# | swa | zhs |
---|
1 | Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu | 乌干达:爆炸案发生后… |
2 | Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. | 世界各地足球迷前晚聚集在酒吧和餐厅里,观看世界杯足球赛决赛实况,乌干达却因首都两处热门场所发生爆炸,让欢乐气氛嘎然而止。 |
3 | Nchini Uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo. | |
4 | Mpaka sasa vyombo vya habari nchini Uganda vimeripoti vifo zaidi ya 70, huku dazeni kwa dazeni wakiwa wamejeruhiwa vibaya kutokana na milipuko hiyo. Polisi wa Uganda wameeleza kwamba huenda milipuko hiyo imefanywa na kikosi cha wapiganaji wa Ki-Somali cha Al-Shabab. | 乌国媒体目前报导逾40人身亡,另有数十人因此受伤,警方指称索马利亚武装团体al-Shabab是幕后凶手,该组织一名领袖最近呼吁攻击乌干达,因为乌国派兵参与非洲联盟在索国的维和任务,该组织事后赞扬攻击行为,但并未承认犯案。 |
5 | Mmoja wa makamanda wa juu wa kikosi hicho hivi karibuni alitaka Uganda ishambuliwe kwa kuwa imepeleka wanajeshi wake katika kikosi cha kulinda amani nchini Somalia. | 死亡爆炸案受害者在Mulago医院等待治疗,照片来自Trevor Snapp,经摄影师许可使用 |
6 | Kundi hilo limepongeza kutokea kwa milipuko hiyo lakini hakikusema kama kinahusika nayo ama hapana. | 乌干达博客Gay Uganda指出: |
7 | Waathirika wa milipuko miwili ya kutisha ya mabomu jijini Kampala wakisubiri kupatiwa huduma katika Hospitali ya Mulago. Picha ilipigwa na Trevor Snapp. | 乌干达遭到攻击,但其实是全人类受到攻击,谁会这么恶毒,对这种灾难感到快乐? |
8 | Picha hii imetumiwa kwa ruhusa ya aliyeipiga Mwanablogu wa Uganda Gay Uganda anaandika: | 索马利亚游击队显然很开心,因为他们在索国与非洲联盟部队交战,认为非洲联盟阻挡他们建立伊斯兰律法统治的国家。 |
9 | Uganda imeshambuliwa. Kwa kusema kweli ni ubinadamu ndiyo ulioshambuliwa. | …但我看见同胞只不过在看足球赛,却遭到杀害及伤害,而他们对暴力背后的目标毫无所知,对非洲联盟部队也毫无影响力。 |
10 | Je, nani anaweza kuthubutu kuwa na furaha kufuatia ukatili mkubwa kama huu? | Ernest Bazanye则提醒,不要太早对爆炸案凶手身分下定论: |
11 | Mpaka sasa ni wapiganaji wa Ki-Somali ndiyo wanaofurahia. Wanafurahi kwa sababu wanapambana na vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Somali, vikosi hivyo vimewazuria wapiganaji hao kuanzisha dola la Kiislamu lenye kuongozwa na Sharia ya Kiislamu. …. | 虽然外国传言这是两起自杀爆炸案,由索马利亚恐怖组织Al-Shahab主使,现在要确定凶手身分与动机还言之过早,我们都应该明白,真相不会那么快厘清,此刻任何结论都还不够明确。 |
12 | Ninachokiona ni raia wenzangu, binadamu ambao kikubwa walichokuwa wanakifanya ni kutazama mechi ya kandanda ambapo wengi wao wameuawa na wengine kujeruhiwa, wamefanyiwa hivyo kwa fikra na njozi ambazo pengine wala hawakuwahi kuziwazia, yaani vitendo ambavyo wala hawawezi kuvitawala au kuwa na ushawishi navyo. | |
13 | Ernest Bazanye anatahadharisha kwamba pengine watu wasifanye haraka kuhukumu kwamba nani hasa alitega na kulipua mabomu hayo, bado ni mapema mno: | |
14 | Ni mapema mno kusema nani anahusika na kwa nini, hata kama kuna minong'ono huko nje ya nchi kwamba kitendo hicho cha kuua watu kwa mabomu kilifanywa na kundi la Al-Shahab, ambalo ni kundi la magaidi huko Somalia. | |
15 | Bila shaka mpaka sasa tumeshakomaa vya kutosha kuelewa kwamba kwa kawaida ukweli hauji haraka hivyo, kwamba bado ni mapema mno. | 记录片摄影师Trevor Snapp居住在乌国首都,他在爆炸案后,前往收容许多伤患的Mulago医院,他写道: |
16 | Trevor Snapp, ambaye ni mpiga picha mtengeneza makala za maoni na anayeishi Kampala, alikwenda Hospitali ya Mulago, mahali ambapo waathirika wengi wa mabomu hayo walipelekwa mara baada ya milipuko. anaandika: | |
17 | Wanafamilia walimiminika kuelekea sehemu ya mapokezi wakati ambapo madaktari na miili iliyojaa damu walikimbizwa na kutolewa katika chumba cha upasuaji. Katika ukumbi wa kuelekea chumba cha upasuaji kulikuwa na mwili umelala sakafuni, damu zilikuwa zikimiminika kutoka kichwani, ilikuwa vigumu kusema kama alikuwa bado yungali hai au alikwishakufa. | 许多家属在柜台前来回踱步,医师与满身是血的伤患不断进出手术室,有名男子倒在走廊地板上,头部鲜血直流,不知他是否仍有生命迹象;不远处的小储藏室里,医院员工设置临时停尸间,六具遗体躺在地上,有些衣服破损不堪,死者都很年轻。 |
18 | Hatua chache kutoka hapo, katika chumba kidogo cha kuhifadhia vifaa vya madaktari, wahudumiaji walipageuza kuwa mahali pa kuhifadhia miili ya watu, kulikwa na miili 6 iliyokuwa imelazwa sakafuni, baadhi ya maiti nguo zikiwa zimechanwachanwa na nguvu ya milipuko. | |
19 | Miili yote ilikuwa ya vijana. Wanablogu wengi wameshtushwa kwamba milipuko hiyo imetokea Kampala, jiji ambalo linafahamika kwamba ni moja ya majiji makuu yaliyo salama zaidi barani Afrika. | 许多博客对爆炸案惊讶不已,因为索国首都向来是非洲最安全首都著称,前全球之声作者Joshua Goldstein曾居住于当地,他描述爆炸发生地点的样貌: |
20 | Joshua Goldstein, a mwandishi wa zamani wa Global Voices ambaye aliwahi kuishi Kampala, anaelezea maeneo mawili ambapo milipuko ilifanyika: | |
21 | Klabu ya Mchezo wa Rugbi ya Kampala ni Baa iliyo na eneo kubwa la wazi, iko pembezoni mwa kiwanja, mahali hapa wanapenda sana kuja wanafunzi wa vyuo ambao huja hapo kurandaranda na marafiki zao. | |
22 | Kama Uganda ingekuwa na makundi fulani ya kiitikadi basi hapa ndiyo mahali ambapo wangefika kufanya sherehe zao. Hapo ni mahali ambapo watumiaji hujipatia vinywaji vyao maalumu vya Nile huku wakisindikizwa na muziki wa mbali wa rege pamoja na hip hop. | Rugby Club这间酒吧形状可随球赛调整,当地许多大学生都会在此与同伴相聚,若乌干达也有兄弟会的概念,这里就是兄弟会举办派对的场所,Nile Special是特色饮料,雷鬼与嘻哈音乐不绝于耳,周末白天会在此播放橄榄球赛,还会搭起棚子遮阳。 |
23 | Katika siku za mwisho wa juma ni makundi ya watu wa aina hiyohiyo ambao huja kutazama ragbi,huku kola zao zikiwa zimenyanyuliwa juu ili kujikinga na jua. …. | |
24 | Upande mwingine wa jiji kuna Kijiji Cha Ki-Ethiopia, upande wa chini wa mtaa kuna Ubalozi wa Marekani, hapa ni katikati kabia ya Kabalagala, ambayo inaweza kuitwa ndiyo Las Vegas ya Kampala. | |
25 | Mgahawa, upo upande wa juu wa kiasi cha nusu dazeni au zaidi kidogo ya mighahawa ya Ki-Ethiopia ndani ya kiasi cha mita 500, ipo katikati ya makutano ya Barabara ya Ggaba na ile ya Tank Hill. | |
26 | Nyakati za Mchana waandishi wa habari wa Ki-Ethiopia waliokimbia kwao hupoteza wakati wao kwa kutafuna miraa na kubadilishana habari za matukio ya siku hiyo. Nyakati za usiku, eneo lote huchangamka kwa mwanga wa taa zinazotoka kwenye baa na mitoko ya usiku. | …Ethiopian Village位于首都的另一边,与美国大使馆同一条街,当地犹如索国首都的拉斯维加斯,短短500公尺距离约有六家衣索比亚餐厅,这家最为高级,座落在 Ggaba路与Tank Hill路交叉口,流亡在外的衣索比亚异议记者会在下午聚集于此,一边嚼着巧茶(miraa),一边讨论新闻,晚上这附近满是酒吧与舞会。 |
27 | Sleek anaandika: | Sleek提及: |
28 | Kutoa picha kamili kwa tukio hili zima, nitasema kwamba mpaka sasa, Kampala imekuwa moja ya sehemu zile ambazo mtu anaweza kutembea mpaka hata saa 9 usiku kutoka upande mmoja wa mji hadi mwingine. | |
29 | Na kwamba sisi ni aina ile ya watu ambao hulalamikia kuongezeka kwa bei za mafuta, kodi zilizo juu za Lipa Kadiri Unavyopata, gharama za juu ya upigaji simu … kwa ujumla ni gharama zilizo juu ya maisha. Lakini pamoja na hayo bado mtu anamudu kwenda sehemu ya burudani na kulipa walau Shilingi za Uganda 5,000 ili kujipatia bia. | 先跟各位说明一下,长期以来,索国首都一直很安全,纵然在凌晨三点,人们可以从市区一端步行至另一端,我们总是在抱怨燃料价格高 涨、税赋太多、飞机票太贵…生活成本整体而言非常高,但我们还是会前往新开的店,花5000乌干达币买瓶啤酒,酒吧里总是人满为患、寸步难行,一切都 显得平常。 |
30 | Na huwa tunajazana kwenye sehemu hizo mpaka mtu unapata shida kupita ili kujinunulia kinywaji. | |
31 | Na hapo tunazungumzia nyakati zile ambazo watu hujazana wa kiwango cha wastani. | |
32 | Na kisha mara unasikia milipuko ya mabomu … | 直到你听见爆炸声… |