# | swa | zht |
---|
1 | Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE | 斯里蘭卡:部落客關注游擊隊領袖身亡消息 |
2 | Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. | |
3 | Vyombo vya habari vinaripoti kwamba Prabhakaran, ambaye alikuwa kwenye uongozi wa moja ya maasi ya kikatili zaidi duniani, aliuwawa kwa kombora wakati alipokuwa kwenye basi dogo na mkuu wa jeshi la majini la LTTE, Soosai, pamoja na mkuu wa upelelezi, Pottu Amman. | |
4 | Mwili wa kiongozi huyo wa waasi utafanyiwa uchunguzi zaidi wa DNA ili kuthibitisha utambuzi wake. Kadri ya wanachama 250 wa waasi wa Chui wa Kitamil waliuwawa kwenye mapambano ya mwisho ya vita vilivyodumu kwa miaka 26. | 斯里蘭卡政府透過國營媒體及手機簡訊,於當地時間5月18日下午宣佈,國內游擊隊「坦米爾之虎」領袖普拉巴卡蘭(Vellupillai Prabhakaran)已身亡,新聞媒體報導,普拉巴卡蘭與游擊隊海軍首長Soosai及情報首長Pottu Amman共乘汽車時,遭到火箭攻擊死亡。 |
5 | Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika alichukuliwa kama muuaji katili kwa wengine. | 斯里蘭卡歷經26年戰火,在最近一波攻擊中,據稱約有250名游擊隊成員遭格斃。 |
6 | Chombo cha habari cha BBC kimeandika, “kwa wafuasi wake, Vellupillai Prabhakaran alikuwa ni mpigania uhuru kwa ajili ya ukombozi wa Watamil. | |
7 | Kwa maadui zake alikuwa ni mtu msiri anayependa kutawala na asiyejali kabisa maisha ya wanaadamu wengine.” Gazeti la The Hindu nchini India linasema, Mpigania uhuru kwa wafuasi wake na gaidi wa kuogopwa kwa wengine, Prabhakaran alikuwa anatafutwa na Chombo cha Polisi cha Kimataifa, Interpol, pamoja na mashirika mengine mengi tangu mwaka 1990 kwa makosa ya ugaidi, mauaji na jinai. | 在關於普拉巴卡蘭的訃聞裡,有些人稱之為英雄,有些人稱之為無情殺手,英國廣播公司指出,「對支持者而言,普拉巴卡蘭是為爭取坦米爾解放的自由鬥士;對敵人而言,他是個神秘的自大狂,毫不尊重人命」;印度《The Hindu》 寫道:「支持者眼中的『自由鬥士』,也是他人眼中的恐怖份子,普拉巴卡蘭自1990年便因恐怖主義、謀殺與組織犯罪,遭國際刑警組嬂等機構追緝」。 |
8 | “kabla dunia haijamsikia Osama Bin Laden au Al-Qaeda, Prabhakaran alianza kutumia mbinu mpya ya vita, mabomu ya kujilipua kwa kujitoa muhanga. Makala hii kwenye gazeti la Tehelka inatoa mwanga kuhusu kiongozi huyu wa vita. | 早在世 界還不認識蓋達組織和賓拉登(Al-Qaeda)之前,普拉巴卡蘭便已使用自殺炸彈這種新游擊戰術,《Tehelka》雜誌的封面故事記錄這位軍閥的許多故事。 |
9 | Mwanablogu wa Beyond the Skin anafafanua hivi: Hisia za mwanzo: WHAAA! | Beyond Skin部落格解釋: |
10 | [vipele vya baridi, kushuka tama na hisia mchanganyiko za hjofu na ahueni.] Hisia zilizofuata: Sasa nini? | 起初反應是一陣驚訝(起了雞皮疙瘩,下巴也快掉下來,也同時出現恐懼和輕鬆兩種情緒)。 |
11 | Baada ya miaka 26 ya mapambano, baada ya kuua mamia ya maelfu, baada ya kuwanyamazisha wale walioipinga serikali na waasi wa LTTE kwa kuwaua, mateso na watu kupotea, sasa itakuwaje kwa watu wa Tamil? | |
12 | Kada wa chama cha United National Party Ajith P. | 第二項反應:接下來怎麼辦? |
13 | Perera ameandika salamu za rambirambi kwa Prabhakaran katika blogu yake, akitaka kuwa tofauti na wengine: “alikuwa muuaji, bila ya shaka, lakini Prabhakaran anastahili salamu za rambirambi, hata kama ni katika lugha ambayo alikuwa haielewi,” | |
14 | Je alifanikisha lolote la maana kwa ajili ya jamii yake? | |
15 | Jibu ni HAPANA. Watamil wazawa (Jaffna) wako pabaya zaidi ya pale walipokuwa katika miaka ya 1970. | 經過26年奮鬥,無數人遭到殺害或被迫離家,透過暗殺、虐待和強行帶走失蹤後,壓制反對政府與游擊隊的異議後,坦米爾人的下一步是什麼? |
16 | Zaidi ya nusu ya Watamil wamehama moja kwa moja. | 「聯合國家黨」領袖Ajith P. |
17 | Watamil Wazawa, kundi kubwa la walio wachache nchini Sri Lanka wakati ule, hivi sasa wapungua na kuchukua nafasi ya tatu baada ya Waislamu na Watamil wanaotokea India. | |
18 | Jaffna, jiji la pili kimaendeleo nchini Sri Lanka, na mfumo wake maarufu wa elimu, hivi sasa iko nyuma sana. Kama jamii, Watamil, wale walio na bahati mbaya ya kubaki, wamerudi nyuma miaka kumi au ishirini. | Perera在部落格Dare to be different留下對普拉巴卡蘭的描述:「普拉巴卡蘭無疑是個恐怖份子,但他理應獲得一份坦米爾文的訃文,縱然他幾乎聽不懂這種語言」。 |
19 | Walitambuliwa kama magaidi duniani kote. | 他為這個社群有達到任何重大目標嗎? |
20 | Kaskazini na mashariki pamekuwa tegemezi kwa Colombo kiuchumi. Kwa miaka michache ijayo, mpaka hapo serikali ya UNP itakapotekeleza sera zake kisiasa, watakuwa wanaendeshwa kutokea Colombo. | 完全沒有,坦米爾人今日情況比七零年代還糟,逾半數坦米爾人已永遠離開,無數坦米爾家庭因失 去親人,必須承擔永恆的痛苦,坦米爾人原是斯里蘭卡最大少數族群,如今卻落於穆斯林及印度裔坦米爾人之後;Jaffna原在斯里蘭卡進步程度居全國第二, 如今已遙遙落後。 |
21 | Yote haya ni shukrani kwa Prabhakaran. Mwanaharakati wa Kitamil na mwanachama wa zamani wa waasi wa LTTE Nirmala Rajasingam anafafanua katika makala kwenye gazeti la Independent kwamba dada yake aliuwawa na waasi wa LTTE miaka 20 iliyopita. | 坦米爾人這個族群的生活倒退了一二十年,全世界稱他們是恐怖份子,國內東部及北部地區在經濟上日益仰賴首都可倫坡,至少在未來幾年,除非 「聯合國家黨」政府落實解決方案,他們將永遠受首都搖控,一切都是拜普拉巴卡蘭之賜。 |
22 | Kwa sababu hiyo, habari za maangamizi ya uongozi wa juu wa LTTE - ambao uliamuru kuuwawa kwake pamoja na Watamil wengine wengi waliowapinga - kumeleta ahueni kubwa sana. | 斯里蘭卡坦米爾運動人士兼前游擊隊成員Nirmala Rajasingam在《獨立報》投書中,表示自己的姐姐在20年前便遭游擊隊殺害: |
23 | Vita na ukatili hatimaye vimesitishwa na kumwagika kwa damu za Watamil kumefikia mwisho. | 當初就是游擊隊首領下令殺害她和其他異議份子,故聽聞普拉巴卡蘭的死訊,我著實鬆了一口氣,戰爭與屠殺終於劃下休止符,坦米爾異議人士的血液也不用再流。 |
24 | Hata hivyo anaonya: | 但她提醒: |
25 | Pingamizi linaloendela la kutoruhusu mashirika ya misaada ya kibinaadamu kuingia halisaidii kupunguza mashaka juu ya nia ya serikali kwa wakimbizi na makada wa LTTE ambao wamesalimu amri. | |
26 | Katika miaka mitatu iliyopita kumekuwa na matukio mengi ya utekaji, mauaji na kutoweka kwa watu, kulikolenga jamii ya Watamil wakati ambapo serikali ya Sri Lanka ilipokuwa ikitekeleza kampeni yake ya kijeshi. | |
27 | Kushamiri kwa uongozi wa kijeshi kitaifa na kwenye jamii kumefanikisha ukandamizwaji wa maoni mbadala kusini mwa nchi, na kumewezesha mashambulizi dhidi ya wanahabari. Tunasuburi ili tuone kama serikali itageuza mwelekeo huu mbaya wa utawala wa kidemokrasi. | 但政府拒絕讓人道組織自由進入,讓外界不免懷疑,政府究竟打算如何處置難民及投降的游擊隊成員,許多坦米爾人在過去三年遭到綁 架、非法殺害及失蹤,幾乎都是政府軍事行動下的受害者,國家與社會走向軍事化,過去不斷壓制南部異議,甚至增加攻擊記者的情況,我們會繼續觀察,看看政府 能否扭轉民主治理的退步情況。 |
28 | Akiwa safarini, mwanablogu na mwandishi wa makala Indi Sumarajiya ametumia zana ya Twita kujadili kifo cha Prabhakaran. | 部落客兼專欄作家Indi Samarajiva運用Twitter,在旅途中表達對普拉巴卡蘭死亡的看法,他在5月18日下午的Twitter訊息指出: |
29 | Alituma jumbe kadhaa kwenye ukurasa wake wa Twita jumatatu mchana: Nipo Hambantota. | 我正在Hambantota,有爆竹聲,普拉巴卡蘭好像死亡,死得並不光彩,但是件好事,願斯里蘭卡能重建。 |
30 | Fataki. Pengine Prabhakan amefariki. | 他們在天然氣槽不遠處燃放鞭炮,魚販回去工作時也大聲歡呼。 |
31 | Hakuna utukufu kwenye kifo, lakini, ni vyema. Tunaomba Sri Lanka ijijenge upya#fb | Hambantota地區居民大多是穆斯林,現在已恢復正常,國旗車隊一路駛過Ambalantota,戰爭終於結束,普拉巴卡蘭死亡,斯里蘭卡萬歲。 |
32 | Wanawasha baruti karibu kabisa na ghala ya mitungi ya gesi. Wauza samaki wanahimizwa kurejea kazini. | 印度清奈部落客Prahalathan KK表示,若對普拉巴卡蘭的死亡感到高興,等於忽視在攻擊游擊隊期間喪生的民眾: |
33 | Mji wa Hambantota una Waislamu wengi, kazi inaendelea. Misafara ya bendera katika Ambalantota. | 恐怖份子普拉巴卡蘭已死亡,高興嗎? |
34 | Vita vimekwisha, Prabha amekufa. Idumu Sri Lanka #fb | 愉快嗎? |
35 | Mwanablogu aliyeko mjini Chennai, India, Prahalathan KK, anasema kuwa kushangilia kifo cha Prabhakaran ni utovu wa heshima kwa raia waliouwawa katika harakati za kuwezesha maangamizi ya LTTE. | |
36 | “Kwa hiyo Prabhakaran gaidi ameuwawa. Mmefurahi? | 就算政府軍在這場屠殺戰裡,動用軍火及化學武器,造成無數坦米爾人喪生,你們也是同樣態度? |
37 | Mnashangilia? Je mmeweza kuwafikiria maelfu ya Watamil wasio na hatia ambao waliuwawa kutokana na matumizi ya jumla ya makombora na silaha za sumu yaliyofanywa na jeshi la Sri Lanka wakati wa vita hivi vya kimbari? | 據國防部網站指出,過去不到一個月時間,近15萬平民逃離戰區,都由軍方負責照顧,但唯一能進入戰區的國際紅十字會表示,「情況與災難無異」。 |
38 | Kwa mujibu wa tovuti ya Wizara ya ulinzi, karibu ya raia 150,000 ambao walikimbia uwanja wa vita wanatunzwa na na jeshi. Lakini Kamati ya Kimataifa ya Hilali Nyekundu (ICRC), shirika huru pekee ambalo liliweza kuwafikia raia katika eneo la mgogoro, liliita hali iliyokuwepo kama “si jingine zaidi ya balaa.” | 今天在新聞稿裡,紅十字會表示已長達九天無法前進東北部地區,主管Pierre Krähenbühl認為:「由於人道救援已超過一星期無法抵達民眾手中,情況相當危急」;游擊隊國際外交部門負責人Selvarasa Pathmanathan在5月17日發佈聲明,強調游擊隊將「停火以保護人民」,他的資料顯示有3000位平民死亡、25000人受傷。 |
39 | Leo hii, wamesema katika taarifa yao kwa vyombo vya habari kwamba hawajaweza kuwafikia raia walioko kaskazini-mashariki kwa siku tisa. | 知名南亞僑民部落格Sepia Mutiny提到加拿大有抗爭持續發生,關於在溫尼伯(Winnipeg)的集會: |
40 | “Hii ni dharura kwani hakuna msaada wowote wa kibinaadamu ambo umeweza kuwafikia wale wanaouhitaji kwa zaidi ya wiki moja'” alisema mkurugenzi wa mipango, Pierre Krähenbühl. Selvarasa Pathmanathan, mkuu wa kitengo cha Diplomasia cha LTTE, alitoa tamko Jumapili kuwa Chui “tutanyamazisha bunduki zetu ili kuwanusuru watu wetu.” | 他們手持蠟燭、標語、黑旗,以及政府軍攻擊下的受害兒童照顧,當斯里蘭卡各地民眾慶祝25年的內戰告終,參與守夜的人民為無辜民 眾而哀悼,並懷疑這樣是否解決任何問題,Singarajah說:「什麼事都沒解決,人民的苦難不會結束,政府實在無情,他們不願意給予我們應有權利,只 要現況不變,問題就會延續下去。」 |
41 | Alisema kuwa raia 3,000 walifariki na wengine 25,000 walijeruhiwa. Blogu maarufu ya Waasia wa Kusini Ughaibuni Sepia Mutiny inaripoti maandamano yanayoendelea nchini Kanada. | 英國倫敦、加拿大各處及澳洲也有抗議活動,但社運人士Rajasingam在《外交政策》雜誌警告,坦米爾僑民的表達方式會令人誤解: |
42 | Katika makala inayohusu maandamano huko Winnipeg, Melvin anaandika: Walibeba mishumaa, mabango, bendera nyeusi na picha za watotot ambao wanawachukulia kama waathirika wa mashambulizi ya serikali ya Sri Lanka dhidi ya raia. | 隨著斯里蘭卡人道危機持續延燒,國際社會必須獲得清楚明白的訊息,游擊隊與僑民並非坦米爾人的「唯一代言人」,分裂也不是合理選 項,在西方世界的游擊隊說客若提出各種膚淺要求,而非實質參與,必然會引起斯里蘭卡國內僧伽羅民族主義者的憤怒,只有堅定的和平及民主訊息才能發揮功用。 |
43 | Wakati ambapo watu jijini Colombo walikuwa wakisherehekea mwisho wa miaka 25 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, wale waliokuwa kwenye maandamano walikuwa wanaomboleza vifo vya raia wasio na hatia huku wakijiuliza, ni nini, kuma kuna chochote, kilichopatiwa ufumbuzi. | |
44 | “haijasuluhisha lolote,” alisema Singaraja. “Kero za wananchi hazitaisha. | Moving Images, Moving People! |
45 | Serikali ni katili mno. Hawataki kutupatia haki zetu. | 部落格的Nalaka Gunawardene表示,他希望相信戰爭真已結束: |
46 | Na kama ni hivyo, matatizo yataendelea.” Maandamano yamekuwa yakiendelea jijini London, katika sehemu nyingi za Canada na hivi karibuni nchini Australia. | 這一切並無獨立的衡量標準,過去幾年這場戰爭都欠缺目擊者,但我仍願意秉持不尋常的信念,促成長久期望的和平,我會走至天涯海角,放棄任何不信任的基礎,以換取長永的和平。 |
47 | Mwanaharakati Rajasingham anaonya kwenye jarida la Foreign Policy kwamba Watamil walio ughaibuni wamechukulia vibaya ujumbe wake: | |
48 | Wakati mgogoro wa kibinaadamu unavyojitokeza nchini Sri Lanka, jumuia ya kimataifa inabidi itoe tamko wazi na la moja kwa moja. | |
49 | Kwamba waasi na Watamil wanawaunga mkono ambao wanaishi ughaibuni hawana hati miliki ya kuwa “wawakili pekee” wa Watamil wote. | |
50 | Na kujitenga siyo suluhisho pekee. | |
51 | Njia nyingine yoyote isipokuwa mapambano imara kungetumiwa na waunga mkono wa LTTE walio nchi za magharibi - na kuwachochea wazalendo wa Ki-Sinhala nchini Sri Lanka. | |
52 | Ni ujumbe huu imara pekee ambao utapelekea amani na demokrasia. Kwenye tovuti ya Moving Images, Moving People! | 總統拉賈帕克薩(Mahinda Rajapaksa)預訂於5月19日早晨向國會及全國發表演說。 |
53 | Mwanablogu Nalaka Gunawardene anasema kuwa angependa kuamini, kwa hakika, kuwa vita vimekwisha: | |
54 | Hakuna vidhibitisho huru - vimekuwa ni vita visivyokuwa na shahidi kwa miaka michache iliyopita. | |
55 | Lakini nipo tayari kuwa na imani isiyo ya kawaida, ikiwa kama ni hilo tu linalohitajika ili kukaribisha amani iliyotuchenga kwa muda mrefu. | |
56 | Nitakwenda mpaka mwisho wa dunia, ili kusimamisha kutoamini kwangu, ili kupokea kurejea kwa amani na amani yenye maana. | |
57 | Rais Mahinda Rajapaksa anategemewa kulihutubia Bunge na taifa jumanne asubuhi. | 校對:Soup |