Sentence alignment for gv-spa-20120702-125708.xml (html) - gv-swa-20120708-3220.xml (html)

#spaswa
1Somalia: nueva Constitución genera profundas divisionesSomalia: Migawanyiko Mikubwa Kuhusu Katiba Mpya
2Somalia no ha tenido un gobierno central que controle a todo el país desde la caída de Mohamed Siad Barre en 1991.Somalia haijawahi kuwa na serikali kuu inayotawala nchi nzima tangu kuanguka kwa Muhammad Siad Barre mwaka 1991.
3El Gobierno Federal de Transición (GFT) [en] es el gobierno reconocido internacionalmente de la República Somalí.Serikali ya shirikisho ya mpito (TFG) ndiyo serikali ya Jamhuri ya Somalia inayotambulika kimataifa.
4Después de llevar a cabo discusiones políticas en etíope, los líderes de diversos partidos somalíes acordaron los pasos políticos a seguir [en] para dar fin al periodo de transición y elegir un nuevo presidente.Baada ya majadiliano ya kisiasa nchini Ethiopia, viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa vya Somalia walikubaliana kuchukua hatua za kisiasa ili kumaliza kipindi cha mpito na kumchagua Raisi mpya.
5Uno de los pasos que se resumen en un calendario detallado es la redacción de una nueva constitución.Miongoni mwa hatua zilizobainishwa katika ratiba changanuzi ni kuandaa muswada wa katiba mpya.
6Un comité de revisión técnica para la nueva constitución participó en una sesión de trabajo de cuatro días [en] en Nairobi:Kamati ya Ufundi ya Mapitio ya katiba mpya ilishiriki katika kikao cha siku nne mfululizo katika jiji la Nairobi:
7Retrato militar del general de división Mohamed Siad Barre, el presidente de Somalia que más duró en el poder.Picha ya Kijeshi ya Meja Jenerali Mohamed Siad Barre, Rais wa Somalia aliyetawala kwa muda mrefu kuliko wengine.
8Fuente: Biblioteca del Congreso de los Estados Unidos (dominio público)Chanzo: maktaba ya Congress (Kwa matumizi ya umma)
9Ha concluido en Nairobi una sesión de trabajo de cuatro días con el Comité de Revisión Técnica de los signatarios.Kikao cha siku 4 mfululizo kilichojumuisha waweka saini wa makubaliano, kimekwishahitimishwa mjini Nairobi.
10Esta sesión fue la continuación de la reciente reunión de los signatarios de Adis donde se acordaron la mayor parte de los temas constitucionales y se enmendaron algunas de las disposiciones -preparadas por la Comisión Independiente de la Constitución Federal- tras negociaciones políticas amigables entre los signatarios de la hoja de ruta para finalizar la transición, que se adoptó en Mogadiscio el pasado septiembre.Kazi hii ni ya ufuatiliaji wa yaliyotekelezwa katika kikao cha waweka saini cha hivi karibuni kilichofanyikia mjini Addis Ababa ambapo mambo mengi ya kikatiba yalikubaliwa na baadhi ya mapendekezo -yaliyoandaliwa na Tume Huru ya Katiba ya Serikali ya Shirikisho- yamerekebishwa baada ya makubaliano ya kisiasa ya amani baina ya waweka saini wa mpango huo wa amani wa kumaliza kipindi cha mpito, yaliyofanyika Mogadishu mwezi wa 9 mwaka jana.
11El mandato del Comité de Revisión Técnica, según el comunicado de Adis Abeba, es completar el proceso constitucional.Mamlaka ya kiufundi ya Kamati ya Mapitio, kwa mujibu wa tamko rasmi la Addis Ababa ni kukamilisha mchakato wa katiba.
12El Ministro de Asuntos Constitucionales, que convocó la reunión, explicó a los participantes y los medios de comunicación que “el camino hacia el fin de la transición está cada día más cerca y necesitamos trabajar en conjunto para producir una constitución que Somalia merezca y que sirva a sus habitantes”.Waziri wa Mambo ya Katiba ambaye ndiye aliyeitisha mkutano aliwaeleza washiriki pamoja na vyombo vya habari kuwa “hatua ya kuelekea mwisho wa kipindi cha mpito zinaendelea kuwapo kukaribia sana siku hadi siku, na tunapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kuipatia Somalia katiba inayoistahili na itakayowatumikia watu wa Somalia
13Miembros del Comité de Revisión Técnica en Nairobi.Washiriki wa kamati ya ufundi ya mapitio wakiwa mjini Nairobi.
14Foto cortesía de http://horn.so/Picha kwa idhini ya: http://horn.so/
15Mahad Abdalle Awad, viceministro de Planeación y Cooperación Internacional de Somalia, cree con optimismo que el país pronto tendrá una nueva constitución [en]:Mahad Abdalle Awad, Naibu Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa wa Somalia ana matumaini makubwa kwamba nchi hiyo katika muda mfupi ujao itapata katiba mpya:
16Las personas que buscan infundir miedo usan tácticas para asustar y para influir en la opinión pública con el fin de impedir el cambio y el progreso mediante la diseminación de información falsa acerca del anteproyecto de constitución y la reunión prevista de la Asamblea Constituyente.Waoga wanatumia mbinu za vitisho ili kushawishi maoni ya wengi yawe ni ya kuzuia mabadiliko na mchakato huu kwa kusambaza taarifa ambazo si sahihi kuhusu uundwaji wa katiba na kikao cha bunge la katiba kilivyopangwa.
17Los negativistas, escépticos naturales y gente cínica, habitualmente expresan negatividad acerca de los logros de otros y ven el cambio con pesimismo.Wale wasiotaka kuamini, na wenyewe wasiwasi kwa asili baina yetu, wamekuwa na tabia ya kuonesha mashaka na mafaninikio ya wengine na ambao si warahisi kupokea mabadiliko.
18La famosa cita de Dale Carnegie describe perfectamente la naturaleza de los negativistas: “Cualquier tonto puede criticar, condenar y quejarse, y la mayoría de ellos lo hace”.Nukuu maarufu ya Dale Carnegie inafafanua kwa usahihi kasumba ya wote wenye tabia za kupinga pale alipoandika “mjinga yeyote anaweza kukosoa, kushutumu na kulalamika, na wajinga wengi ndivyo wafanyavyo.”
19Estos negativistas a menudo difunden mentiras flagrantes para oponerse a cualquier cosa que otras personas hagan.Walalamikaji mara nyingi wanasambaza uongo kupinga kila kitu ambacho wengine wanakifanya.
20En el caso de la Asamblea Constituyente, afirman que la constitución solo puede ser aprobada por referéndum popular, sin tomar en cuenta el patente hecho histórico que la República Somalí misma fue fundada por la Constitución de 1960, que fue aprobada por una asamblea constituyente compuesta por solo 110 delegados en apenas 29 días, mientras que el reférendum público se llevó a cabo el 21 de julio de 1961, más de un año después.Kuhusu suala hili la Bunge la Katiba, wanasema kuwa katiba inaweza kuidhinishwa kwa kukubaliwa na wengi kupitia kura ya maoni tu bila kujali ukweli wa kihistoria ulio wazi kuwa Jamhuri ya Somalia yenyewe ilipatikana kwa katiba ya mwaka 1960, iliyoidhinishwa na bunge la katiba lililokuwa na wajumbe 110 tu, tena kwa mchakato uliochukua siku 29, ambapo mchakato wa kupata maoni ya wananchi ulifanyika tarehe 21 Julai, 1961, zaidi ya mwaka mmoja baadae..
21Sin embargo, Mohamed Ali Hassan, presidente del Consejo de Paz Somalí-Estadounidense, y Manuela Melandri, estudiante de doctorado en el University College de Londres, señalan que [en] la mayoría de los somalíes ven con profundo escepticismo el anteproyecto de constitución:Hata hivyo, Mohamed Ali Hassan, Mwenyekiti wa Baraza la Amani la Somalia-Marekani na Manuela Melandri, mwanafunzi anayesomea shahada ya uzamivu katika Chuo Kikuu cha London, waliweka bayana kuwa wasomali wengi wanauangalia muswada wa katiba kwa mashaka makubwa:
22Los somalíes no comparten el optimismo de la comunidad internacional, sino que ven con profundo escepticismo el documento, al que perciben como impuesto desde el exterior, lleno de fallos y fundamentalmente antidemocrático.Matumaini makubwa kwa jamii ya kimataifa hayaeleweki kwa wa-Somali wenyewe, ambao badala yake wanaiangalia rasimu hiyo kwa mashaka makubwa wakiiona kama iliyoandaliwa na wageni, yenye makosa na kimsingi isiyo ya kidemokrasia.
23Para entender esta dinámica, uno debe comenzar por cuestionar los hechos.Kuielewa hali hii, lazima mtu aanze kwa kuhoji masuala ya msingi.
24¿Qué hay de malo en la nueva constitución somalí y por qué su adopción genera resistencia por parte de somalíes cultos, figuras religiosas, secularistas, ex primeros ministros somalíes, mujeres, académicos y por las organizaciones de la diáspora somalí?Kitu gani hakiendi sawa katika mchakato wa katiba mpya ya Somalia na kwa nini ukamilishaji wa katiba hii umekuwa ukikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa wasomali walioelimika, watu maarufu wa dini, wale wasio katika mrengo wowote wa dini, Mawaziri Wakuu waliotangulia wa Somalia, wanawake, wasomi na hata jumuiya za wa-Somali waishio nje ya nchi?
25En primer lugar, hay desacuerdo respecto al contenido de la constitución y de sus disposiciones.Kwanza, kuna mambo yanayohusiana na maudhui ya Katiba na utekelezekaji wa mapendekezo yake.
26Por sobre todo, la cuestión del federalismo sigue generando profundas divisiones.Lililo kubwa kabisa, ni swali la hali ya kuwa shirikisho ambalo linabaki kuwa jambo linaloleta mpasuko mkubwa kabisa.
27Hay puntos de vista a favor y en contra de la adopción de una estructura federal en Somalia.Maoni yanaweza kuwa ya kuunga mkono na ya kupinga mpango wa Somalia kuwa na muundo wa shirikisho.
28El presidente somalí Sharif Sheid en Adis Abeba, Etiopía, durante la 12.a Cumbre de la Unión Africana, 2 de febrero de 2009.Rais wa Somalia, Sharif Sheikh akiwa Addis Ababa, Ethiopia, wakati wa mkutano wa 12 wa nchi huru za Afrika uliofanyaka Feb. 2, 2009.
29Fuente: gobierno federal de los EE. UU. (dominio público)Chanzo: Serekali ya shirikisho ya Marekani (Kwa matumizi ya Umma)
30Pero un somalí alega que la nueva constitución puede mejorarse en el futuro [en]; los somalíes no tienen tiempo de esperar por una constitución perfecta:
31Nos guste o no, cuando vemos imágenes de somalíes en todo el mundo y las comparamos con nuestra propia situación (al menos aquellos de la diáspora que vivimos en paz), ¿sentimos que nuestros hermanos y hermanas necesitan una constitución que les sirva ahora que están pasando por situaciones horribles?Tupende tusipende, tunapoona taswira ya watu wa Somalia ulimwenguni kote, na tukifananisha na hali yetu (angalau, wenzetu waishio nje ya nchi kwa amani), je ni kweli tunahisi kuwa hao kaka na dada zetu wanahitaji katiba inayoweza kuwasaidia hivi sasa kwa kuwa wanahanganika kujinasua na hali mbovu?
32Piensen en esto: maxay ku gaaraan mustaqbalka?Lifikirie hili: maxay ku gaaraan mustaqbalka?
33Debo decirles que yo no escribí esos artículos que se mencionan más arriba, yo no formo parte del grupo que produjo la nueva constitución y no estoy aquí para justificar si la nueva constitución es buena, mala o fea.Unapaswa kufahamu kuwa, sikuandika makala hizo za habari zilizotajwa hapo juu, mimi sio miongoni mwa kundi linalojadili katiba mpya na sipo hapa kwa nia ya kuhalalisha ikiwa katiba mpya ni nzuri, mbaya au ni mbovu.
34Lo único que quiero recordarles es que aquellos que están necesitados tal vez no tienen tiempo de esperar por una constitución perfecta y bonita; necesitan una que les sirva por ahora. Aún más importante, no estoy aquí para oponerme a ninguna idea, solo expreso mi punto de vista como cualquiera.Ninachotaka kuwakumbusha ni kuwa: wale walio kakika uhitaji wanaweza wasiwe na muda wa kusubiri katiba mpya isiyo na makosa na yenye mvuto; wanahitaji katiba itakayoweza kuwasaidia kupita katika mazingira waliyonayo hivi sasa; Tena lililo muhimu zaidi, siko hapa kupinga wazo la yeyote yule -ninatoa maoni yangu tu kama ambavyo na mwingine yeyote angeweza kufanya.
35No obstante, la mejor solución que veo, al menos en mi opinión, es que comencemos a discutir cómo mejorar las nuevas constituciones en el futuro.Pamoja na hayo, suluhisho bora zaidi ninaloliona, angalau kwa maoni yangu, hebu tuanze kujadili jinsi ya kuiboresha katiba mpya kwa ajili ya wakati ujao.
36Mohamud Uluso considera el anteproyecto de constitución [en] como “un trabajo a la carrera, con la versión más reciente solo disponible en lengua somalí, mientras varias versiones obsoletas o falsas circulan en la red”:Mohamud Uluso anauchukulia rasmu ya katiba kama “kazi inayoharakishwa, toleo la hivi karibuni zaidi likipatikana katika lugha ya kisomali pekee wakati rasimu nyingine za zamani au zile batili zikiwa zinazagaa katika mtandao wa intaneti”:
37Al parecer la hoja de ruta para Somalia, a la manera de la ONU, no es sino parte de un plan pérfido para mantener a Somalia y los somalíes en estado de agitación.Inaonekana kuwa mpango wa amani wa Umoja wa Mataifa unaoonekana kuwa ni wa busara kwa Somalia si chochote bali ni sehemu ya mkakati wa ulaghai ili kuiweka Somalia na wa-Somali katika matatizo.
38En lugar de liberar a los verdaderos somalíes, que necesitan y quieren seguir viviendo en y desarrollar su propio país y las comunidades dentro de Somalia, la constitución que se planea parece ser la manifestación de las ataduras perpetuas de la opresión interna y extranjera sobre los somalíes.Badala ya kuwakomboa wasomali halisi, wanaohitaji na wanaoendelea kuishi nchini mwao na kuendelea kuiendeleza nchi yao wenyewe na jamii zao ndani ya Somalia, rasimu hii ya katiba inaonekana kuwa ilani ya kuwakumbatia wageni na pia kuwakandamiza milele wazawa wa Somalia.
39- La mayoría de los somalíes y sus académicos dudan de que sea el mejor momento para producir una nueva constitución, durante una era de conflictos civiles y agitación en Somalia, y se preguntan por qué los participantes de la presunta comunidad internacional se han gastado millones de dólares para reinventar la rueda, mientras que la actual constitución somalí se podría simplemente enmendar si fuera necesario y se expresara de manera legal y representativa, reflejando así la verdadera y libre voluntad de los somalíes.Wasomali wengi pamoja na wasomi wao wanaonesha mashaka yao kuwa ni wakati muafaka wa kujihusisha katika mchakato wa kuunda katiba mpya katika kipindi cha migongano ya kiraia na matatizo ndani ya Somalia na ushangae ni kwa nini mamilioni ya dola yameshatumiwa na waongozaji watokanao na kile kinachojulikana kama jamii ya kimataifa ya kuiunda tena katiba, wakati katiba iliyopo ya Somalia ingaliweza kurekebishwa tu kama sababu yoyote halisi ingeweza kutolewa na tena kwa kufuata taratibu na pia kwa mfumo wa uwakilishi-inayotoa taswira ya kweli na utayari wa watu wa Somalia.
40- Según personas que participan dentro del proceso, la MGF (mutilación genital femenina) será permitida por la nueva constitución somalí, la cual será presentada para su adopción a selectos “líderes tradicionales”.- Kwa mujibu wa chanzo cha habari kilichopo ndani ya serikali ya mpito ya shirikisho (FGM) kwa sasa imeruhusiwa na katiba mpya ya Somalia iliyopendekezwa, ambayo itawasilishwa kwa utekelezaji kwa baadhi ya “viongozi wa jadi” waliochanguliwa.
41Un ardid típico de cómo la ONU y sus títeres quieren todo a su modo, o al modo que sus amos quieren.Ni utaratibu wa aina yake ambao umoja wa mataifa na washirika wake wanataka mambo yawe kwa kadiri ya wanavyotaka, au kwa kadiri ya wakubwa wao wanavyotaka iwe..
42Abduallhi Jamaa analiza diversos argumentos [en] acerca del anteproyecto de constitución que aparecen en línea, en la radio vernácula y en las reuniones y cafés de los pueblos:Abduallhi Jamaa anachanganua hoja mbalimbali kuhusu mswada huu wa katiba unaoonekana mtandaoni, katika redio zinazotangaza kwa lugha za ki-Somali na katika mikutano vijiji na hata migahawani:
43Los analistas dicen que la ley propuesta al parecer es un hito, pero uno que puede fragmentar aún más a Somalia y dividirla en miniestados y regiones autónomos y semiautónomos.Wachambuzi wanasema kuwa mswada wa sheria uliopendekezwa unaonekana kama hatua muhimu sana, lakini ambayo inaweza kuigawa zaidi Somalia katika maeneo mawili yanayojitegemea au yenye aina fulani ya kujitegemea, na hata kufikia kuwa na majimbo madogo madogo. --
44-- “Existe confusión absoluta.“Kuna mkanganyiko wa wazi kabisa.
45No ha habido educación cívica para comunicar la letra y el espíritu de las leyes propuestas y esto significa que la mayoría de la gente no está familiarizada con el contenido, y muchos más no han oído nada del proceso”, [Hassan Sheikh, líder del Partido de la Paz y el Desarollo] declaró a Somalia Report.Hakukuwa na elimu yoyote ya uraia ya kufafanua suala la muswada wa katiba pamoja na dhima ya sheria zilizopendekezwa na hii inamaanisha kuwa watu wengi hawana uhakika na yaliyomo (katika mswada wa katiba), wengi zaidi hawajawahi hata kuusikia mchakato wenyewe” yeye [Hassan Sheikh, kiongozi wa Chama cha Amani na Maendeleo, PPD) alilieleza shirika la Habari ya Somalia.
46- Entre los asuntos polémicos se incluyen el modelo de gobierno propuesto, el polémico asunto de los recursos naturales y la influencia religiosa.- Miongoni mwa mambo yanayojadiliwa ni pendekezo la mfumo wa serikali, mkanganyiko wa masualaa ya mali asili na ushawishi wa kidini.
47Algunos participantes alegan que el lenguaje del anteproyecto no es comprensible, lo que puede dar lugar a malas interpretaciones.Baadhi ya wadau wanasema kuwa lugha iliyotumika katika mswada haieleweki, jambo linaloweza kuleta tafsiri tofauti na ile iliyokusudiwa. --
48-- “El problema no es solo la disputa sobre el contenido, sino que se relaciona con la falta de representación pública.“Suala hapa sio kutokuelewana kuhusu maudhui yaliyomo. Suala hapa linahusiana na kukosekana kwa uwakilishi wa walio wengi.
49No quiero formar parte de una asamblea constituyente que no represente la visión y la misión de Somalia”, dijo el anciano tradicional Mohamed Hersi.Sitamani kuwa sehemu ya bunge la katiba ambalo haliwakilishi dira na malengo ya Somalia”, alisema kiongozi wa jadi, Mohamed Hersi..
50Google Ideas desarrolló un proyecto piloto [en] con el servicio somalí, de la división africana de Voice of America (VOA), para ayudar a los somalíes a presentar su opinión con solo unos cuantos clics.Mradi wa ‘Google Ideas' ulitengeneza mpango wa majaribio kwa kushirikiana na idhaa ya Somalia, Idaara ya Afrika ya Sauti ya Marekani (VOA) kuwasaidia wa-Somali kuandikisha maoni yao kwa njia rahisi kwa kubofya mara kadhaa tu.
51La encuesta muestra [en], entre otras cosas, que los somalíes quieren una Somalia que se base en los códigos civil y criminal de la charia, un gobierno central fuerte, y están divididos respecto a la inclusión de mujeres en el gobierno.Pamoja na mambo mengine, takwimu za maoni zinaonyesha kwamba, wa-Somali wanahitaji Somalia itakayozingatia misingi ya “Sharia” za kiislamu kwa makosa ya madai na jinai, serikali kuu iliyo imara na (wa-Somali) wamegawanyika juu ya hatua za kuwajumuisha wanawake katika muundo wa serikali.