# | srp | swa |
---|
1 | Osnivač zabranjene vojne grupe u Pakistanu nudi pomoć SAD-u | Mwanzilishi wa Kikundi cha Kijeshi Kilichofutwa Nchini Pakistani Ajitolea Kuisaidia Marekani. |
2 | Pošto je izazvala veliku štetu duž obale Atlantika u SAD-u, super oluja Sendi je označena kao najskuplja oluja koja se ikada desila. | Baada ya kusababisha uharibifu mkubwa pembezoni mwa pwani ya atlantiki nchini Marekani, Kimbunga kikubwa sandy kinachukuliwa kama kimbunga kilichosababisha madhara makubwa ambayo hayakuwahi kutokea. |
3 | Uz procene štete koje idu i do US$45 milijardi za rekonstrukciju i građenje, zemlja se priprema da se suoči sa gubitcima. | Kiasi cha fedha kinachokadiriwa kufikia dola za kimarekani milioni 45 zinahitajika ili kurekebisha na kujenga upya makazi na miundombinu, ambapo nchi inajiandaa kukabiliana na hasara hiyo. |
4 | Prijavljeno je da je najmanje 33 osobe poginulo, a desetine njih je raseljeno širom istočne obale. | Watu wasiopungua 33 inaelezwa kuwa wamepoteza maisha na idadi kubwa ya watu wameachwa bila makazi katika maeneo mbalimbali ya pwani ya Mashariki. |
5 | Usred opšte uzbune, Hafiz Mohammad Saeed, osnivač zabranjene vojne organizacije Lashkar e Taiba (LeT) i šef Jaamat ud Dawa (JuD) je ponudio značajnu količinu humanitarne pomoći SAD-u. | Huku kimbunga hiki kikiendelea kuleta madhara, Hafiz Mohammad Saeed, mwanzilishi wa kundi la kijeshi lililofutwa, Lashkar e Taiba (LeT) na kiongozi wa Jaamat ud Dawa (JuD) alitoa msaada wa kibinadamu kwa nchi ya Marekani ili kuisaidia kufuatia uharibifu uliotokea. |
6 | Uragan Sendi je izazvao haos na Rockaways i Breezy Point u Kvinsu. | Kimbunga Sandy kilichosababisha uharibifu mkubwa ulioenea sehemu za mwambao na pwani ya Queens. |
7 | Mnogi su izgubili svoje domove, poslove i imanja. | Wengi wamepoteza makazi yao, biashara na mali zao. |
8 | Slika Kevin Dovns. | Picha na Kevin Downs. |
9 | Autorska prava Demotix. | Haki miliki na Demotix. |
10 | Nudeći pomoć svake vrste, rekao je: “Jamaat-ud-Dava je spreman da pošalje svoje dobrovoljce, lekare, hranu, lekove i drugu humanitarnu pomoć, ako nam vlada SAD to dozvoli.” | Akiahidi kusaidia kwa hali na mali misaada ya kila aina, alisema, “Jamaat-ud-Dawa iko tayari kutuma watu wa kujitolea, madaktari, vyakula, madawa na vitu vingine vya kuwasaidia wahanga endapo serikali ya Marekani itaturuhusu”. |
11 | Poznat kao osoba koja je skovala napad u Mombaju 2008 godine, osnivač JuD-a takođe nosi poklon od US$10 miliona u svojim rukama. | Akijulikana kama muongozaji mkuu wa mashambulizi ya Mumbai ya mwaka 2008, mwanzilishi wa JuD pia alitoa msaada wa dola milioni 10 za kimarekani . |
12 | Međutim, Američka ambasada u pakistanskom gradu Islamabadu je odbila da prihvati pomoć od Saeed-a. | Hata hivyo, ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Islamabad nchini Pakistani umekataa kupokea msaada kutoka kwa Saeed. |
13 | Koristeći svoj Tvitter nalog, ambasada je jasno saopštila da dok cene spremnost muslimana da pomognu, oni očigledno njegovu ponudu ne shvataju ozbiljno. | Wakitumia ukurasa wao wa Twita, ubalozi huo umeweka bayana kuwa pamoja na kuwa wanathamini kitendo cha waislamu kutoa misaada, hawakutilia maanani kabisa msaada wa ndugu Saeed. |
14 | @usembislamabad (Ambasada SAD u Islamabadu): Mi poštujemo islamsku tradiciju da pomognu onima kojima je to potrebno, ali Hafiz Saeed-ovu ponudu ne možemo shvatiti ozbiljno. | @usembislamabad (Ubalozi wa Marekani Islamabad): Tunaheshimu utamaduni wa Waislamu wa kutoa misaada kwa wahitaji, lakini hatuwezi kutilia mkazo msaada wa Hafiz Saeed. |
15 | Nakon tweeta, portparol JuD-a je postavio sledeći odgovore: | Kufuatia maelezo hayo katika Twita, msemaji wa JuD alijibu kama ifuatavyo: |
16 | @JuD_Službeno (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad Naša ponuda je rezultat ozbiljnosti sitaucije. | @JuD_Official (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad Tulitoa msaada wetu wa dhati kutokana na hali halisi ya janga. |
17 | Nadamo se da će Muslimani u SAD održati #tradiciju živom. | Ni matarajio yetu kuwa Waislamu wanaoishi Marekani watauendeleza utamaduni huu. |
18 | Inshallah | Inshallah |
19 | @JuD_Službeno (Jamat ‘ud' Da'wah) @usembislamabad Naša ponuda pomoći je za američki narod, mi ćemo angažovati muslimane u SAD-u da bude na čelu onih koji pomažu svojim zemljacima. | @JuD_Official (Jamat ‘ud' Da'wah) @usembislamabad Msaada wetu ni kwa ajili ya watu wa Marekani, tutawahusisha Waislamu wa Marekani kuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia ndugu zao. |
20 | @JuD_Službeno (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad #USAID Rajiv Shah nas je ozbiljno shvatio kada je posetio naš kamp za pomoć 2010 godine & kada je tamo razdelio pomoć - #Hafiz Saeed | @JuD_Official (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad Rajiv Shah kutoka shirika la Kimarekani la kutoa misaada alitoa kipao mbele kwetu pale alipotembelea kambi yetu ya kutoa misaada mwaka 2010 na kutoa misaada - #Hafiz Saeed |
21 | Američka ambasada je otišla tako daleko da je Saed-a proglasila osumnjičenim za umešanost u napade u Mombaju i pripisivajući njegovoj organizaciji JuD epitet organizacije koja je ‘teroristički opredeljena'. | Ubalozi wa Marekani ulienda mbali pale walipomuhusisha Saeed na tuhuma za kujihusisha na mashambulizi ya Mumbai na pia kuliita shirika lake JuD kuwa ni shirika lililo na mrengo wa kigaidi. |
22 | @usembislamabad (Ambasada SAD u Islamabadu ): Saaed-a traže zbog sumnje da je umešan u napad u Mombaju, u kome je poginulo 166 ljudi. | @usembislamabad (US Embassy Islamabad ): Saaed anatafutwa kuhusishwa na mashambulizi ya Mumbai yaliyopelekea watu 166 kuuawa. |
23 | JuD je od strane UN-a i SAD-a označena kao teroristička organizacija. | JuD ni shirika linalotambuliwa na Umoja wa Mataifa na Marekani kuwa ni la Kigaidi. |
24 | Twitter nalog za JuD je još jednom bio spreman za odgovor. | Ukurasa wa Twita wa JuD ulikuwa tayari kutoa majibu. |
25 | @JuD_Službeno (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad Američka vlada je priznala da su činjenice neprihvatljiv dokaz protiv Hafiz Saeed-a. | @JuD_Official (Jamat ‘ud' Da'wah): @usembislamabad Serikali ya Marekani imekubali ukweli ambao haukudhibitishwa kuwa ni sahihi ndidi ya Hafiz Saeed. |
26 | UNSCR saslušanje treba da se obavi. | Kauli ya UNSCR bado inasubiriwa. |
27 | Ništa ne ostavlja iza sebe. | Hakuna kinachoachwa. |
28 | Reakcije na ovu ponudu ostaju pomešane. | Maoni kuhusiana na msaada huu bado yanakanganya. |
29 | Dok je mnogi posmatraju kao velikodušnu, neki takođe vide ironiju iza svega toga. | |
30 | @Rifaqat_Mir (Rifaqat A. | @Rifaqat_Mir (Rifaqat A. |
31 | Mir): Uprkos neprijateljstva koje SAD predstavlja za Hafiza Saed on je i dalje velikodušan i dobronameran u pokazivanju saosećanja za svog neprijatelja | Mir): pamoja na uadui unaowekwa na Marekani kwa Hafiz Saeed, bado ana nia ya dhati ya kutoa misaada katika kuendelea kuonesha kumjali adui yake. |
32 | @humayusuf (Huma Yusuf): Kažu da Muslimani nemaju smisao za humor, ali Hafiz Saed-ova ponuda za pomoć žrtvama #Sendi je SMEŠNA http://www.thenews.com.pk/Današnje-Novosti-13-18499-Hafiz-Saeed-nudi-humanitarnu-pomoć-za-SAD … | @humayusuf (Huma Yusuf): wanasema kuwa Waislam hawana roho ya huruma, lakini utayari wa Hafiz Saeed wa kuwasaidia wahanga wa kimbunga cha Sandy inaonekana ni kichekesho. http://www.thenews.com.pk/Todays-News-13-18499-Hafiz-Saeed-offers-humanitarian-aid-to-US … |
33 | @anDYRude (Anirudh Malladi): Upravo sam pročitao da je Hafiz Saed, strašni terorista, ponudio “pomoć u vidu hrane, lekara itd” žrtvama #Oluje Sendi. | @anDYRude (Anirudh Malladi): Punde tu nimesoma kuwa, Hafiz Saeed, gaidi aliyeogopeka, amejitolea”kutoa msaada wa vyakula, madaktari, n.k ” kwa wahanga wa kimbunga cha sandy. |
34 | LMAO! | LMAO! |
35 | @nidak_ (Nida Khan): Interesantna razmena šala dešava se između Hafiz Saeed-a i SAD ambasade u Islamabadu. 1-1, rekao bih. | @nidak_ (Nida Khan): Kuvumilia jumbe za kashfa zinazoendelea kati ya Hafiz Saeed na ubalozi wa Marekani mjini Islamabad ni 1-1, ningeweza kusema. |
36 | #Sledeća Runda? | #Mzunguko unaofuata? |
37 | @anamzehra86 (Anam Zehra): Odgovor ambasade SAD-a na ponudu Hafiz Saeed-a je njihov način da se kaže “mi mislimo da je Vaša religija ozbiljna, a i Vi bi to trebali da uradite” | @anamzehra86 (Anam Zehra): Majibu ya Ubalozi wa Marekani kufuatia kujitolea kwa Hafiz Saeed ni namna yao ya kutaka kusema kuwa, ”tunachukulia dini yako kwa uzito mkubwa sana, nawe ungalipaswa pia kufanya hivyo” |