# | swa | zht |
---|
1 | Irani: Ziara ya Rais Ahamdinejad Nchini Lebanoni Rais wa Irani, Mahmoud Ahmadinejad, amemaliza ziara yake ya siku mbili nchini Lebanoni. | 伊朗:總統出訪黎巴嫩 |
2 | Ilikuwa ni ziara yake rasmi ya kwanza tangu mwaka 2005 wakati alipochukua madaraka. Alikuwa na mazungumzo na maofisa wa Lebanoni na alizuru ngome za maswahiba wa Irani, Hezbollah, katika vitongoji vya kusini mwa mji mkuu na kusini mwa Lebanoni ambako alipata mapokezi ya shujaa. | 伊朗總統阿曼尼內賈德(Mahmoud Ahmadinejad)剛結束黎巴嫩的兩天訪問行程,這是他自2005年上任以來,首次出訪該國,除了與官員會晤,亦前往首都南部郊區及黎國南部,獲得如英雄式的接待,這兩地均為真主黨重鎮,該組織和伊朗往來相當密切。 |
3 | Wanablogu kadhaa wa Irani walitoa maoni kuhusu ziara hiyo. | 對此次出訪,多位伊朗部落客都表達看法。 |
4 | Meybodema amechapisha picha kadhaa za ziara ya Ahmadinejad nchini Lebanoni na kumnukuu [fa] Sayyid Hassan Nasrallah, kiongozi wa Hezbollah, ambaye aliisifu Jamhuri ya Kiislamu na kumkaribisha Ahmadinejad. | Meybodema張貼幾張訪問行程照片,並引述真主黨領袖納斯拉亞(Sayyid Hassan Nasrallah)的言論,讚揚伊朗與歡迎阿曼尼內賈德。 |
5 | Mwanablogu huyo alimnukuu Nasrallah akisema kwamba kinyume na propaganda zote, “Irani inawasaidia wanaokandamizwa”. | 納斯拉亞表示,伊朗所為與所有政治宣傳相反,「是在幫助受迫害者」。 |
6 | Sayeh Azadi alichapisha tena (tafadhali angalia hapo juu) kikaragosi kilichochorwa na mchoraji vikaragosi anayeongoza nchini Irani Nikahang kutoka kwenye Roozonline [fa] kikaragosi hicho kilikuwa na kichwa cha habari kinachosema “Ndoto za Ahmadinejad kwa Lebanoni”. | Sayeh Azadi轉載(見上圖)知名伊朗漫畫家Nikahang在Roozonline張貼的漫畫,圖說寫著「阿曼尼內賈德的黎巴嫩美夢」。 |
7 | Z8unak anahesabu sababu zinazoeleza ni kwa nini watu wa Lebanoni walimkaribisha Ahmadinejad. | Z8unak寫下黎巴嫩人民歡迎阿曼尼內賈德的原因: |
8 | Mwanablogu huyo anaandika [fa]: | 阿曼尼內賈德在黎巴嫩受到熱情歡迎,各位為何驚訝? |
9 | Kwa nini mlishangaa kwamba Ahmadinejad alipokelewa vizuri mno nchini Lebanoni? | 兩伊戰爭結束至今已20年,伊朗邊境城市尚未重建,但黎巴嫩的房屋卻是用伊朗經費重建;每天都有許多伊朗民眾無法負擔醫療費用而死亡,但伊朗卻為黎巴嫩興建醫院。 |
10 | Baada ya miaka 20 ya vita vya Iraki-Irani, miji ya mpakani haikujengwa lakini nyumba nchini Lebanoni zilijengwa kwa pesa zetu. | Mollah以諷刺口吻寫道: |
11 | WaIrani wengi hawawezi kumudu kwenda kwa daktari au hospitali na matokeo yake wanakufa kila siku, wakati huo huo irani inajenga hospitali nchini Lebanoni. Mollah anaandikakwa kejeli: | 黎巴嫩民眾沒看到伊朗政府做任何壞事,若我們是黎巴嫩人,又拿到錢,我們都會成為伊朗的支持者,他們說,我們不在乎這些人是否以政變上台或虐待人民…把錢拿來就可以。 |
12 | WaLebanoni hawakuona ubaya wowote wa serikali ya Irani. | 校對:Soup |
13 | Kama tungekuwa WaLebanoni na kupokea pesa hizo tungegeuka kuwa waunga mkono wa Jamhuri ya Kiislamu… Wanasema, hartujali ikiwa wapo madarakani baada ya ‘mapinduzi ya nguvu' au ikiwa wanatesa watu… ili mradi wanatoa pesa. | |