# | swa | zhs |
---|
1 | Irani: Ziara ya Rais Ahamdinejad Nchini Lebanoni Rais wa Irani, Mahmoud Ahmadinejad, amemaliza ziara yake ya siku mbili nchini Lebanoni. | 伊朗:总统出访黎巴嫩 |
2 | Ilikuwa ni ziara yake rasmi ya kwanza tangu mwaka 2005 wakati alipochukua madaraka. Alikuwa na mazungumzo na maofisa wa Lebanoni na alizuru ngome za maswahiba wa Irani, Hezbollah, katika vitongoji vya kusini mwa mji mkuu na kusini mwa Lebanoni ambako alipata mapokezi ya shujaa. | 伊朗总统阿曼尼内贾德(Mahmoud Ahmadinejad)刚结束黎巴嫩的两天访问行程,这是他自2005年上任以来,首次出访该国,除了与官员会晤,亦前往首都南部郊区及黎国南部,获得如英雄式的接待,这两地均为真主党重镇,该组织和伊朗往来相当密切。 |
3 | Wanablogu kadhaa wa Irani walitoa maoni kuhusu ziara hiyo. | 对此次出访,多位伊朗博客都表达看法。 |
4 | Meybodema amechapisha picha kadhaa za ziara ya Ahmadinejad nchini Lebanoni na kumnukuu [fa] Sayyid Hassan Nasrallah, kiongozi wa Hezbollah, ambaye aliisifu Jamhuri ya Kiislamu na kumkaribisha Ahmadinejad. | Meybodema张贴几张访问行程照片,并引述真主党领袖纳斯拉亚(Sayyid Hassan Nasrallah)的言论,赞扬伊朗与欢迎阿曼尼内贾德。 |
5 | Mwanablogu huyo alimnukuu Nasrallah akisema kwamba kinyume na propaganda zote, “Irani inawasaidia wanaokandamizwa”. | 纳斯拉亚表示,伊朗所为与所有政治宣传相反,“是在帮助受迫害者”。 |
6 | Sayeh Azadi alichapisha tena (tafadhali angalia hapo juu) kikaragosi kilichochorwa na mchoraji vikaragosi anayeongoza nchini Irani Nikahang kutoka kwenye Roozonline [fa] kikaragosi hicho kilikuwa na kichwa cha habari kinachosema “Ndoto za Ahmadinejad kwa Lebanoni”. | Sayeh Azadi转载(见上图)知名伊朗漫画家Nikahang在Roozonline张贴的漫画,图说写着“阿曼尼内贾德的黎巴嫩美梦”。 |
7 | Z8unak anahesabu sababu zinazoeleza ni kwa nini watu wa Lebanoni walimkaribisha Ahmadinejad. | Z8unak写下黎巴嫩人民欢迎阿曼尼内贾德的原因: |
8 | Mwanablogu huyo anaandika [fa]: | 阿曼尼内贾德在黎巴嫩受到热情欢迎,各位为何惊讶? |
9 | Kwa nini mlishangaa kwamba Ahmadinejad alipokelewa vizuri mno nchini Lebanoni? | 两伊战争结束至今已20年,伊朗边境城市尚未重建,但黎巴嫩的房屋却是用伊朗经费重建;每天都有许多伊朗民众无法负担医疗费用而死亡,但伊朗却为黎巴嫩兴建医院。 |
10 | Baada ya miaka 20 ya vita vya Iraki-Irani, miji ya mpakani haikujengwa lakini nyumba nchini Lebanoni zilijengwa kwa pesa zetu. | Mollah以讽刺口吻写道: |
11 | WaIrani wengi hawawezi kumudu kwenda kwa daktari au hospitali na matokeo yake wanakufa kila siku, wakati huo huo irani inajenga hospitali nchini Lebanoni. Mollah anaandikakwa kejeli: | 黎巴嫩民众没看到伊朗政府做任何坏事,若我们是黎巴嫩人,又拿到钱,我们都会成为伊朗的支持者,他们说,我们不在乎这些人是否以政变上台或虐待人民…把钱拿来就可以。 |
12 | WaLebanoni hawakuona ubaya wowote wa serikali ya Irani. | 校对:Soup |
13 | Kama tungekuwa WaLebanoni na kupokea pesa hizo tungegeuka kuwa waunga mkono wa Jamhuri ya Kiislamu… Wanasema, hartujali ikiwa wapo madarakani baada ya ‘mapinduzi ya nguvu' au ikiwa wanatesa watu… ili mradi wanatoa pesa. | |