Sentence alignment for gv-swa-20091024-441.xml (html) - gv-zht-20091114-4901.xml (html)

#swazht
1Uanaharakati na Umama Barani Asia亞洲的社運人士與母親
2Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake?為了要爭取與奮鬥的目標,女性得犧牲什麼?
3Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama (wazazi).面對母親受迫害,孩子會經歷什麼影響?
4Irene Fernandez ni mwanamke na mwanaharakati anayepigania haki za wahamiaji nchini Malaysia.本文粗略介紹亞洲同為人母的女性社運人士。
5Kwa zaidi ya miaka kumi, Irene amekuwa akikabiliwa na mashtaka ya ‘uhalifu wa kuvunjia heshima” (ambayo kwa sasa yamefutwa) baada ya kuchapisha memoranda akiihimiza serikali ya Maylasia kuchunguza tuhuma za mateso yanayofanywa katika kambi za wakimbizi nchini humo.
6Licha ya kuwa mwanaharakati, jambo ambalo limempatia tuzo ya Right Livelihood mwaka 2005, Irene pia ni mama wa watoto watatu, Camverra Jose Maliamauv, Tania Jo na Katrina Jorene, mlezi wa watoto wengine kadhaa.
7Ni vigumu kufikiri kuhusu yale yanayopita kwenye vichwa vya wanaharakati kama Irene, hasa pale anapowawaza watoto wake. Wakati alipokuwa akisomewa hukumu mwanzoni mwa mashtaka mwaka 2003, Irene aliripotiwa kusema:Irene Fernandez是馬來西亞移民權運動者,她長達十年以上都面臨「刑事誹謗」告訴(現已撤銷),因為她發表一份備忘錄,要求馬國政府調查國內移民營的傷害事件。
8Nataka watoto wangu na watoto wa watu wote ninaofanya kazi nao kama kiongozi wa Tenaganita kufurahia na kuishi katika jamii iliyo na amani, ambapo hatuogopi misukosuko inayosababishwa na dola. Pengine dhima ya Irene kama mama inaelezwa vizuri zaidi katika macho ya binti yake, Katrina Jorene, ambaye aliandika katika blogu inayoitwa Micah Mandate (blogu ya Kikristu inayolenga kuamsha utetezi wa umma):除了參與社運讓她在2005年獲得Right Livelihood獎之外,她也有Camverra Jose Maliamauv、Tania Jo、Katrina Jorene三個孩子及數名養子女,外人恐怕不易想像Irene身為社運份子,想到子女時會有什麼感受,在2003年官司一審判決時,Irene在報導中表示:
9Ninampongeza mama yangu ambaye alinilea niwe mstahimilivu katika maisha na kuwa wazi na king'ang'anizi wa kutafuta ukweli na katika haki, kweli na haki.我希望無論是自己的孩子,或是其他我們組織所幫助的孩子,都能生活在和平社會中,不必害怕政府暴力。
10Ninawapongeza mashujaa wasio na idadi ambao nimekuwa nao maishani mwangu, hasa wanafamilia yangu na familia ya Tenaganita [Taasisi anayoongoza Irene Fernandez].Irene的母親身分或許可從女兒Katrina Jorene筆下展露,女兒在強調公共利益的基督教部落格Micah Mandate寫道:
11Ninawapongeza wote waliofanya kazi kimya kimya, pasipo kuchoka na kwa umakini mkubwa kwa miaka yote hii ili kupigania manufaa ya umma mpana zaidi. Yaelekea mafunzo ya Irene yamemvuta walau mmoja wa watoto wake kuchukua mrengo wa uanaharakati kama alivyo yeye mwenyewe.我感謝母親養育我長大,讓我時時對生活保持警戒、堅持真理,也堅守正義、真實與正確原則;我感謝無數生命中曾出現的英雄,尤其是我的家人,以及Tenaganita(Irene所帶領的組織)裡的家庭,我感謝所有不眠不休、默默努力的人,謝謝他們多年來關心他人。
12Hivi sasa Katrina huandika makala mbalimbali zinazohusiana na haki na utetezi wa walio wachache katika jamii.因為Irene Fernandez的身教,讓她至少有一個孩子也投身社會運動,目前Katrina常書寫有關少數族群權利與保護的文章。
13Tofauti na ilivyo kwa Katrina Jorene, kwa bahati mbaya, Alexander na Kim Aris, watoto wa mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Aung San Suu Kyi, hawakupata bahati ya kujifunza kutoka kwa mama yao kwa zaid ya muongo mmoja sasa.
14Mapenzi ya Bibi Suu Kyi kwa nchi yake ya Myanmar yamekuwa makubwa kiasi kwamba ametumikia kifungo cha nyumbani kwa takribani miaka kumi na nne katika nyumba iliyo kandokando ya ziwa huko Yangon, ambapo amechagua kuishi kwa kuhofia kwamba huenda utawala wa mabavu wa kijeshi hautamruhusu tena kurudi ikiwa atatoka. Blogu inayohusu wanawake ya Womensphere inaandika:反觀諾貝爾和平獎得主翁山蘇姬(Aung San Suu Kyi)的兩子Alexander及Kim Aris,卻超過十年無法向母親學習,翁山蘇姬因為熱愛緬甸,卻遭軟禁在仰光(Yangon)湖邊住家近14年,她之所以不願離開,是害怕軍政府從此不會再准許她入境,女性議題部落格Womensphere指出:
15Mume wa Bibi Suu Kyi, aliyekuwa raia wa Uingereza na mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Oxford, Michael Aris, alifariki kwa kansa mwaka 1999 akiwa na umri wa miaka 53. Mama huyu hakuweza kumwona mumewe wakati alipokuwa anafariki - serikali ya kijeshi ilimkatalia mume huyo viza ya kuingia nchini, wakati kwa upande wake mama huyo naye alihofia kutoka Burma, kwamba pengine asingeruhusiwa kurudi tena nchini humo.翁山蘇姬的英國籍丈夫是牛津大學學者Michael Aris,他在1999年死於癌症,得年53歲,她無法見到先生最後一面,軍政府拒絕發給丈夫入境簽證,而翁山蘇姬害怕自己若離開緬甸,就無法再度回國,她的兒子現年已超過30歲,已十年未與母親見面。
16Kwa hiyo hajakutana na watoto wake wawili, ambao hivi sasa wana umri wa zaidi ya miaka thelathini, kwa zaidi ya muongo mmoja sasa.關於這兩個孩子的消息並不多,不過長子Alexander在1991年代表母親赴奧斯陸領取諾貝爾和平獎,同樣透過孩子的觀點,我們或許能更瞭解翁山蘇姬身為母親的樣貌:
17Kuna machache sana yaliyoandikwa juu ya (au kuandikwa na) Alexanderson au Kim.身為她的兒子,我個人相信透過她個人犧牲,讓世人瞭解緬甸民眾的苦痛,沒有人應低估他們的苦難。[ …]
18Hata hivyo, mnamo mwaka 1991, mtoto mkubwa wa Bibi Suu Kyi, Alexander, alipokea tuzo ya Amani ya Nobel huko Oslo kwa niaba ya mama yake.我們也不能忘記,她獨自在仰光戒備森嚴的屋宅裡奮鬥,象徵著全世界努力幫助人性精神脫離暴政與心理迫害。[ …]
19Hapa tena, tunaweza kutumia lensi za mtoto huyu ili kupata kumwelewa vema zaidi Bibi Suu Kyi kama mama:雖然外界看待我母親時,仍形容她是位以和平手段爭取民主變革的政治異議人士,但我們仍應記住,她是為追求精神目標。[ …]
20Nikizungumza kama mtoto wake, ningependa kuongeza kwamba mimi binafsi naamini kwamba kwa kujitolea kwake na kutoa sadaka yake binafsi, ametokea kuwa alama yenye thamani ambapo kupitia kwake, mateso ya watu wote wa Burma yametambulika.
21Na, hakuna aliye na haki ya kuyapuuza mateso hayo.我希望母親能很快直接與世人分享她的感受,而不需要透過我的口。
22… Pia tukumbuke kwamba, mapambano yake akiwa katika upweke wake huku akiwa chini ya ulinzi mkali katika makazi yake ya huko Rangoon ni sehemu ya mapambano mapana zaidi, ulimwengu kote, katika kutafuta kuikomboa roho ya kibinadamu kutoka katika tawala za kimabavu za kisiasa na manyanyaso ya kisaikolojia. … Ingawa mama yangu anaelezwa mara nyingi kama mpigania haki za kisiasa na ambaye anajaribu kwa njia za amani kuleta mabadiliko ya kidemokrasia, hatuna budi kukumbuka kwamba mapambano yake, kimsingi, ni ya kiroho.亞洲許多社運份子身為人母仍受迫害,例如Fan Guijuan的住家據說是因上海世博會而遭拆除,她在北京遭逮捕後,送回上海立刻入獄,她的兒子因此無家可歸;菲律賓的Edita Burgos博士則為身為社運人士的兒子Jonas Burgos爭取正義,她的兒子據說已經「失蹤」,她目前主持「失蹤人士家屬正義」組織,為許多失蹤人士追求正義,許多人認為人口「失蹤」現象在艾洛優(Arroyo)政權格外顯著。
23… Ni matumaini yangu kwamba hivi karibuni mama yangu ataweza kuwashirikisha hisia zake na kuzungumza moja kwa moja yeye mwenyewe badala ya kuzungumza kupitia kwangu. Wakati huo huo, wanawake wengi wanaharakati barani Asia wanaendelea kukabili mateso.伊朗的人道份子母親也迅速成為全球人權運動象徵,她們組成「伊朗的哀悼母親」組織,舉行公開靜默抗議活動,以和平方式為死去或入獄的孩子爭取正義。
24Kwa mfano, Fan Guijuan, ambaye nyumba yake iliamriwa kubomolewa sababu ya Mradi wa Shangai World Expo, alikamatwa huko Beijing na kurejeshwa Shanghai, na kisha kuwekwa kizuizini.
25Mtoto wake wa kiume hana mahali pa kuishi, kwa sababu ya bomoabomoa hiyo.「一日為母,終身為母」
26Wakati huohuo, huko Ufilipino, Dkt Edita Burgos, ambaye ni mama wa Jonas Burgos, anapigania haki ya mtoto wake huyo mwanaharakati, ambaye inasemekana “ametoweka“.
27Dkt Burgos ni mwenyekiti wa chama cha haki za Familia za watu Waliotoweka, yaani asasi inayotafuta haki za watu waliopoteza maisha yao pasipo kujulikana, jambo ambalo linasemekana ni kielelezo cha utawala wa Arroyo.
28Hivi sasa, huko Irani, akina mama wanaharakati wa haki za binadamu, wanazidi kuwa alama za ulimwengu katika kupigiania haki za binadamu ulimwenguni kote.
29Katika mgomo baridi wa kimyakimya ulioshirikisha umma, ‘Akina Mama Wanaoomboleza wa Irani‘, ambao wanajulikana huko Tehran kama “Akina Mama wa Laleh”, kwa njia za amani wanatafuta haki kwa ajili ya watoto wao waliokufa au waliofungwa.
30“Mama ni mama ili mradi tu aishi.”校對:Soup