# | spa | swa |
---|
1 | Mundo árabe: Cuestionan los planes de Romney para Medio Oriente | Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala |
2 | El discurso de Mitt Romney sobre política exterior ha sido debatido por internautas de todo el mundo árabe. | Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. |
3 | Los tuiteos que cuestionaban la política exterior en el Medio Oriente fueron apareciendo mientras Romney, candidato republicano a las elecciones presidenciales de EE.UU., hablaba en el Instituto Militar de Virginia. | Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. |
4 | Si sale elegido, Romney ha prometido seguir una política exterior más «comprometida», a diferencia de la fórmula de «esperar a ver qué pasa» que ha aplicado Obama, puesto que la región se encuentra sacudida por una «profunda agitación». | Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati. |
5 | También dijo que armaría [en] a los rebeldes sirios, al menos a los que comparten sus valores. | Alisema piaangewapa mafunzo ya kijeshi waasi wa Kisyria, angalau wale wenye mtazamo unaofanana na wake. |
6 | En Venezuela, la periodista Dima Khatib no está contenta. | Akiandika kutoka Venezuela, mwandishi Dima Khatib hakupendezwa na maneno hayo. |
7 | Tuitea [ar]: | Alituma twiti[ar]: |
8 | @Dima_Khatib: ¡¡¡Lo que nos faltaba era un candidato a la presidencia de EE.UU que utilizara a Siria en su campaña electoral para promoverse con el pretexto de que es mejor que Obama!!! | @Dima_Khatib: Tulichokikosa kwa muda sasa ni mgombea Urais wa Marekani kuitumia Syria katika kampeni zake za uchaguzi kwa lengo la kujitafutia umaarufu wa kisiasa kwa madai kwamba yeye ni bora kuliko Obama!!! |
9 | La trama se completa | Mkakati umekamilika |
10 | Y pregunta: | Anauliza: |
11 | @Dima_Khatib: ¿Queda alguien que no haya chupado la sangre de la revolución siria para sus propios intereses? | @Dima_Khatib: Kuna aliyebaki ambaye hajanyonya damu ya mapinduzi ya Syria kwa maslahi yake mwenyewe? |
12 | El argelino Imad Mesdoua bromea: | Raia wa Algeria Imad Mesdoua anasema: |
13 | @ImadMesdoua: #Romney conoce bien el MENA [Medio Oriente y Norte de África]. | @ImadMesdoua: #Romney anaifahamu vizuri Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. |
14 | Ha visto #Libya y ha pensado que es una buena idea, ¡armemos a los rebeldes en #Syria! | Aliiona #Libya na akapata wazo hilo alilonalo, kuwapa waasi wa #Syria mafunzo ya kijeshi! #letmeknowhowthatworksoutforyou (naomba kujua namna inavyowezekana kwako) |
15 | #letmeknowhowthatworksoutforyou Shadi Hamid, del Brooking Doha Centre de Qatar, escribe: | Shadi Hamid, kutoka Kituo cha Brooking Doha, nchini Qatar, anaandika: |
16 | @shadihamid: El discurso de Romney sobre Medio Oriente podría ser importante. | @shadihamid: Hotuba ya Romney kuhusu Mashariki ya Kati inaweza kuwa muhimu. |
17 | Esperemos que anime a Obama a aclarar su propia línea de acción, que hasta ahora ha sido tímida y vaga. | Angalau sasa tunaweza kutazamia hotuba hiyo imsukume Obama kufafanua sera yake, ambayo kwa kweli imekuwa haieleweki sawa sawa |
18 | Y añade: | Anaongeza: |
19 | @shadihamid: La cuestión del «liderazgo» contra el «liderazgo en la sombra» de EE.UU es real y no debe menospreciarse. | @shadihamid: Suala la Marekeni “kuongoza” au “kuongoza kutokea nyuma” ni halisi na halipaswi kupuuzwa. |
20 | Existen serias dudas sobre si EE.UU. podrá resolver los problemas y seguir teniendo poder en el mundo árabe. | Mashaka halisi kuhusu nguvu ya Marekani kutatua na kukaa katika nchi za ki-Arabu. |
21 | La activista de derechos humanos de Bahréin, Maryam Al Khawaja, dice: | Mwanaharakati wa haki za binadamu wa Bahraini Maryam Al Khawaja anasema: |
22 | @MARYAMALKHAWAJA: A juzgar por sus afirmaciones, #Romney será un completo desastre para los #humanrights [#derechoshumanos] en el #GCC [Consejo de Cooperación del Golfo], incluso más que #Obama… #bahrain | @MARYAMALKHAWAJA: Kwa kupima matamshi yake tu, #Romney atakuwa janga kubwa kwa masuala ya haki za binadamu katika Baraza la Ushirikiano la Ghuba [Gulf Cooperation Council], zaidi sana kuliko #Obama… #bahrain |
23 | Y el editor de gestión de política externa Blake Hounshell está de acuerdo: | Na Mhariri Mtendaji wa Sera za Nje Blake Hounshell anakubaliana na hayo: |
24 | @blakehounshell: Romney y Obama parecen estar de acuerdo en un punto: Dejar a Bahréin fuera de la lista de revoluciones que apoya América. | @blakehounshell: Kitu kimoja ambacho Romney na Obama wanaonekana kukubaliana: Kuindoa Bahrain katika orodha ya mapinduzi ambayo Marekani inayaunga mkono. |
25 | Mientras que la catarí Shayma Al-Naimi, que estudia en EE.UU., tuitea: | Wakati raia wa Qatar Shayma Al-Naimi, anayesoma nchini Marekani, alitwiti: |
26 | @iShayma: ¿¿¿¿¿De verdad que #Romney quiere hablar de los «antecedentes americanos» en la historia pacífica????? | @iShayma: #Romney anataka kweli kuzungumzia “rekodi ya Marekani” katika historia ya amani???? Na anaongeza: |
27 | @iShayma: ¡Honradamente, no puedo creer lo que #Romney está diciendo ahora mismo! | @iShayma: Kwa dhati kabisa siwezi kuamini kile anachokisema #Romney kwa sasa! |
28 | Absolutamente vergonzoso. | Inakera kwa kweli. |
29 | Es triste saber que existe gente con esa mentalidad. | Inasikitisha kujua kwamba watu wenye mtazamo kama wake nao wapo. |
30 | El palestino Iyad El-Baghdadi, que tuitea desde Dubai, señala: | Mpalestina Iyad El-Baghdadi, anayetwiti akiwa Dubai, anaangaliza: |
31 | @iyad_elbaghdadi: La última vez que los EE.UU. mostraron algo de «liderazgo en Medio Oriente» murieron 600 000 iraquíes. #Romney | @iyad_elbaghdadi: Mara ya mwisho Marekani imeonyesha “Uongozi katika Mshariki ya Kati”, wa-Iraq wapatao 600,000 walipoteza maisha yao. |
32 | Y propone un compromiso: | Na anapendekeza suluhu: |
33 | @iyad_elbaghdadi: La mitad de mi timeline dice #Obama es un asco, y la otra mitad dice #Romney es un asco. | @iyad_elbaghdadi: Nusu ya yaliyoandikwa kwenye ukurasa wangu inasema Obama hafai, na nusu nyingi inasema Romney hafai. |
34 | Chicos, estoy de acuerdo con vosotros. | Jamani, ninakubaliana na ninyi. |