# | swa | zht |
---|
1 | Serikali Ya Irani Yautumia Mgogoro Wa Gaza Kukandamiza | 伊朗政府利用加薩壓制輿論 |
2 | Wakati wanablogu kadhaa wa Kiirani (pamoja na wale wa-Kiislamu) waliongeza makala zao na jitihada nyingine za kidijitali, kama vile “Google bomb” kulaani uvamizi wa Israeli katika ukanda wa Gaza, wanablogu wengine wanasema kwamba serikali ya Irani inatumia ‘mwanya wa mgogoro wa Gaza' kukandamiza vyombo vya habari na asasi za kiraia ndani ya nchi hiyo. | |
3 | Wiki iliyopita, utawala wa Irani uliifungia Kargozaran, moja ya jarida mashuhuri la mabaliko, kwa sababu ilichapisha tamko la chama cha wanafunzi (Tahkim Vahadat) ambalo liliilaani Israeli lakini pia liligusia kundi moja la Wapalestina wenye siasa kali ambalo hujificha kwenye mahospitali na mashule, kama ni kundi la magaidi. | |
4 | Nik Ahnag, bloga mashuri na mchoraji wa vikaragosi, alichora picha za vichekesho zinazohusu uvamizi wa Gaza na mizani ya nguvu zisizolingana kati ya Israeli na Palestina kwenye upande mmoja na ukandamizaji wa serikali ya Irani kwenye upande mwingine. Moja ya michoro hiyo inaonyesha nyundo kubwa yenye chapa ya Gaza ikilipiga jarida la Kargorazan. | 伊朗有些部落客(包括伊斯蘭主義者)運用文章與網路行動(如「Google炸彈」)譴責以色列入侵加薩地區,亦有許多部落客指出,伊朗政府趁著加薩動盪時刻,藉機壓制國內媒體與公民社會。 |
5 | Katika mchoro huo inaonekana kwamba waalimu, wanawake na wanafunzi ndio wanaofuatia katika zoezi la kulengwa shabaha. Mwanablogu Jamhour anaandika kuhusu tamko lililopelekea kufungwa kwa jarida hilo la mabadiliko. | 不久前伊朗政府關閉知名改革派網站Kargozaran,因為其中刊登學生運動Tahkim Vahdat的聲明,除譴責以色列之外,亦提到巴勒斯坦武裝團體躲藏於醫院及學校中進行恐怖活動。 |
6 | Anasema [Fa]: Inawezekana kuwa mantiki ya tamko hili ni kuwa wengi wa wanasiasa wa Kiirani wanafikiri, lakini hawawezi kuthubutu kusema, kwamba mgogoro wa Gaza ni kisingizio [cha utawala wa Irani] cha kukwepa matatizo ya kiuchumi na kijamii yanayoongezeka. | 知名漫畫家兼部落客Nik Ahnag刊登數則關於加薩危機的作品,一方面是以色列與加薩兩地權力不平衡,另一方面是伊朗政府的高壓手段,其中一幅漫畫裡,有支寫著「加薩」的大槌子重擊Kargozaran部落格,教師、女性與學生似乎是之後的對象。 |
7 | Leo hii inatupasa kujiuliza na kutathmini, mapambano ya mwaka jana kati ya Hamas na Fatah huko Gaza ambapo mamia ya Wapalestina waliawa na kujeruhiwa. | Jomhour認為[波斯文]是這紙聲明導致部落格遭關閉: |
8 | Ghasia zilikuwa kali kiasi kwamba ziliwafanya baadhi ya waunga mkono wa Fatah wakimbilie Israeli kwa ajili ya hifadhi. Bloga huyo anahitimisha kwamba mashambulizi ya kinyama ya Israeli pamoja na ufisadi wa baadhi ya viongozi wa Kipalestina unarutubisha makundi ya kigaidi na yale yanayochochea ghasia na chuki za kikabila na kidini. | 伊朗許多政治人物可能對這紙聲明心有同感,但沒有勇氣說出口,不敢明白表示加薩危機只是伊朗政府避免經濟與社會問題的藉口,我們應該捫心自問,究竟該如何看待去年哈瑪斯與法塔兩大組織在加薩的衝突,當時導致數百名巴勒斯坦人喪生,當時情況相當激烈,部分法塔支持者甚至前往以色列避難。 |
9 | Katika blogu ya Mibibi tunasoma [Fa]: | Jomhour認為是因為以色列野蠻攻擊與部分巴勒斯坦領袖貪腐,才讓恐怖組織與煽動種族及宗教仇恨暴力的團體坐大。 |
10 | Kufungwa kwa Kargozaran kumewafanya watu wengi wapoteze ajira, na imekuwa vigumu zaidi [bila ya majarida yasiyo rasmi] kuwapa habari zinazohusu Gaza watu ambao hawaziamini idhaa za televisheni za serikali pamoja na tovuti zake. | Mibibi blog指出[波斯文]: |
11 | Bloga Hossein Ghazian naye analalamika na kupinga uchujwaji wa habari. | Kargozaran網站關閉讓數十人失業,人們若不相信官方網站或國營電覙台對加薩的報導,現在也愈來愈來獲知其他資訊。 |
12 | Bloga huyo anasema [Fa]: “Kama hatuwezi kuitetea Israeli na kuongea dhidi ya Wapalestina, maneno yangu ya kuulani uvamizi na ubabe wa Israeli yatakuwa hayana maana kadhalika hayatakuwa na uzito…” St Behesht anaandika kuhusu “Kushindwa kwa televisheni ya Irani pamoja na kuchujwa kwa habari”. | Hossein Ghazian也抱怨[波斯文]網路審查日盛:「若我們不能自由捍衛以色列人或批評巴勒斯坦人,譴責以色列入侵的言辭就顯得無用與缺乏公信力…」 |
13 | Bloga huyo anasema [Fa]: Siku hizi, katika kila sehemu ya Irani ambako watu huongelea siasa, huongelea ugomvi wa Israeli na Hamas. | St Behesht則提及[波斯文]「伊朗電視的失敗與審查」: |
14 | Idhaa ya televisheni ya Irani inachochea mjadala huo, lakini utawala wa Irani haujagundua bado kwamba propaganda zao kwenye televisheni matokeo hasi dhidi ya Hamas. Tofauti na malengo ya televisheni ya Irani, kuna watu zaidi ya wachache ambao wanachukua upande unaoipinga Hamas na kuiunga mkono israeli…. | 這些日子以來,伊朗各地民眾談論政治時,都是關於哈瑪斯與以色列的衝突,伊朗國營電視引起人們的討論,但政府卻還沒察覺到,他們在電視的宣傳對哈瑪斯造成負面影響,不少人因為伊朗電視台的報導,反而開始反對哈瑪斯並支持以色列,…可惜伊朗政府還沒明白此事,仍期望這些報導能影響輿論觀感。 |
15 | Kwa bahati mbaya utawala wa Irani haujalielewa hili, na wanaendelea na njozi zao wakitumaini [kuwa propaganda zao] zanawashawishi Wairani. | 校對:Soup |