# | spa | swa |
---|
1 | Bahréin: Niegan la entrada al país a periodistas en el aeropuerto | Bahrain: Waandishi wa Habari Wazuiwa Kuingia Wakiwa Uwanja wa Ndege |
2 | Este post es parte de nuestra cobertura especial de las Protestas de Baréin 2011. | Makala hii ni sehemu ya Makala zetu maalumu kuhusu Maandamano ya Upinzani Bahrain 2011. |
3 | Bahréin se despertó el miércoles pasado con una violenta ofensiva de la policía contra los manifestantes acampados en la emblemática rotonda Lulu (Pearl). | Bahrain iliingia kwenye vurugu kubwa zilizoambatana na polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji waliopiga kambi katika eneo muhimu la wazi linalohusudiwa sana liitwalo Lulu Jumatano iliyopita. |
4 | Ese mismo día por la tarde cogí un avión de Doha (Qatar) a Bahréin, en parte porque quería ver con mis propios ojos lo que está pasando en el país al que, en algún momento, consideré mi patria. | Mchana wa siku hiyo nilipanda ndege inayotoka Doha, nchini Qatar, kwenda Bahrain, kwa upande mmoja nikitaka kujionea mwenyewe nini kilikuwa kikitokea katika nchi hii ya kisiwa ambayo ilipata kuwa nyumbani kwangu. |
5 | A continuación podréis leer mi historia, en la que cuento con detalle cómo se desarrollaron los hechos: | Saa kadhaa baadaye nilijikuta kwenye ndege ya kurudi Doha, baada ya kunyimwa ruhusa ya kupita pale uwanja wa ndege. |
6 | Vista desde el aeropuerto internacional de Bahréin. | Hivi ndivyo habari hii yangu ilivyotokea: |
7 | Foto de stephen_bostock, usuario de Flickr (CC BY-NC 2.0). | Mandhari ya nje kutokea Uwanja wa Kimataifa wa Bahrain. |
8 | @omarc: Mmm, los tuits no funcionan. Estoy en el aeropuerto de Doha, de camino a Bahréin. | Picha ya Flickr na stephen_bostock (CC BY-NC 2.0). |
9 | Supongo que pronto podré saber si es cierto que el gobierno no está dejando entrar gente en el país | @omarc: Ala! twita kupitia ujumbe mfupi wa maneno hazifanyi kazi … nipo uwanja wa ndege wa Doha, kuelekea Bahrain. |
10 | @omarc: Me han dicho que tomara asiento al llegar al control de inmigración. | Nina imani tutajionea kwa macho yetu kama kweli serikali inawazuia watu kuingia |
11 | No me han dicho por qué, así que estoy esperando a ver qué me dicen… | @omarc: Baada ya kufika naamriwa kuketi ofisi ya Uhamiaji ya Bahrain. Sielezwi sababu, naendelea kusubiri watasema nini … |
12 | No sé qué es lo que les ha hecho sospechar… mi mezcla de etnias, los visados de Omán o Irak en mi pasaporte, o el patrocinador de mi antiguo permiso de residencia en Qatar… | Sina uhakika nini kiliwafanya wanitilie shaka - mchanganyiko wangu wa damu, viza kwenye pasi yangu ya kusafiria kutoka Oman kwenda Iraki, au mhisani wangu katika makazi yangu ya zamani kule Doha … |
13 | @omarc: Llevo en el control de inmigración una hora. Me han preguntado dónde trabajo…”Trabajabas para Al Jazeera, ¿no?” | @omarc: Nipo uhamiaji hapa Bahrain kwa saa 1, wananiuliza ninfanya kazi kwa nani… “Uliwahi kufanya kazi Al Jazeera, au siyo?” |
14 | Sí, ¿pasa algo? | Ndiyo, je, kuna tatizo? |
15 | “No, ningún problema”. | “Hakuna tatizo.” |
16 | @omarc: Ya llevo dos horas esperando en inmigración en el aeropuerto de Bahréin para poder entrar en el país. | @omarc: Tayari imeshatimu saa 2 bado nipo hapa @ dawati la uhamiaji Bahrain ili niruhusiwe kuingia nchini. |
17 | También hay periodistas de Reino Unido, Francia y Japón esperando. | Waandishi wa habari kutoka Uingereza, Ufaransa na Japani nao pia wapo wameketi. |
18 | @omarc: Han dejado entrar a mujeres de Ch 4 y de Radio Francia, así como a algunos hombres japoneses. | @omarc: Wanawake wanaofanya kazi Ch 4 & wale wa Redio Ufaransa (mmoja baada ya mwingine) na yule kijana Mjapani wameruhusiwa kuingia Bahrain. |
19 | Yo sigo esperando… | Naendelea kusubiri… |
20 | Se ha permitido la entrada a algunos periodistas, mientras que a otros (incluyendo a los de la BBC Árabe y del canal de noticias Al Hurra, financiado con fondos estadounidenses) no les han dejado [en] pasar. | Wakati baadhi ya waandishi wa habari waliruhusiwa kuingia, wengine - ikiwa ni pamoja na wale wa BBC ya Kiarabu na Al Hurra inayopata ufadhili wa Marekani hawa inasemekana walizuiwa kuingia. |
21 | El Ministro de Información ha pedido a Mohammed Jamjoom, periodista de la CNN, que deje el país. | Mohammed Jamjoom, ambaye ni mwandishi wa CNN aliamriwa na Wizara ya Habari kuondoka nchini. |
22 | @JamjoomCNN: No me han dejado entrar en Bahréin, así que estoy de vuelta en Abu Dhabi… #bahrain | @JamjoomCNN: Mimi nilitimuliwa kutoka Bahrain … sasa nimerejea Abu Dhabi … #bahrain |
23 | @JamjoomCNN: No me han explicado por qué no me han dejado entrar. Me han dicho que soy el único miembro del equipo de la CNN al que le han pedido que se vaya… #Bahrain | @JamjoomCNN: wala sikuelezwa sababu za kutimuliwa kwangu kutoka Bahrain … nilielezwa tu kuwa mimi ndiye mwandishi pekee katika timu ya wenzangu wa CNN niliyetakiwa kuondoka … #Bahrain |
24 | En este informe de la CNN [en] se puede ver a Jamjoon hablando sobre su experiencia en Bahréin . | Jamjoom anaweza kuonekana kwenye taarifa hii ya CNN akizungumzia kuhusu kile alichokionja kule Bahrain. |
25 | Alex Delmar-Morgan, corresponsal de WSJ en Doha, también fue detenido [en] cerca de la rotonda Lulu (Pearl) en Manama, mientras que Toula Vlahou, periodista de CBS, denunció ser objetivo [en] de las autoridades. | Alex Delmar-Morgan, ambaye ni mwandishi wa WSJ aliye nchini Doha, naye alishikiliwa kwa muda karibu na makutano ya barabara pale Lulu (Pearl) katika Manama, wakati mwandishi wa CBS Toula Vlahou ilitutolewa taarifa kwamba alikuwa akilengwa na mamlaka. |
26 | Mi experiencia fue la siguiente: | Kwa upande wangu: |
27 | @omarc: Llevo tres horas en el control de inmigración. Ahora dicen que el país no deja entrar a los visitantes, que Manama no es segura y que me vaya a casa. | @omarc: Ni saa ya tatu bado nipo uhamiaji Bahrain - sasa wanasema kwamba wageni hawaruhusiwi kuingia nchini, Manama si salama, na sina budi kurudi nyumbani. |
28 | @omarc: los funcionarios del control de inmigración en Bahréin me han pedido que acepte sus disculpas por no dejarme entrar en el país, pero dicen que, “en 2 o 3 días, todo habrá vuelto a la normalidad”. | @omarc: Maofisa wa uhamiaji wa Bahrain wananitaka radhi kwa kutoniruhusu kuingia nchini humo, lakini wanasema, “mambo yatakuwa shwari baada ya siku 2 hadi 3″. |
29 | @omarc: Me han devuelto mi pasaporte, después de darnos largas durante 5 horas, junto con una tarjeta de embarque para las 5.30 de la mañana…Qatar Airways, muy amablemente, me ha reservado otra plaza en el vuelo de las 11.25 de la noche | @omarc: Napata pasi yangu ya kusafiria baada ya saa 5, pamoja na kadi ya kuniruhusu kupanda ndege inayoonyesha saa 11.30 alfajiri … QA ilinifanyia utaratibu wa kusafiri kwa ndege ya saa 5.25 |
30 | Mientras esperaba en el control de inmigración en Bahréin no pude acceder a internet. Lo que hice entonces fue narrar los acontecimientos a medida que iban sucediendo en Twitter. | Nikiwa pale kwenye dawati la uhamiaji Bahrain, sikuwa na mawasiliano ya intaneti, badala yake niliendelea kutuma twita kupitia ujumbe mfupi wa siku kutokea palepale. |
31 | Al llegar a Doha me encontré con una avalancha de mensajes de respuesta a mis tuits, que iban de gente que mostraba su preocupación: | Baada ya kuwasili Doha, nilikuta msururu wa miitiko ya twita kuhusu tukio lililonipata, zikitoka kwa wale walioguswa: |
32 | @realrogerbird: @omarc Espero que estés sano y salvo | @realrogerbird: @omarc Tunakuombea usalama |
33 | a personas que me daban su apoyo: | Zikitoka kwa waungaji mkono: |
34 | @nabeelalmahari: @omarc suerte, tío. Espero que podáis llegar | @nabeelalmahari: @omarc nakutakia heri rafiki yangu, tunatumaini mtafaulu |
35 | @bhrabroad: @omarc podemos darte toda la información que necesitas incluso si estás en el aeropuerto #Bahrain | @bhrabroad: @omarc tunaweza kukupa taarifa zote unazotaka hapo uwanja wa ndege #Bahrain |
36 | También había mensajes de algunos escépticos: | Wapo waliokuwa na mashaka: |
37 | @Nninanina: @omarc eso demuestra que el régimen no quiere que nadie vea cómo se cometen crímenes contra manifestantes desarmados. cuál es la diferencia entonces entre #bahrain y libia, si allí también están utilizando las armas para atacar al pueblo | @Nninanina: @omarc hiyo inadhihirisha utawala hautaki yeyote aone uhalifu wanaoufanya dhidi ya waandamanaji wasio na silaha, je, kuna tofauti gani kati ya #Bahrain na Qaddafi ambaye ametumia silaha dhidi ya watu wake |
38 | @maljaya3: @omarc harán todo lo necesario para que, cuando llegues, sólo puedas ver lo que ellos quieren que veas. | @maljaya3: @omarc Utakaporudi tena, watakuwa wameshaandaa kitu ambacho watataka wewe ukione - maigizo fulani hivi |
39 | y de gente maleducada: | Na wengine walikuwa hawana adabu: |
40 | @HubiBahrain: @omarc a ver si te enteras de una vez… NO eres bienvenido en este país. Sois todos una panda de mentirosos | @HubiBahrain: @omarc pata ukweli wa mambo …. ninyi nyote HAMRUHUSIWI kuingia ninyi ni kundi la walaghai watupu |
41 | Muchas gracias a todos los que han intentado ayudarme, y les deseo buena suerte a todos los periodistas que están allí, intentando informar lo que está pasando en Bahréin en un momento tan difícil. | Asante sana kwa wote mliotaka kusaidia, na nawatakia kila la heri waandishi wa habari mliofaulu kuingia nchini humo ili kutuma taarifa kuhusu yanayoendelea nchini Bahrain hasa katika kipindi hiki kigumu. |
42 | Si queréis, podéis leer el relato de esta experiencia en Boing Boing [en], así como todos los tuits y reacciones a los mismos en Doha News [en]. | Unaweza kusoma nakala iliyo katika muundo wa simulizi ya habari hii kupitia Boing Boing, na vilevile seti kamili ta twita & miitiko kupitia Doha News. |