# | spa | swa |
---|
1 | Salafistas atacan hogares chiítas en Egipto, matan a cuatro | Misri: Wasalafi Washambulia Makazi ya Washia, Wanne Wauawa |
2 | Cuatro adeptos egipcios de la fe chiíta fueron asesinados el domingo 23 de junio en Egipto, cuando la casa en la que estaban reunidos fue atacada por salafistas, después de dos semanas de instigación contra los chiítas. | Watu wanne nchini Misri ambao ni wafuasi wa imani ya Shia wameuawa nchini humo hii leo mara baada ya nyumba waliyokuwa wanakutania kushambuliwa na Waislam wenye msimamo mkali , hali iliyotokana na uchochezi dhidi ya watu wa imani ya Shia. |
3 | Según varios informes, la casa donde los chiítas se reunían, en Giza, El Cairo, fue atacada e incendiada. | Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, nyumba ambayo washia waliyokuwa kikikutania huko Giza, jijini Cairo, ilishambuliwa na kuchomwa moto. |
4 | Al Badil News cita a un testigo del depósito de cadáveres que dijo [ar] que uno de los fallecidos estaba masacrado y los otros tres tenían heridas en la cabeza. | Kwa mujibu wa habari kutoka Al Badil, mtu mmoja alikaririwa kutoka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti[ar] ambaye alisema kuwa, mmoja kati ya watu waliouawa kwa kuchinjwa na wengine watatu walijeruhiwa vibaya vichwani mwao. |
5 | El horrible incidente desató la ira en línea. | Tukio hili la kuhuzunisha liliibua hasira kwa watumiaji wa mtandao wa intaneti. |
6 | Hazem Barakat documentó el crimen, compartiendo fotografías sangrientas y un video del ataque (Advertencia: el video [ar] muestra imágenes gráficas) en línea. | Hazem Barakat aliandaa waraka wa tukio hili la kinyama, aliweka picha za watu walioonekana kutokwa na damu nyingi pamoja na kuweka video inayoonesha shambulio hili (Warning: Graphic video) mtandaoni. |
7 | En Twitter, dijo que fue amenazado [ar] por compartir el incidente del que fue testigo. | Katika ukurasa wa Twita, anasema kuwa alitishwa kwa kuweka mtandaoni tukio hili alilolishuhudia. |
8 | Y añadió: | Anaongeza [ar]: |
9 | @7azem122 [ar]: Estoy dispuesto a declarar ante la Fiscalía y voy a decir lo que pasó en detalle y voy a decir que los clérigos fueron los que instigaron este crimen | @7azem122: nipo tayari kuthibitisha kwa mwendesha mashitaka wa umma na nitasema kwa kina kile kilichotokea na nitataja wazi kuwa makasisi ndio waliochochea mauaji haya. |
10 | La gente se reúne en el callejón en el que está la casa donde los chiitas fueron asesinados en El Cairo. | watu wakiwa wamejikusanya katika barabara nyembamba karibu na nyumba ambayo washia hao walipouawa leo huko jijini Cairo. |
11 | Fotografía compartida en Twitter por @7azem122 Y continuó: | Picha iliwekwa katika mtandao wa Twita na @7azem122 |
12 | @7azem122 [ar]: La instigación contra los chiítas empezó hace dos semanas en todas las mezquitas y hoy ejecutaron el plan. | @7azem122: Uchochezi dhidi ya watu wa imani ya Shia ulianza wiki mbili zilizopita katika misikiti yote na siku ya leo wamekamilisha mpango wao. |
13 | Esos clérigos son hijos de perra. | Makasisi hao ni watoto wa Mbwa. |
14 | Mataron a gente con niños pequeños | Waliwatumia watoto kwenye mauaji haya ya kikatili. |
15 | El domingo por la tarde tuiteó: | Masaa matano yaliyopita aliTwiti: |
16 | @7azem122 [ar]: Los salafistas han comenzado a romper el techo de la casa en la que están los chiítas. | @7azem122: Waislam wenye msimamo mkali wameanza kuvunja paa la nyumba walipo watu wa imani ya Shia. |
17 | Es una escena surrealista. | Tukio hili, kama vile ni la kusadikika, lakini ndio hali halisi. |
18 | La policía permaneció inactiva mientras salafistas atacaban una casa donde se reunían chiítas egipcios, dice Hazem Barakat (@7azem122) | Hazem Barakat anasema kuwa, polisi hawakutimiza wajibu wao kufuatia Salafists kushambulia nyumba waliyokuwa wakikutania waumini wa Shia huko Misri (@7azem122) |
19 | También afirmó que la policía, incluyendo oficiales, se quedó parada cerca y viendo cómo se producía el linchamiento. | Pia aliwatuhumu askari polisi pamoja na maafisa wengine kuwa walifahamu fika tukio lile na pia walishuhudia mauaji yale. |
20 | El incidente fue recibido con ira en Internet. | Tukio hili liliwaghadhabisha watumiaji wengi wa mtandao wa intaneti. |
21 | Dr Bassem Youssef, presentador de un programa satírico de televisión, tuiteó: | Mwandishi wa Tashtiti, Daktari Bassem Youssef anatwiti: |
22 | @DrBassemYoussef: Hoy es un chiíta, mañana un sufí, y luego un copto, y antes de él un bahaí. | @DrBassemYoussef: Leo ni kwa waumini wa Shia; kesho itakuwa Sufi, na kisha waumini wa Kopti, na kabla yake Bahai. |
23 | Después será un musulmán que no esté de acuerdo con la forma en que desean implementar la Sharia (enseñanzas islámicas) con su ideología y después será una persona cuyo aspecto no les gusta | Kisha itakuwa ni zamu ya waislam ambao hawakubaliani na namna usimamiavyo sheria ya sharia (mafundisho ya kiislam) ikilinganishwa na msimamo wako na kisha itakuwa zamu ya mtu ambaye hapendezwi tu na muonekano wake. |
24 | La bloguera egipcia Zeinobia compartió una idea similar: | Mwanablogu wa Misrir Zeinobia alitoa mawazo yafananayo na yaliyotangulia kusemwa: |
25 | @Zeinobia [ar]: Y hoy son los chiítas y mañana tu vecino que no está de acuerdo contigo, política e intelectualmente | @Zeinobia: na leo ikiwa ni kwa waumini wa shia, kesho itakuwa kwa jirani yako ambaye mmetofutiana kisiasa na kiweledi. |
26 | Ahmed Abou Hussein preguntó: | Ahmed Abou Hussein anauliza: |
27 | @abouhussein7 [ar]: Cuando tu clérigo [el presidente Mohamed Morsi] dice que los manifestantes son infieles y que los chiítas son impuros, no te sorprendas cuando les maten. | @abouhussein7: Kasisi wako [Rais Mohamed Morsi] anasema kuwa, waandamanaji ni wapagani na kuwa waumini wa Shia ni wafuska na hivyo usishangae wanapouawa. |
28 | Morsi, la pregunta no es si usted ha perdido su legitimidad. | Morsi, swali siyo labda umeshapoteza uhalali kama Rais. |
29 | La pregunta es: ¿cuántas veces ha perdido usted su legitimidad? | Swali ni kuwa, ni mara ngapi umeshapoteza uhalali kama Rais? |
30 | Ahmad Khalil estaba sorprendido por la manera en que la gente está razonando el asesinato: | Ahmad Khalil anashangazwa na jinsi watu wanavyoyachukulia mauaji: |
31 | @ahmad_khalil: Los salafistas han matado a cuatro chiítas. | @ahmad_khalil: Wakereketwa wa harakati za Kiislam wameshawaua waumini wanne wa Shia. |
32 | Lo sorprendente es que hay algunos entre los que condenan el acto que dicen que derramar la sangre de un musulmán es haram [prohibido en el Islam]. | Kinachoshangaza ni kuwa kuna baadhi ya watu ambao miongoni mwao ndio wanaolaani kitendo hiki na kwa upande mwingine watu hawa wanaamini kuwa kumwaga damu ya Muislam ni Haramu (yaani hairuhusiwi katika Uislam). |
33 | Es como si derramar la sangre de un cristiano fuera halal (aceptable en el Islam]. | Yaani ni kama vile, kumwaga damu ya Mkristo ni halali (yaani inaruhusiwa katika Uislam). |
34 | Estas ideas sectarias nos afectaron a todos. | Mawazo ya kimadhehebu ya aina hii yamemtesa kila mmoja. |
35 | Sherif Azer señaló: | Sherif Azer aandika [ar]: |
36 | @sherif_azer [ar]: Hubo muchos incidentes y declaraciones que se han producido en los últimos tiempos, que prepararon el terreno para el ataque contra los chiítas en Egipto. | @sherif_azer: kuna matukio mengi na kauli zilizotokea kipindi fulani kilichopita yaliyokuwa sehemu ya matayarisho ya tukio la kushambuliwa kwa waumini wa Shia huko Misri. |
37 | No estar preparado para tal incidente es un delito en sí. | Matayarisho ya tukio hili hayachukuliwi kama ni kosa la jinai. |
38 | Y Adel Salib se preguntó por qué la gente se sorprende de que los chiítas estén siendo atacados en Egipto cuando la policía atacó previamente -y mató- a egipcios coptos: | Na Adel Salib anashangaa ni kwa nini watu wanapatwa na mshituko kufuatia kushambuliwa kwa waumini wa Shia huko Misri wakati kabla ya hapo polisi waliwashambulia na kuwaua wakristo wazawa wa Misri: |
39 | @Adel_Salib: Alguien se sorprende de que la policía estuviera mirando mientras se asesinaba a los chiítas, cuando hace dos meses la policía atacaba la catedral. | @Adel_Salib: mtu fulani anaweza kushangazwa kuwa polisi walikuwa wakishuhudia wakati waumini wa Shia walipokuwa wakiuliwa, wakati kwa upande mwingine miezi miwili iliyopita, polisi walishambulia Parokia. |
40 | ¿Estás bajo un hechizo o eres simplemente estúpido? | Umelaaniwa au ni upumbavu? |
41 | Captura de pantalla de un tuiteo por Mohammed Saber, presentador en una televisión egipcia, que celebra el asesinato de chiitas en Egipto. | picha iliyopigwa kutoka kwenye Twiti iliyowekwa na Mohammed Saber, ambaye ni mtangazaji na msimamizi wa matangazo katika Televisheni ya Misri akisherehekea mauaji ya waumini wa Shia waishio Misri. |
42 | Fotografía compartida por @Gemyhood en Twitter Ali añadió: | Picha imewekwa na @Gemyhood katika mtandao wa Twita |
43 | @ali4592000: Te enfadas porque musulmanes están asesinando sunitas en Myanmar y te alegras de que estpen quemando vivos a musulmanes chiítas en Egipto y que estén profanando sus cadáveres. | @ali4592000: una hasira kuwa waumini wa kiislam wa Sunni wanauawa huko Burma na kuwa na furaha kuwa waumini wa kiislam wa Shia wanachomwa moto wakiwa hai nchini Misri na kisha miili yao kunajisiwa? |
44 | Necesitas ver a un buen veterinario. | Unapaswa kumtafuta daktari mzuri wa wanyama. |
45 | Rawah Badrawi compartió algo de historia: | Rawah Badrawi ashirikisha historia fulani: |
46 | @RawahBadrawi: Cairo fue fundada por los chiítas, neandertales. | @RawahBadrawi: Kairo ilijengwa na watu wa Shia enyi watu msiostaarabika. |
47 | Ellos establecieron la mitad de su patrimonio, incluyendo Al Azhar. | Walianzisha nusu ya maeneo ya Urithi wa Kairo ikiwa ni pamoja na Al Azhar. |
48 | Y la bloguera yemení Noon Arabia concluyó: | Naye mwanablogu wa Yemeni, Noon Arabia anahitimisha: |
49 | @NoonArabia: Estamos volviendo a la edad de Jahiliyya (ignorancia). | @NoonArabia: We are returning to the age of Jahiliyya [ignorance]. |
50 | El Islam es inocente de la sangre que se derrama hoy en Egipto, Líbano y Siria | Uislam hauna hatia kwa watu wanaouawa huko Misri, Lebanon na Syria. |
51 | Por supuesto no todo el mundo se horrorizó por el ataque. | Kwa kweli, siyo kila mmoja aliyeshitushwa na shambulizi hili. |
52 | El bloguero Mohamed Bashir compartió el tuit de un presentador en la televisión egipcia llamado Mohammed Saber, que celebró el asesinato de los chiitas y pedía más muertes. | Mwanablogu Mohamed Beshir aweka Twiti ya mtangazaji wa Televisheni ya Misri ajulikanaye kwa jina la Mohammed Saber, ambaye anasherehekea mauaji ya waumini wa Shia na kutaka wengine zaidi wa shia wauawe. |
53 | @Gemyhood [ar]: Este es un presentador en la televisión [estatal] egipcia, feliz por el asesinato de chiítas. | @Gemyhood: Huyu ni mtangazaji wa Televisheni ya Taifa ya Misri akifurahia mauaji ya waumini wa Shia |