage: [NI VIDEO INAYOTISHA]: |