# | swa | zhs |
---|
1 | Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE | 斯里兰卡:博客关注游击队领袖身亡消息 |
2 | Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. | |
3 | Vyombo vya habari vinaripoti kwamba Prabhakaran, ambaye alikuwa kwenye uongozi wa moja ya maasi ya kikatili zaidi duniani, aliuwawa kwa kombora wakati alipokuwa kwenye basi dogo na mkuu wa jeshi la majini la LTTE, Soosai, pamoja na mkuu wa upelelezi, Pottu Amman. | |
4 | Mwili wa kiongozi huyo wa waasi utafanyiwa uchunguzi zaidi wa DNA ili kuthibitisha utambuzi wake. Kadri ya wanachama 250 wa waasi wa Chui wa Kitamil waliuwawa kwenye mapambano ya mwisho ya vita vilivyodumu kwa miaka 26. | 斯里兰卡政府透过国营媒体及手机简讯,于当地时间5月18日下午宣布,国内游击队「坦米尔之虎」领袖普拉巴卡兰(Vellupillai Prabhakaran)已身亡,新闻媒体报导,普拉巴卡兰与游击队海军首长Soosai及情报首长Pottu Amman共乘汽车时,遭到火箭攻击死亡。 |
5 | Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika alichukuliwa kama muuaji katili kwa wengine. | 斯里兰卡历经26年战火,在最近一波攻击中,据称约有250名游击队成员遭格毙。 |
6 | Chombo cha habari cha BBC kimeandika, “kwa wafuasi wake, Vellupillai Prabhakaran alikuwa ni mpigania uhuru kwa ajili ya ukombozi wa Watamil. | |
7 | Kwa maadui zake alikuwa ni mtu msiri anayependa kutawala na asiyejali kabisa maisha ya wanaadamu wengine.” Gazeti la The Hindu nchini India linasema, Mpigania uhuru kwa wafuasi wake na gaidi wa kuogopwa kwa wengine, Prabhakaran alikuwa anatafutwa na Chombo cha Polisi cha Kimataifa, Interpol, pamoja na mashirika mengine mengi tangu mwaka 1990 kwa makosa ya ugaidi, mauaji na jinai. | 在关于普拉巴卡兰的讣闻里,有些人称之为英雄,有些人称之为无情杀手,英国广播公司指出,「对支持者而言,普拉巴卡兰是为争取坦米尔解放的自由斗士;对敌人而言,他是个神秘的自大狂,毫不尊重人命」;印度《The Hindu》 写道:「支持者眼中的『自由斗士』,也是他人眼中的恐怖份子,普拉巴卡兰自1990年便因恐怖主义、谋杀与组织犯罪,遭国际刑警组嬂等机构追缉」。 |
8 | “kabla dunia haijamsikia Osama Bin Laden au Al-Qaeda, Prabhakaran alianza kutumia mbinu mpya ya vita, mabomu ya kujilipua kwa kujitoa muhanga. Makala hii kwenye gazeti la Tehelka inatoa mwanga kuhusu kiongozi huyu wa vita. | 早在世 界还不认识盖达组织和宾拉登(Al-Qaeda)之前,普拉巴卡兰便已使用自杀炸弹这种新游击战术,《Tehelka》杂志的封面故事记录这位军阀的许多故事。 |
9 | Mwanablogu wa Beyond the Skin anafafanua hivi: Hisia za mwanzo: WHAAA! | Beyond Skin博客解释: |
10 | [vipele vya baridi, kushuka tama na hisia mchanganyiko za hjofu na ahueni.] Hisia zilizofuata: Sasa nini? | 起初反应是一阵惊讶(起了鸡皮疙瘩,下巴也快掉下来,也同时出现恐惧和轻松两种情绪)。 |
11 | Baada ya miaka 26 ya mapambano, baada ya kuua mamia ya maelfu, baada ya kuwanyamazisha wale walioipinga serikali na waasi wa LTTE kwa kuwaua, mateso na watu kupotea, sasa itakuwaje kwa watu wa Tamil? | |
12 | Kada wa chama cha United National Party Ajith P. | 第二项反应:接下来怎么办? |
13 | Perera ameandika salamu za rambirambi kwa Prabhakaran katika blogu yake, akitaka kuwa tofauti na wengine: “alikuwa muuaji, bila ya shaka, lakini Prabhakaran anastahili salamu za rambirambi, hata kama ni katika lugha ambayo alikuwa haielewi,” | |
14 | Je alifanikisha lolote la maana kwa ajili ya jamii yake? | |
15 | Jibu ni HAPANA. Watamil wazawa (Jaffna) wako pabaya zaidi ya pale walipokuwa katika miaka ya 1970. | 经过26年奋斗,无数人遭到杀害或被迫离家,透过暗杀、虐待和强行带走失踪后,压制反对政府与游击队的异议后,坦米尔人的下一步是什么? |
16 | Zaidi ya nusu ya Watamil wamehama moja kwa moja. | 「联合国家党」领袖Ajith P. |
17 | Watamil Wazawa, kundi kubwa la walio wachache nchini Sri Lanka wakati ule, hivi sasa wapungua na kuchukua nafasi ya tatu baada ya Waislamu na Watamil wanaotokea India. | |
18 | Jaffna, jiji la pili kimaendeleo nchini Sri Lanka, na mfumo wake maarufu wa elimu, hivi sasa iko nyuma sana. Kama jamii, Watamil, wale walio na bahati mbaya ya kubaki, wamerudi nyuma miaka kumi au ishirini. | Perera在博客Dare to be different留下对普拉巴卡兰的描述:「普拉巴卡兰无疑是个恐怖份子,但他理应获得一份坦米尔文的讣文,纵然他几乎听不懂这种语言」。 |
19 | Walitambuliwa kama magaidi duniani kote. | 他为这个社群有达到任何重大目标吗? |
20 | Kaskazini na mashariki pamekuwa tegemezi kwa Colombo kiuchumi. Kwa miaka michache ijayo, mpaka hapo serikali ya UNP itakapotekeleza sera zake kisiasa, watakuwa wanaendeshwa kutokea Colombo. | 完全没有,坦米尔人今日情况比七零年代还糟,逾半数坦米尔人已永远离开,无数坦米尔家 庭因失 去亲人,必须承担永恒的痛苦,坦米尔人原是斯里兰卡最大少数族群,如今却落于穆斯林及印度裔坦米尔人之后;Jaffna原在斯里兰卡进步程度居全国第二, 如今已遥遥落后。 |
21 | Yote haya ni shukrani kwa Prabhakaran. Mwanaharakati wa Kitamil na mwanachama wa zamani wa waasi wa LTTE Nirmala Rajasingam anafafanua katika makala kwenye gazeti la Independent kwamba dada yake aliuwawa na waasi wa LTTE miaka 20 iliyopita. | 坦米尔人这个族群的生活倒退了一二十年,全世界称他们是恐怖份子,国内东部及北部地区在经济上日益仰赖首都可伦坡,至少在未来几年,除非 「联合国家党」政府落实解决方案,他们将永远受首都摇控,一切都是拜普拉巴卡兰之赐。 |
22 | Kwa sababu hiyo, habari za maangamizi ya uongozi wa juu wa LTTE - ambao uliamuru kuuwawa kwake pamoja na Watamil wengine wengi waliowapinga - kumeleta ahueni kubwa sana. | 斯里兰卡坦米尔运动人士兼前游击队成员Nirmala Rajasingam在《独立报》投书中,表示自己的姐姐在20年前便遭游击队杀害: |
23 | Vita na ukatili hatimaye vimesitishwa na kumwagika kwa damu za Watamil kumefikia mwisho. | 当初就是游击队首领下令杀害她和其他异议份子,故听闻普拉巴卡兰的死讯,我着实松了一口气,战争与屠杀终于划下休止符,坦米尔异议人士的血液也不用再流。 |
24 | Hata hivyo anaonya: | 但她提醒: |
25 | Pingamizi linaloendela la kutoruhusu mashirika ya misaada ya kibinaadamu kuingia halisaidii kupunguza mashaka juu ya nia ya serikali kwa wakimbizi na makada wa LTTE ambao wamesalimu amri. | |
26 | Katika miaka mitatu iliyopita kumekuwa na matukio mengi ya utekaji, mauaji na kutoweka kwa watu, kulikolenga jamii ya Watamil wakati ambapo serikali ya Sri Lanka ilipokuwa ikitekeleza kampeni yake ya kijeshi. | |
27 | Kushamiri kwa uongozi wa kijeshi kitaifa na kwenye jamii kumefanikisha ukandamizwaji wa maoni mbadala kusini mwa nchi, na kumewezesha mashambulizi dhidi ya wanahabari. Tunasuburi ili tuone kama serikali itageuza mwelekeo huu mbaya wa utawala wa kidemokrasi. | 但政府拒绝让人道组织自由进入,让外界不免怀疑,政府究竟打算如何处置难民及投降的游击队成员,许多坦米尔人在过去三年遭 到绑 架、非法杀害及失踪,几乎都是政府军事行动下的受害者,国家与社会走向军事化,过去不断压制南部异议,甚至增加攻击记者的情况,我们会继续观察,看看政府 能否扭转民主治理的退步情况。 |
28 | Akiwa safarini, mwanablogu na mwandishi wa makala Indi Sumarajiya ametumia zana ya Twita kujadili kifo cha Prabhakaran. | 博客兼专栏作家Indi Samarajiva运用Twitter,在旅途中表达对普拉巴卡兰死亡的看法,他在5月18日下午的Twitter讯息指出: |
29 | Alituma jumbe kadhaa kwenye ukurasa wake wa Twita jumatatu mchana: Nipo Hambantota. | 我正在Hambantota,有爆竹声,普拉巴卡兰好像死亡,死得并不光彩,但是件好事,愿斯里兰卡能重建。 |
30 | Fataki. Pengine Prabhakan amefariki. | 他们在天然气槽不远处燃放鞭炮,鱼贩回去工作时也大声欢呼。 |
31 | Hakuna utukufu kwenye kifo, lakini, ni vyema. Tunaomba Sri Lanka ijijenge upya#fb | Hambantota地区居民大多是穆斯林,现在已恢复正常,国旗车队一路驶过Ambalantota,战争终于结束,普拉巴卡兰死亡,斯里兰卡万岁。 |
32 | Wanawasha baruti karibu kabisa na ghala ya mitungi ya gesi. Wauza samaki wanahimizwa kurejea kazini. | 印度清奈博客Prahalathan KK表示,若对普拉巴卡兰的死亡感到高兴,等于忽视在攻击游击队期间丧生的民众: |
33 | Mji wa Hambantota una Waislamu wengi, kazi inaendelea. | 恐怖份子普拉巴卡兰已死亡,高兴吗? |
34 | Misafara ya bendera katika Ambalantota. | 愉快吗? |
35 | Vita vimekwisha, Prabha amekufa. Idumu Sri Lanka #fb | 就算政府军在这场屠杀战里,动用军火及化学武器,造成无数坦米尔人丧生,你们也是同样态度? |
36 | Mwanablogu aliyeko mjini Chennai, India, Prahalathan KK, anasema kuwa kushangilia kifo cha Prabhakaran ni utovu wa heshima kwa raia waliouwawa katika harakati za kuwezesha maangamizi ya LTTE. | |
37 | “Kwa hiyo Prabhakaran gaidi ameuwawa. Mmefurahi? | 据国防部网站指出,过去不到一个月时间,近15万平民逃离战区,都由军方负责照顾,但唯一能进入战区的国际红十字会表示,「情况与灾难无异」。 |
38 | Mnashangilia? Je mmeweza kuwafikiria maelfu ya Watamil wasio na hatia ambao waliuwawa kutokana na matumizi ya jumla ya makombora na silaha za sumu yaliyofanywa na jeshi la Sri Lanka wakati wa vita hivi vya kimbari? | 今天在新闻稿里,红十字会表示已长达九天无法前进东北部地区,主管Pierre Krähenbühl认为:「由于人道救援已超过一星期无法抵达民众手中,情况相当危急」;游击队国际外交部门负责人Selvarasa Pathmanathan在5月17日发布声明,强调游击队将「停火以保护人民」,他的资料显示有3000位平民死亡、25000人受伤。 |
39 | Kwa mujibu wa tovuti ya Wizara ya ulinzi, karibu ya raia 150,000 ambao walikimbia uwanja wa vita wanatunzwa na na jeshi. | |
40 | Lakini Kamati ya Kimataifa ya Hilali Nyekundu (ICRC), shirika huru pekee ambalo liliweza kuwafikia raia katika eneo la mgogoro, liliita hali iliyokuwepo kama “si jingine zaidi ya balaa.” | |
41 | Leo hii, wamesema katika taarifa yao kwa vyombo vya habari kwamba hawajaweza kuwafikia raia walioko kaskazini-mashariki kwa siku tisa. | 知名南亚侨民博客Sepia Mutiny提到加拿大有抗争持续发生,关于在温尼伯(Winnipeg)的集会: |
42 | “Hii ni dharura kwani hakuna msaada wowote wa kibinaadamu ambo umeweza kuwafikia wale wanaouhitaji kwa zaidi ya wiki moja'” alisema mkurugenzi wa mipango, Pierre Krähenbühl. Selvarasa Pathmanathan, mkuu wa kitengo cha Diplomasia cha LTTE, alitoa tamko Jumapili kuwa Chui “tutanyamazisha bunduki zetu ili kuwanusuru watu wetu.” | 他们手持蜡烛、标语、黑旗,以及政府军攻击下的受害儿童照顾,当斯里兰卡各地民众庆祝25年的内战告终,参与守夜的人民为 无辜民 众而哀悼,并怀疑这样是否解决任何问题,Singarajah说:「什么事都没解决,人民的苦难不会结束,政府实在无情,他们不愿意给予我们应有权利,只 要现况不变,问题就会延续下去。」 |
43 | Alisema kuwa raia 3,000 walifariki na wengine 25,000 walijeruhiwa. Blogu maarufu ya Waasia wa Kusini Ughaibuni Sepia Mutiny inaripoti maandamano yanayoendelea nchini Kanada. | 英国伦敦、加拿大各处及澳洲也有抗议活动,但社运人士Rajasingam在《外交政策》杂志警告,坦米尔侨民的表达方式会令人误解: |
44 | Katika makala inayohusu maandamano huko Winnipeg, Melvin anaandika: Walibeba mishumaa, mabango, bendera nyeusi na picha za watotot ambao wanawachukulia kama waathirika wa mashambulizi ya serikali ya Sri Lanka dhidi ya raia. | 随着斯里兰卡人道危机持续延烧,国际社会必须获得清楚明白的讯息,游击队与侨民并非坦米尔人的「唯一代言人」,分裂也不是 合理选 项,在西方世界的游击队说客若提出各种肤浅要求,而非实质参与,必然会引起斯里兰卡国内僧伽罗民族主义者的愤怒,只有坚定的和平及民主讯息才能发挥功用。 |
45 | Wakati ambapo watu jijini Colombo walikuwa wakisherehekea mwisho wa miaka 25 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, wale waliokuwa kwenye maandamano walikuwa wanaomboleza vifo vya raia wasio na hatia huku wakijiuliza, ni nini, kuma kuna chochote, kilichopatiwa ufumbuzi. | |
46 | “haijasuluhisha lolote,” alisema Singaraja. “Kero za wananchi hazitaisha. | Moving Images, Moving People! |
47 | Serikali ni katili mno. Hawataki kutupatia haki zetu. | 博客的Nalaka Gunawardene表示,他希望相信战争真已结束: |
48 | Na kama ni hivyo, matatizo yataendelea.” Maandamano yamekuwa yakiendelea jijini London, katika sehemu nyingi za Canada na hivi karibuni nchini Australia. | 这一切并无独立的衡量标准,过去几年这场战争都欠缺目击者,但我仍愿意秉持不寻常的信念,促成长久期望的和平,我会走至天涯海角,放弃任何不信任的基础,以换取长永的和平。 |
49 | Mwanaharakati Rajasingham anaonya kwenye jarida la Foreign Policy kwamba Watamil walio ughaibuni wamechukulia vibaya ujumbe wake: | |
50 | Wakati mgogoro wa kibinaadamu unavyojitokeza nchini Sri Lanka, jumuia ya kimataifa inabidi itoe tamko wazi na la moja kwa moja. | |
51 | Kwamba waasi na Watamil wanawaunga mkono ambao wanaishi ughaibuni hawana hati miliki ya kuwa “wawakili pekee” wa Watamil wote. | |
52 | Na kujitenga siyo suluhisho pekee. | |
53 | Njia nyingine yoyote isipokuwa mapambano imara kungetumiwa na waunga mkono wa LTTE walio nchi za magharibi - na kuwachochea wazalendo wa Ki-Sinhala nchini Sri Lanka. | |
54 | Ni ujumbe huu imara pekee ambao utapelekea amani na demokrasia. Kwenye tovuti ya Moving Images, Moving People! | 总统拉贾帕克萨(Mahinda Rajapaksa)预订于5月19日早晨向国会及全国发表演说。 |
55 | Mwanablogu Nalaka Gunawardene anasema kuwa angependa kuamini, kwa hakika, kuwa vita vimekwisha: | |
56 | Hakuna vidhibitisho huru - vimekuwa ni vita visivyokuwa na shahidi kwa miaka michache iliyopita. | |
57 | Lakini nipo tayari kuwa na imani isiyo ya kawaida, ikiwa kama ni hilo tu linalohitajika ili kukaribisha amani iliyotuchenga kwa muda mrefu. | |
58 | Nitakwenda mpaka mwisho wa dunia, ili kusimamisha kutoamini kwangu, ili kupokea kurejea kwa amani na amani yenye maana. | |
59 | Rais Mahinda Rajapaksa anategemewa kulihutubia Bunge na taifa jumanne asubuhi. | 校对:Soup |