# | swa | zht |
---|
1 | Marekani: Mauaji ya Fort Hood Yasababisha Kumulikwa kwa Waislamu Walio Jeshini | 美國:軍營殺人事件與穆斯林身分 |
2 | Shambulizi la upigaji risasi la kushtukiza lililofanywa na mwanajeshi wa Jeshi la Marekani, Meja Nidal Malik Hassan, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine 31 katika kambi ya kijeshi ya Fort Hood, jimbo la Texas, kwa mara nyingine limesababisha Waislamu nchini Marekani kumulikwa - hasa wale wanaolitumikia jeshi. | |
3 | Kitambo kifupi baada ya Meja Hassan kutangazwa kama mfyatuaji aliyetuhumiwa, kulikuwa na kukosa raha kuliko wazi kabisa miongoni mwa warusha habari na watoa maoni kuhusu usuli wake wa kidini na asili yake. Iliripotiwa pia kwa wingi kwamba wanajeshi wengine wa Kiislamu mara nyingine walikabiliana na mashambulizi kutoka kwa wanajeshi wenzao. | 美國軍官Nidal Malik Hasan在德州Fort Hood的掃射行動造成13人死亡、31人受傷,再度讓美國穆斯林(尤其是穆斯林軍人)成為輿論焦點。 |
4 | Howard M. Friedman, Profesa Mwandamizi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Toledo, anasema katika blogu yake ijulikanayo kama ReligionClause: | 警方公佈嫌犯為這位軍官後,新聞媒體與評論員顯然對他的宗教與種族背景感到不安,過去不時有報導指稱,穆斯林在軍中遭到同袍攻擊。 |
5 | “Jeshi limekuwa likiandikisha Waislamu walio na ujuzi wa lugha na welewa wa utamaduni, vitu vinavyohitajika ili kupigana vita huko Iraki na Afganistani. | 托雷多大學榮譽法學教授Howard M. |
6 | Hata hivyo, Waislamu walio jeshini sasa wanatiliwa shaka na baadhi ya maofisa wao.” | Friedman在ReligionClause部落格表示: |
7 | Bila kujali mashaka dhidi ya wanajeshi Waislamu yaliyokuwapo kabla ya shambulizi hili, mtu anaweza kuwa na hofu kwamba mashaka hayo yamepata msukumo mpya baada ya mauaji ya watu kule Fort Hood. | 軍方一直積極招募穆斯林入伍,因為在伊拉克與阿富汗戰事中,他們具備當地語言技能及文化素養,但穆斯林在軍旅中當受部分同袍的異樣眼光。 |
8 | Maswali bado yanaendelea kuibuliwa endapo Meja Hassan alikuwa mwenye siasa kali na ambaye alifanya mashambulizi hayo kwa msukumo wa itikadi ya kidini au labda tu alikuwa na tatizo la kiakili. | 無論過往外界對穆斯林軍人有多少質疑,在此次大規模殺人事件後,這種懷疑肯定會愈來愈多,也有人在討論,這名軍官究竟是因極端宗教意識型態而痛下殺機,抑或只是罹患心理疾病。 |
9 | Kule Kanada, mwandishi Gwynne Dyer wa gazeti huru la kila wiki la Vancouver kupitia mtandao wa Straight.com, anabuni kwamba kuelekeza fikra kwenye dini ya muuaji ni kufumbia macho baadhi ya masuala mengine muhimu: | 作家Gwynne Dyer在加拿大溫哥華免費週報Straight.com認為,兇手的宗教背景掩蓋某種重要議題: |
10 | “Baada ya siku chache wakati watoa maoni wakisitasita kutoa maelezo yanayoshindana, vyombo vya habari vinaanza kujikita katika maelezo kwamba ilikuwa ni unyanyasaji wa kirangi/kiasili/kidini ndiko kulikomsukuma Nidal kupata ukichaa. | 評論員起初幾天都不敢妄下斷言,之後媒體才定調是因為族群/種族/宗教歧視讓這位軍官發瘋,認為這場悲劇是因為壞人犯下不符美國精神的行為。 |
11 | Watu wabaya, wanaofanya vitu kinyume na Wamarekani mwisho wa siku ndiyo wenye kuhusika na msiba huo, na kuna mwisho wake. Maelezo yanayokwepwa ni kwamba vita vya Wamarekani vinavyoendeshwa ng'ambo katika ardhi za Waislamu vinawajenga Waislamu nyumbani kuchukua msimamo mkali. | 這種詮釋忽略因為美軍出兵伊斯蘭世界,造成國內穆斯林趨於激進,無論是2005年在英國倫敦地鐵犯案的伊斯蘭恐怖份子,或是其他西方國家在案發前便破獲的 恐怖主義陰謀,這些穆斯林都指控西方世界入侵伊斯蘭國家,才讓他們變得激進,況且到頭來,這些西方國家的軍事行動也未提高國家安全。 |
12 | Usijali sana kwamba magaidi wa Kiislamu waliokuzwa nyumbani walioshambulia mfumo wa usafiri jijini Landani mwaka 2005, na wafanya njama wa Kiislamu kadhaa ambao wamekamatwa katika nchi za Magharibi kabla njama zao hazijazaa matunda, wote wamelaumu uvamizi unaofanywa na mataifa ya Magharibi kwenye nchi za Kiislamu kama kitendo kilichowasukuma wao kuwa na msimamo mkali. | |
13 | Zaidi sana, usijali kwamba kile kilichowafanya kuwa na msimamo mkali ni ukweli kwamba uvamizi huo haukuwa na maana kwa masuala ya usalama wa Magharibi.” Fox News, ambayo mara nyingi hukosolewa kwa kuelemea kwake upande mmoja katika masuala yanayohusiana na uhamiaji na siasa mgando, inasemekana kuitisha wazo la “uchunguzi kwa Waislamu” walio jeshini. | 美國福斯新聞台對移民及保守政治立場向來受到詬病,此次該頻道要求軍方「審查穆斯林」,美國海岸防衛隊退役軍官Tom Barnes在Veterans Today網站上表示,福斯新聞台又在操弄「敵我對立」的緊張關係: |
14 | Katika tovuti ya Veterans Today, ofisa mstaafu wa Jeshi la Ulinzi wa Pwani ya Marekani, United States Coast Guard, Tom Barnes, anasema chombo hicho cha habari kinachochea mtazamo uleule wa siku zote kwa kujaribu kujenga imani potofu ya “sisi dhidi ya wao”: | …這個頻道實在對社會沒有幫助,將原本合理的問題又轉變成福斯新聞台的十字軍東征,這種角度不僅老套、而且危險,相關報導請見此。 |
15 | “… chombo hicho cha habari kinazidi kuwa “kisichosaidia”, yaani kwa lugha nyepesi, hasa kama swali hili la msingi linageuka kuwa vita nyingine ya Fox Channel dhidi “yao”. Taarifa kama hizi siyo tu zinazidi kupitwa na wakati bali ni za hatari pia. | 如前所述,此類事件過去也曾在美軍內部發生,我已厭倦由福斯新聞台告訴我誰是敵人,他們總是一而再地這麼做,我根本不覺得社會有這麼多敵人! |
16 | Hapa ndipo palipo na habari nzima. Kama nilivyoonyesha hapo kabla, jambo kama hili limewahi kutokea katika Jeshi la Ulinzi la Marekani. | 多家報紙已在分析,此次事件會如何影響穆斯林在美軍內部及Fort Hood附近地區的處境。 |
17 | Ninazidi kuchoshwa na habari za Fox News zinazoniambia kuwa adui zangu ni akina nani. Kila wakati. | euroamericannews在YouTube網站上提供一段畫面,由Fort Hood地區穆斯林表達對此事的看法: |
18 | Bila kukoma. Sikuwa na habari kwamba “wao” wapo wengi!” | 案件調查尚在進行中,穆斯林美軍所受注目一時間還不會消退。 |
19 | Magazeti mengi hivi sasa yanachunguza ni kwa namna gani vitendo vya Hassan vitawaathiri Waislamu wanaotumikia katika Jeshi la Marekani, na wakazi Waislamu wanaoishi karibu na kambi ya Fort Hood. | |
20 | Hapa kuna taarifa ya habari ya video ya euroamericannews katika YouTube kuhusu maoni ya Waislamu walio Fort Hood kuhusiana na tukio hilo. | |
21 | Wakati ambapo uchunguzi wa mauaji hayo unaendelea, bila shaka jicho litaendelea kutupwa wa Waislamu wanaotumikia jeshi. | 校對:Soup |