# | swa | zht |
---|
1 | Irani: Mwaka Mpya Waanza na Ujumbe Kutoka Kwa Obama | 伊朗:傳統新年與歐巴馬談話 |
2 | Mwaka huu, sherehe za mwaka mpya wa Ki-Irani zilianza na ujumbe usiotarajiwa kutoka kwa rais wa Marekani Barak Obama, uliolekezwa kwa watu wa Irani na kwa mara ya kwanza, kwa viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu, ujumbe huo ulitoa rai ya kuanza upya kati ya nchi hizo mbili. | |
3 | Wanablogu kadhaa wametoa maoni kuhusu ujumbe huo, na wengine wanaanza kuziona zama mpya baada ya zaidi ya miaka 30 ya misukosuko kati ya mataifa haya mawili. | |
4 | Mohammad Ali Abtahi, makamu wa rais wa zamani, anadhani ujumbe wa Obama ni wa muhimu sana na anaandika: | |
5 | Kwa jina la jamhuri ya Kiislamu ya Irani, pia nawapongeza taifa la Irani na viongozi wake. | |
6 | Bila ya shaka hii ni fursa ya kihistoria. | 本文英文版原載於2009年4月6日 |
7 | Hatuwezi kudharau umuhimu wa Marekani katika hali ya sasa ya Irani. Bila ya shaka hatuwezi kupuuza nyayo za Marekani katika kila majalada ya wasifu wa Irani hasa yale ya kiuchumi hata kama ni kwa uchache, kutokana na vikwazo vilivyowekwa dhidi ya taifa la Irani. | 今年的伊朗新年一開始,便意外收到來到美國總統歐巴馬(Barack Obama)的訊息,他直接訴諸伊朗民眾,也首次直接向伊朗領導人喊話,希望兩國能有新的開始,多位部落客有所回應,有些人認為雙方歷經30年的爭論與吵鬧,即將跨入新時代。 |
8 | Kutuma ujumbe wa pongezi kunaweza kuwa ni fursa muhimu kisiasa, kiuchumi na kihistoria, leo hii na hata baada ya kubadilishwa serikali ya Marekani. | 伊朗前副總統Mohammad Ali Abtahi認為歐巴馬的談話極為重要,他表示[英文]: |
9 | Kadhalika kupuuza kunaweza kuifanya hali izidi kuwa ya hatari zaidi ya ilivyokuwa wakati wa utawala wa Bush kwa sababu Obama anaweza kukusanya viongozi wa kisiasa na maoni ya wananchi dhidi ya Irani. Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari Masih Alinejad anaandika [fa] kuhusu sababu zilizoifanya Idhaa ya Taifa ya Televisheni kutotangaza ujumbe wa Obama. | 恭喜伊朗這個國家與領袖,這肯定是個歷史機會,我們不能忽視美國對伊朗現狀的重要性,我們亦不可忽視美國領袖對伊朗一切事物中的痕跡,至少對伊朗的禁運令即影響經濟,發送祝賀訊息能成為最重要的政治、經濟與歷史機會,美國政府將從今日起改變,若忽視這件事情,可能讓伊朗陷入比布希政府時代更危險的境界,因為歐巴馬能動員政治領袖和輿論一同反對伊朗。 |
10 | Anaongeza: kama Obama angeongea kama Bush na kuitathmini Irani kama tishio, Idhaa ya Televisheni ya Taifa ingetangaza mara kadhaa. | 部落客兼記者Masih Alinejad提及[波斯文],為何伊朗國營電視台沒有播出歐巴馬的談話: |
11 | Mwanablogu huyu anatukumbusha ile hotuba ya mashuhuri ya Bush ambayo aliita Irani mwanachama wa kundi la waovu ilitangazwa mara kadhaa kwenye televisheni ya taifa. | 若歐巴馬言論與布希無異,同樣認為伊朗是個威脅,伊朗國營電視台就會播出好幾次,有部落客提醒,布希曾在演說中,將伊朗列為邪惡軸心一員,國營電視台當天就播出數次。 |
12 | Zandgieh Sagi ameuita [fa] ujumbe wa Obama kama ujumbe chanya na jambo ambalo linawastahili watu wa Irani. | Zandegieh Sagi認為[波斯文]歐巴馬的言論相當正面,也是伊朗人民應得的對待,他表示伊朗政府應先學著使用合宜的政治語言。 |
13 | Mwanablogu huyu anasema kuwa jambo la kwanza ambalo serikali ya Irani inaweza kulifanya ni kutumia lugha inayofaa kisiasa. | View from Iran部落格指出[英文]: |
14 | Katika blogu ya In View from Iran tunasoma: | 美國政府有許多途徑可建立信任,並非所有都得等待伊朗政府願意和美國對話,我認為歐巴馬的新年談話很正面,但我們的需求並不止於一段談話。 |
15 | Kuna hatua nyingi ambazo serikali ya Marekani inaweza kuzichukua ili kujenga imani. Siyo zote ambazo zitategemea nia ya serikali ya Irani ya kuanzisha mazungumzo na Marekani. | Mmoeeni提到[波斯文],雖然伊朗電視台未播出歐巴馬談話內容,伊朗總統仍在美國污辱美國領導人,他還語帶諷刺地表示,伊朗總統現在可說,國內擁有絕對自由。 |
16 | Nauona ujumbe wa Obama wa mwaka mpya kama ujumbe chanya, lakini tunahitaji zaidi ya hilo. | 新年假期 |
17 | Mmoeeni anaandika [fa] kwamba wakati televisheni ya Irani haikutangaza habari zinazohusu ujumbe wa Obama, rais wa Irani aliweza kuwatukana viongozi wa Marekani huko Marekani. Mwanablogu huyo anaongeza, kwa kejeli, kwamba Ahmedinejad atasema kwamba kuna uhuru wa kweli nchini Irani. | 伊朗人在春季第一天慶祝Norouz (Nowruz)為新年假期,有些民眾會到帕薩爾加德[中文](Pasargad,即上圖),赴波斯帝國創建者居魯士二世[中文](Cyrus the Great)陵寢獻花,Save Pasargad網站指出[波斯文],伊朗政府並未照顧這個歷史遺跡訪客的需求,但近年來有愈來愈多人前往帕薩爾加德慶祝新年。 |
18 | Sherehe za Mwaka Mpya Wairani walisherehekea Norouz (Nowruz) kunako siku ya kwanza ya msimu wa kuchipuka mimea. | 校對:dreamf |
19 | Katika dhifa hii, baadhi ya Wairani huweka maua kwenye kaburi la Cyrus Mkuu, mwanzilishi wa ufalme wa kwanza wa Persia katika Pasargad (pichani juu). | |
20 | Kwenye tovuti ya Okoa Pasargad imeandikwa [fa] kwamba utawala wa jamhuri ya Kiislamu hausaidii wageni wanaozuru sehemu hii ya kihistoria, lakini katika miaka ya hivi karibuni watu wengi wamekuwa wakizuru ili kuusherekea mwaka mpya huko Pasargad. | |