# | swa | zhs |
---|
1 | Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera | 南非:对抗爱滋新时代? |
2 | Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii huenda ikaashiria mabadiliko ya sera za serikali kuhusu suala la VVU na UKIMWI. | 九月底时,南非临时总统Kgalema Motlanthe任命霍根(Barbara Hogan)出任卫生部长,取代备受争议的前部长Manto Tshabalala-Msimang,爱滋病运动人士和许多南非民众都希望,这件人事案将改变政府的爱滋病政策。 |
3 | Hogan, mwanamama mwanaharakati mkongwe dhidi ya ubaguzi wa rangi na mwanachama wa muda mrefu wa ANC, yaani African National Congress, hapo awali alikuwa mwenyekiti wa kamati ya kusimamia masuala ya fedha. Tangu kuteuliwa kwake kuwa waziri wa afya, amebadili mwelekeo wa serikali iliyopita kuhusu VVU na UKIMWI na kuapa kutoa kipaumbele kwa masuala ya UKIMWI. | 霍根为长期反种族隔离人士、执政党「非洲民族议会」资深党员,亦为金融商品组合委员会前主席,自就任卫生部长以来,她已破除前任政府对 爱滋病的立场,宣示将把 爱滋病列为优先政策。 |
4 | Jambo hili limezua mshawasha miongoni mwa raia wa Afrika ya Kusini, ambapo wengi wao wanaamini kwamba Hogan anaweza kuimarisha vita vya nchi dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kufuata sera yenye kuzingatia mtizamo wa kisayansi zaidi. | |
5 | Katika picha hii ya video, wanaharakati wa masuala ya UKIMWI wanashangilia uteuzi wa Hogan katika nafasi yake hiyo mpya. | 许多南非民众对此相当兴奋,有信心霍根能依据科学订定爱滋病防治政策,爱滋病运动人士在这段录像中庆祝霍根获任命。 |
6 | Siku za nyuma Hogan alipata kumkosoa waziwazi Rais wa zamani Thabo Mbeki na msimamo wake juu ya sera ya VVU na UKIMWI. | 过去霍根曾公开批判前总统姆贝基(Thabo Mbeki)对爱滋病的立场与政策,南非约有570万名爱滋病患,去年也有35万人因此死亡(平均每日约千人)。 |
7 | Wastani wa watu milioni 5.7 nchini Afrika ya Kusini wanasemekana kuishi na VVU na kiasi cha watu 350,000 walifariki kutokana na UKIMWI mwaka jana nchini humo (wastani wa watu 1,000 kila siku). Kwa upande mwingine Tshabalala-Msimang amelaumiwa vikali kwa kutofanya juhudi za kutosha kukabili tatizo la VVU na UKIMWI nchini humo. | 外界批评前部长处理 爱滋病问题不当,他鼓吹吃甜菜根、大蒜等食品能治疗爱滋病,因此得到「甜菜根博士」的绰号,舆论更指控他造成社会对 爱滋病药物的困惑。 |
8 | Waziri huyo wa zamani wa afya alihamasisha matumizi ya vyakula kama vile beetroot, vitunguu saumu na vinginevyo kama tiba ya VVU na UKIMWI, jambo lililosababisha watu kumbatiza jina la “Dkt Beetroot”, na zaidi ameshutumiwa kwa kusababisha mkanganyo kuhusu matumizi ya dawa za kurefusha maisha (ARV). | |
9 | Stephen, akiandika kwenye tovuti ya irreverence, alimuita Tshabalala-Msimang kama aibu ya taifa na papo hapo akimwita Hogan kama tumaini lililorejea. Ciaran Parker, akitumia blogu yake ya Ciaran's Peculier [sic] Blog, anafafanua kuhusu msimamo wa Tshabalala-Msimang usiokubaliwa na wengi: | irreverence网站的Stephen称呼前部长为全国之耻,认为霍根是希望曙光;Ciaran's Peculier博客的Ciaran Parker进一步说明前部长非正统的观念: |
10 | “Ingawa Kgalema Motlanthe ameahidi kutoleta mabadiliko makubwa, bado ameatosa baadhi wa mawaziri wenye utata mkubwa waliokuwa kwenye serikali ya Mbeki. Mmoja wao akiwa ni Waziri wa Afya, Dkt Manto Tshabalala-Msimang, aliyekuwa mwananadharia mkubwa katika hoja ya Mbeki ya sera za kukana uwepo wa UKIMWI. | 临时总统虽表示将萧规曹随,但至少摆脱前政府受人争议的几位部长,包括主导过去爱滋病政策的前卫生部长Manto Tshabalala-Msimang,姆贝基政府否认人体免疫缺损病毒(HIV)导致爱滋病,前卫生部长亦认为逆滤过性病毒药品虽对治疗 爱滋病有部分效果,但价格过于昂贵。 |
11 | Serikali ya Mbeki ilikataa katakata kuona uhusiano uliopo kati ya VVU na UKIMWI, na waziri wake wa afya alijenga hoja kwamba hata dawa za kurefusha maisha, ambazo kwa kweli zimeonyesha kusaidia katika juhudi za kukabili gonjwa hili, zilikuwa ghali mno … Wataalamu wa afya wanaofanya kazi nchini Afrika ya Kusini na ambao walipingana waziwazi na nadharia za kushangaza za waziri huyu walijikuta wakifanywa kuwa wahanga.” | |
12 | Mapema juma lililopita, wakati wa uzinduzi wa mkutano juu ya Chanjo ya UKIMWI ya Kimataifa ya 2008 (International AIDS Vaccine 2008) huko Cape Town, Hogan, alitangaza hadharani kwamba VVU husababisha UKIMWI na kwamba ni lazima kukabiliana nao kwa kutumia dawa za hospitalini. | |
13 | Pia alieleza kwamba serikali ilikuwa na nia ya dhati kuongeza nguvu katika programu za kuzuia uambukizaji wa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, dawa zinazozuia akina mama wajawazito wenye VVU kuwapatia watoto wao ambao hawajazaliwa maambukizo na kueleza kwamba chango madhubuti ya VVU ilikuwa ikihitajika mno. | |
14 | Wanasayansi, wanaharakati na wanablogu wengi wameeleza furaha yao kufuatia hotuba iliyotolewa na Hogan. | …南非卫生单位专家若公开反对部长的怪异言论,就会遭到惩处。 |
15 | Haley, akiblogu katika tovuti inayoitwa ujasura kama mwanafunzi balozi, ana hili la kusema: “Kusema kweli, watu wengi ninaozungumza nao wanashangazwa na jambo hili - kwamba maafisa wa serikali waliochaguliwa kwa njia za kidemokrasi wanakana fikra … kwamba … VVU husababisha UKIMWI. | 2008年国际爱滋病疫苗研讨会于十月中在南非开普敦举行,霍根在开幕致词公开表示,就是HIV病毒造成 爱滋病,也应使用正规药物治疗,她亦强调政府将扩大母子传染预防计划,避免患病母亲将爱滋传染给孩子,而世界也亟需有效的疫苗。 |
16 | Hata hivyo, kwa bahati mbaya, hapa Afrika ya Kusini hivyo ndivyo hali ilivyokuwa … lakini sasa mambo yamebadilika, msimamo si huo tena.” Ray Hartley, anayeandika katika The Times, Afrika ya Kusini, anablogu akiongeza: | 听完霍根致词后,许多科学家、社运人士与博客都松了一口气,adventures as an ambassadorial scholar博客的Haley指出: |
17 | “‘Tunajua kwamba VVU husababisha UKIMWI.' Kwa kauli hii, Waziri wa Afya, Barbara Hogan, amehitimisha muongo mzima wa aibu ya kukana uwepo wa UKIMWI jambo ambalo limeigharimu Afrika ya Kusini idadi isiyohesabika ya maisha ya binadamu, wakati huohuo wale waliokuwa wakiishi na VVU wakiishia kuishi kana kwamba kwenye kivuli chao wenyewe.” | 我和多数人谈起此事时,他们都很意外今日竟还有民选官员,会否认HIV病毒造成爱滋病,可惜先前南非情况就是这样,不过现在不同了。 |
18 | Ni vigumu kueleza idadi kamili ya watu walioathiriwa na sera zilizopita juu ya VVU na UKIMWI, lakini Shirika la Treatment Action Campaign (TAC) (Kampeni ya Kutetea Tiba) linakadiria kwamba kiasi cha raia milioni mbili wa Afrika ya Kusini walikufa kutokana na kuugua UKIMWI katika kipindi ambapo Mbeki alikuwa madarakani, na kwamba walau jumla ya vifo 300,000 vingeweza kuepukwa endapo tu angetimiza baadhi ya mambo ya msingi ya kikatiba. | |
19 | Baadhi ya wanablogu wanasema kwamba wote wawili, Mbeki na Tshabalala-Msimang wametapakaa damu mikononi mwao. Soneka Kamuhuza, anayeandika kupitia blogu ya Things That Make You Go Mmmh! anamshutumu vikali Mbeki. | Ray Hartley在The Times, South Africa博客另表示: |
20 | “Umawazo mgando wao [Mbeki na Tshabalala-Msimang], umbumbumbu wa kukusudia na kujitia kwao kuwa wanyofu kulichochea tu uendelevu wa janga hili. | 「我们知道HIV病毒导致爱滋病」,由这句话开始,卫生部长霍根终结南非令人羞耻的十年爱滋否认期,这段时间牺牲南非无数生命,也迫使患者生活在阴影中。 |
21 | Kutumia njia ya kutazama tatizo zima kwa upana badala ya chanzo chake, pasipo kuingiza na njia nyingine, hakuwezi kuwa njia madhubuti ya kutibu VVU, waliingiza nchi katika wakati mgumu kwa kutumia umbumbumbu wao ambao waliulinda kwa njia zote. Hivi sasa inakadiriwa kwamba Afrika ya Kusini inaongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU. | 我们难以计算多少人受过去的爱滋病政策影响,不过「治疗行动运动」(TAC)指出在姆贝基执政期间,超过200万南非民众因 爱滋病而死,若前总统能遵守宪法基本原则,至少能避免30万人死亡。 |
22 | Kwa namna fulani, naona ushawishi wa Mbeki katika jambo hili … Katika nchi ambayo ina utajiri mkubwa wa maliasili, amehadaa rasilimali watu iliyo muhimu sana, kwa kuwanyima fursa ya watu kuamua na kuanza kupambana na tatizo hili la UKIMWI kikamilifu.” | 有些博客指控前总统与前卫生部长手上染血,Things That Make You Go Mmmh! |
23 | Wengi wanaamini kwamba Hogan atarekebisha mambo yaliyoharibika kwa sehemu fulani. | 博客的Soneka Kamuhuza怪罪姆贝基: |
24 | Makala katika Peripheries inaonyesha kwamba watu wanatarajia kwamba wakati wa kuwa na ukanaji wa UKIMWI huku ukipewa nguvu na msukumo wa kisiasa nchini Afrika ya Kusini tayari umefikia kikomo. | 前总统与前卫生部长对此事淡漠、短视与虚伪,致使爱滋病持续蔓延,过去的策略无法有效治疗疾病,他们因忽视的态度重创全国。 |
25 | Hata hivyo, wapo ambao hawako kupaparikia mambo haraka hivyo. BillyC, akitoa maoni yake juu ya makala iliyoandikwa katika The Times, la Afrika ya Kusini anasema: | 目前估计,南非 爱滋病患者人数高居全球之冠,我觉得处处都有姆贝基介入的影子,…在此天然资源丰富的国家,人民受到他的欺骗,失去对抗爱滋病的起始机会。 |
26 | “Barbara Hogan ana kazi kubwa mbele yake ili kurekebisha mambo ambayo kwa kiasi fulani tayari amekwishasababisha madhara kwa mfumo wa afya katika uangalizi wa Manto. Uwezo wa wafanyakazi, ari ya kazi, na viwango vya utendaji ukiachia mbali sera za afya na sheria, yote ni mambo ambayo hayana budi kushughulikiwa. | 许多人希望霍根能弥补部分伤害,peripheries博客指出,许多人期待获政治支持的爱滋否认态度能在南非终结,但其它人仍持保留态度,BillyC响应The Times, South Africa的文章时认为: |
27 | Zaidi ya hilo, kuna uhamasishaji wa matumizi ya dawa na upungaji pepo wa kivuduu, vilevile uhusianishaji wa kishetani na sayansi ya magharibi vyote vikiwa vimejikita sawasawa katika mfumo wa kufikiri wa taifa. Itachukua miaka mingi ya kazi ngumu, yenye kujaa ujasiri na unyoofu ili kuturejesha katika mfumo wa afya ulio wa heshima na wenye ufanisi. | 霍根眼前还有重重险阻待克服,才能扭转前政府造成的种种伤害,执行者的能力、士气、卫生政策等都需要处理,使用草药食疗与丑化西方医学等印象已深植于国民心中,必须经过多年的努力与奋斗,才能让我们重返有效且令人尊重的卫生体系,我们只能祈祷霍根如有神助、快马加鞭,她必须加快脚步。 |
28 | Tumwombee Barbara Hogan apate kasi. Kusema kweli anaihitaji.” | 南非爱滋病象征照片来自Flickr用户 mvcorks |
29 | Picha ya Utepe wa Ukimwi wa Afrika ya Kusini imetoka kwa mvcorks katika mtandao wa picha wa Flickr. | 校对:Sophie Chiang |