Sentence alignment for gv-spa-20080724-2412.xml (html) - gv-swa-20080906-4.xml (html)

#spaswa
1La determinación de una bloguera de ayudar al Bebé Kamba en MadagascarNia ya Mwanablogu Mmoja Kumsaidia Mtoto Kamba huko Madagaska
2Si usted intenta estar al día con las noticias de Madagascar, es mas que probable que lea regularmente el Madagascar Tribune.Ikiwa unataka kwenda sambamba na habari mpya mpya kutoka Madagaska, inawezekana kabisa ukawa ni msomaji wa Madagascar Tribune.
3Y si usted de hecho es un suscriptor, habrá notado recientemente una pequeña noticia del periodista Herimanda R sobre una rara y exitosa operación que se llevó a cabo en el departamento de neurocirugía del Hospital de Ravoahangy el 10 de junio.Na kama wewe ni mdau wa gazeti hilo, hivi karibuni yawezekana ulishakutana na habari iliyoandikwa na mwandishi wa habari Herimanda R kuhusu upasuaji wa maradhi ya nadra na mafanikio yake ambao ulifanyika katika kitengo cha tabibu za mishipa ya fahamu cha Hospitali ya Ravoahangi mnamo tarehe 10 Juni.
4Tombotsara Ambinindrazana de un año de edad, mas conocido como “Bebé Kamba” entre los blogueros alrededor del mundo, nació con un raro caso de meningoencefalitis frontal-nasal, la cual genera una gran protuberancia en su frente, como puede verse en la foto siguiente:Mtoto wa mwaka mmoja Tombotsara Ambinindrazana, ambaye milele atajulikana kwa jina la “mtoto Kamba” ndani ya jamii ya wanablogu duniani, alizaliwa na hitilafu nadra sana katika sehemu ya mbele ya viungo vya pua meningoencephalitis, hitilafu iliyosababisha uvimbe mkubwa kujitokeza kwenye paji lake la uso, kama inavyoonekana pichani:
5Un articulo de Midi Madagasikara menciona que solo se han visto 37 casos de meningoencefalitis en el Hospital de Ravoahangy.Makala kutoka katika jarida la Midi Madagasikara inadokeza kwamba ni kesi 37 tu ambazo zimeshawahi kutokea katika hospitali ya Ravoahangy.
6Pero lo que no cuenta el artículo es la sorprendente historia de fondo sobre una decidida bloguera de 18 años llamada Diana Chamia quien fue la primera en poner en conocimiento sobre la condicion de Kamba con el post en su blog “ Ayúdenme a Ayúdarlos“.Lakini jambo ambalo makala zote hazikulielezea ni la mazingira ya kusisimua yanayoambatana na habari hii ya kijana mwanablogu pinduani mwenye umri wa miaka 18, Diana Chamia, ambaye ndiye alikuwa wa kwanza kuelimisha umma juu ya hali ya mtoto kamba katika ujumbe wa blogu yake aliouita “Nisaidieni ili niwasaidie wengine“
7Diana Chamia fotografiada con Kamba antes de su operación, la cual fue posible en gran parte por el arduo trabajo de Diana.Diana Chamina pichani, akiwa na mtoto Kamba kabla ya upasuliwaji ambao ulifanikishwa kwa juhudi za Diana.
8Diana, una joven estudiante de periodismo en Mahajanga, Madagascar, aprendió a bloguear gracias a los workshops de medios ciudadanos organizados por los auspiciados de Rising Voices, Foko Madagascar.Diana, kijana mwanafunzi wa uandishi wa habari huko Mahajanga, Madagaska, alijifunza kublogu katika warsha ya uandishi wa kiraia iliyoandaliwa na Foko Madagascar, asasi iliyofadhiliwa na mradi wa Sauti Zinazoinukia (Rising Voices).
9Otros blogueros de Foko de Mahajanga son Cylnice, Jombilo, Lomelle, Mielmanja, Rondro, Tonkataly, Ysiastella, y Zouboon.Wanblogu wengine kutoka mahajanga ni Cylnice, Jombilo, Lomelle, Mielmanja, Rondro, Tonkataly, Ysiastella pamoja na Zouboon.
10Blogueros del Foko Blog Club en Mahajanga, con Diana vestida de negro en el medio.Mabloga kutoka kilabu cha kublogu cha Foko huko Mahajanga, wakiwa na Diana alivalia nyeusi katikati.
11Pero fue Diana quien decidió utilizar su blog como un espacio para la acción social.Lakini ni Diana ndiye aliamua kuitumia blogu yake kama ulingo wa harakati za kijamii.
12Como describe en un post del blog del 19 de abril, Diana conoció por primera vez al bebé Kamba y su mamá soltera, Philomène Georgine, luego de pasarse de su parada de omnibus habitual mientras estaba perdida en sus pensamientos.Kama navyoeleza katika ujumbe wake wa tarehe 19 mwezi wa nne, Diana alikutana na mtoto kamba na mama yake, Philomène Georgine, baada ya kupitiliza kituo chake cha basi cha kawaida baada ya kupitiwa na mawazo.
13Tomé el ómnibus número 5 desde casa al Bazar Mahabibo, pero estaba demasiado soñadora o quizás era el destino de este niñito.Nilipanda basi nambari 5 kutokea nyumbani kuelekea soko la Mahabibo, lakini nilikuwa nimejawa mawazo au pengine ilikuwa ni hatima tu ya kukutana na huyu mtoto.
14Perdí mi parada.Nilipitiliza kituo.
15Ya estábamos en la parada del ómnibus de la ciudad cuando me di cuenta de mi error.Tulikuwa tayari katika kituo cha jengo la jiji ndipo nilipogundua nimekosea.
16En el camino de regreso al mercado, vi a esa señora quien llevaba un niño en su espalda, otro en sus brazos y una gran cartera roja en su hombro.Wakati nikirudi kuelekea sokoni, nikamuona huyu mama aliyekuwa amebeba mtoto mgongoni, na mwingine mikononi na mfuko mkubwa mwekundo begani.
17El que iba al frente estaba envuelto en un sari verde.Huyu aliyekuwa mbele alikuwa amezibwa na na sari ya kijani.
18(Me preguntaba porque ella usaba tal protección con el cálido clima de Majunga).(Nikajiuliza inakuwaje anamsitiri mtoto namna ile katika hali ya hewa ya joto kali la Majunga).
19Una ráfaga sopló, revelando la cara del niño.Upepo ulipopiga ukaonyesha sura ya mtoto.
20Diana continúa describiendo la interacción con Philomène quien, a pesar de sus mejores esfuerzos, no pudo conseguir ayuda para afrontar la operación que extraería la gran protuberacia en la frente de su hijo.Diana anaendelea kuelezea maongezi yake na Philomène, ambaye, pamoja na jitihada zote, hakuwa amefanikiwa kupata msaada kwa ajili ya upasuaji ili kuondoa uvimbe ule mkubwa uliokuwa kwenye paji la uso la mwanawe.
21Ese mismo día Diana se prometió a sí misma que trabajaría para conseguir la operación para Kamba y que le permitiría crecer como un niño normal sin atraer las extrañas miradas de los transeúntes a las cuales su madre ya se había acostumbrado.Siku ile ile Diana alijiwekea nadhiri kwamba atafanya jitihada zitakazomuwezesha Kamba kupasuliwa ili naye apate makuuzi kama watoto wengine bila ya kutupiwatupiwa macho na wapita njia, hali ambayo mama yake alikwishaizowea.
22Los meses siguientes Diana había reunido a sus compañeros blogueros malgaches para ayudar a su causa.Kwa miezi michache iliyofuatia Diana aliwahamasisha wanblogu wenzie ili wamsaidie katika wito wake.
23El proyecto Foko completo fue tras la iniciativa y ayudó a Diana a levantar Zaza sy Vavy Gasy (”Para Mujeres y Niños Malagaches”), un sitio bilingüe dedicado a conseguir ayuda y financiamiento para la costosa operación de remover la protuberancia de la frente de Kamba.Kundi zima la mradi wa kublogu wa Foko wakaitikia wito na kumsaidia Diana kuanzisha Zaza sy Vavy Gasy (“Kwa mama wa Ki-Malagasy na mwanawe”) , tovuti ya lugha mbili yenye lengo la kuongeza misaada na ufadhili kwa ajili ya upasuaji aghali utakaoondoa uvimbe kwenye paji la uso la Kamba.
24También fue creada una Página por la Causa en Facebook.Kadhalika ukurasa wa Facebook pia ulianzishwa.
25La larga campaña de Diana fue bien documentada por la coordinadora del proyecto Foko, Joan Razafimaharo tanto en su blog personal como en el blog colectivo nacional, Malagasy Miray.Kampeni hiyo ndefu ya Diana imeandikwa na kuorodheshwa vyema na mratibu wa mradi wa Foko, Joan Razafimaharo, kwanza katika blogu yake binafsi, na pia katika blogu ya jumuiya ya kitaifa ya wanablogu Malagasy Miray.
26Mientras tanto en Canadá, Jean Razafindambo, un expatriado malgache con fuertes raíces en Mahajanga, estaba navegando en internet el día en que nació su nieto cuando tropezó con el blog de Diana.Wakati huo huo huko nchini Kanada, Jean Razafindambo, mtaalamu muhamiaji wa Ki-Malagasy mwenye mizizi imara huko Mahajanga alikuwa akiperuzi kwenye mtandao wa intaneti siku hiyo ambayo mjukuu wake wa kiume alikuwa amezaliwa, na ndiyo alipokumbana na blogu ya Diana.
27Como Razafindambo dijo al Ottawa Citizen, “Pensé en mi nieto, él era saludable, y si (Kamba) era mi nieto, ¿qué haría?”Kama Razafindambo alivyolieleza jarida la the Ottawa Citizen, “Nilimfikiria mjukuu wangu, alikuwa ni mwenye afya, na kama (Kamba) angalikuwa mjukuu wangu, ningefanya nini?”
28Con la ayuda de amigos, compañeros de trabajo y extraños generosos, Jean y su esposa Baku recaudaron cerca de $1,500 para la operación de Kamba corriendo la media maratón en Ottawa en mayo.Kwa msaada wa wafanyakazi wenzake na watu baki, Jean na mkewe baku walichangisha karibu ya dola 1500 kwa kukimbia nusu-mbio ndefu za mji wa Ottawa ajili ya matibabu ya Kamba mnamo mwezi wa tano.
29Baby Kamba recuperándose bienMtoto Kamba akipona vizuri.
30Como puede verse en la foto anterior, el bebé Kamba está recuperandose notablemente dada la seriedad de la operación (con una duración de más de 8 horas).Kama unavyoona pichani hapo juu, mtoto kmaba anapona vilivyo ikizingatiwa kuwa upasuaji wake ulikuwa nyeti (ulichukua zaidi ya masaa 8).
31Dicha operación nunca podría haberse llevado a cabo si no fuese por el gran corazón de Diana y su obstinada persistencia.Upasuaji ule usingewezekana kutokea ghairi ya moyo mwema na jitihada zisizokoma za Diana.
32¿Cuántas veces pasamos junto a un individuo con necesidades y culpamos a nuestros gobiernos por la falta de un sistema de salud o viviendas de protección decentes?Ni mara ngapi tunawapita watu wanaohitaji msaada na kuilaumu tu serikali kwa kutotoa huduma nzuri za afya na makazi?
33Pero luego seguimos caminando.Ikesha tunatembea mbele.
34Diana no siguió caminando.Lakini Diana hakupita.
35Armada con nada más que un blog y su decisión, cambió para siempre la vida de un bebé quien fue conocido en el mundo como el Bebé Kamba.Bila silaha nyingine zaidi ya blogu na nia yake, ameweza kubadilisha milele maisha ya mtoto ambaye amejulikana duniani kama mtoto kamba.
36Puede escuchar directamente a la mamá de Kamba Philomène y a la misma Diana en el siguiente video con subtitulado en inglés.Unaweza kusikiliza moja kwa moja kutoka kwa mama yake Kamba, Philomene na kutoka kwa Diana mwenyewe katika filamu ifuatayo yenye vielelezo katika kiingereza.