# | swa | zht |
---|
1 | Irani: Kimbunga cha Maandamano Baada Ya Uchaguzi | 伊朗:選舉後引爆大規模抗爭 |
2 | Maelfu ya watu waliandamana mjini Tehran, Mashdad na kwenye miji mingine mikubwa ya Irani ili kupinga ushindi wa Rais Mahmoud Ahmadinejad katika uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa. | 大批民眾走上德黑蘭、Mashhad及伊朗各大城市示威,抗議現任總統阿曼尼內賈德(Mahmoud Ahmadinejad)宣稱在6月12日的大選中勝出,兩位改革派候選人及其支持者宣稱選舉過程中有弊。 |
3 | Washindani wawili wanamageuzi pamoja na mashabiki wao wanasisitiza kwamba palitokea udanganyifu. Mir Hussein Mousavi, mpinzani mkuu wa Ahmedinejad alisema kuwa matokeo yaliyotolewa na “waangalizi wasioaminika” yanaakisi “udhaifu wa nguzo zinazosimamisha mfumo mtakatifu” wa Irani na “utawala wa mabavu.” | 主要在野候選人穆沙維(Mir Hussein Moussavi)表示,選舉結果由「無法信賴的監察人」公佈,突顯「伊朗神聖制度的支柱受到動搖」,以及「暴政及獨裁統治國家」,許多街頭抗爭及鬥毆畫面也出現在YouTube網站上。 |
4 | Matukio kadhaa ya kupigana mitaani na maandamano yamewekwa kwenye YouTube. | 首都德黑蘭Valiasr街的抗議現場中,數千名抗爭民眾高喊反政府口號。 |
5 | Maandamano katika mtaa wa Valiasr mjini Tehran ambako maelfu ya waandamanaji walipinga kwa kuimba kauli mbiu dhidi ya serikali ya Ahmadinejad. | 還有民眾高呼:「穆沙維,拿回我的選票!」: |
6 | Na hapa watu waliimba: ‘Mousavi, rejesha kura yangu!'. | 軍警人員鎮壓抗議者: |
7 | Vyombo vya usalama vilidhibiti waandamanaji: Maandamano mengine yalifanyika mjini Mashad ambako waandamanaji waliwaomba wanausalama wawaunge mkono [badala ya kuwadhibiti]. | Mashhad的抗爭活動中,抗議者要求軍警支持他們,而非阻擋他們: |
8 | Ghomar Ashegahne amechapisha picha kadhaa zinazoonyesha wanausalama wakiwapiga waandamanaji (tazama picha hapo juu). Mwanablogu huyo anaandika [fa] kwamba udhibiti ungekuwa ni sababu nzuri ya kutokwenda kwenye maandamano, lakini ‘tufanye nini na uchungu huu?' | Ghomar Ashegahne張貼[波斯文]許多軍警毆打抗議群眾的照片(如上圖所示),他亦指出,暴力壓制會讓人們不敢上街反抗,但「痛苦的我們還能怎麼辦?」,他認為兩位改革派候選人若希望改變國內現況,此刻就該開始。 |
9 | Anasema kuwa Karoubi na Mousavi [wanamageuzi wawili waliogombea] walitaka kubadili hali nchini, na inawabidi waanze sasa. Belgiran anaandika [fa] kwamba Kiongozi wa Irani, Ali Khamenei, alimpindua Mousavi hata kabla hajakuwa rais na akamweka Ahmadinejad… Anaandika, “Utawala huu umepoteza uaminifu mdogo uliokuwepo.” | Belgiran提到,伊朗領導人Ali Khamenei過去在穆沙維還沒上任,就已發動政變推翻他,並由阿曼尼內賈德取而代之,…他寫道:「這個政權如今喪失了最後一點點合法性」。 |
10 | Mehrdadd anaandika kwenye Twita, kwamba kiongozi wa Irani anaonyesha kuwa yuko dhidi ya watu wa Irani. | Mehrdadd在Twitter上指出,伊朗總統展現反人民的態度,任何政治人物也都該表明對人民的立場。 |
11 | Na sasa kila mwanasiasa anapaswa achukue msimamo ulio kwa ajili ya wananchi au dhidi ya wananchi. | Mehri912則說:「若伊朗今晚睡去,就將永遠沉睡」。 |
12 | Mehri912 anasema kwenye Twita, “Kama Irani italala usiku wa leo, basi ndiyo italala daima”. | 校對:Soup |