# | deu | swa |
---|
1 | GV Face: Weltweite Medienberichterstattung zu Syrien | GV Face: Mitazamo Tofauti Kuhusu Habari za Mgogoro wa Syria |
2 | Wie unterscheidet sich die Berichterstattung über die syrische Krise in Abhängigkeit zu dem Ort, an dem du dich gerade aufhältst? | Ni namna gani habari zinazozungumzia mgogoro wa Syria zinategemeana na mahali uliko? |
3 | Und was bedeutet das für Syrer? | Na hiyo ina maana gani kwa raia wa Syria? |
4 | Wir haben darüber und zu weiteren Themen in unserer zweiten Ausgabe von GV Face im Rahmen eines Google Hangouts am Montag, den 23. September 2013 um 15 Uhr UTC [koordinierte Weltzeit, in Deutschland ist das nach der mitteleuropäischen Sommerzeit 17 Uhr] diskutiert. | Tulijadili suala hili na mengine mengi kwa kutumia zana ya majadiliano ya Google Hangout Jumatatu ya Septemba 23, 2013, saa 3 alasiri UTC katika toleo letu la pili la GV Face. |
5 | Berichte aus den USA und Großbritannien legen nah, chemische Waffen seien durch das Regime von Präsident Assad verwendet worden um im letzten Monat über tausend Menschen in Syrien zu töten. | Taarifa katika nchi za Marekani au Uingereza zinadai kuwa silaha za maangamizi zilitumiwa na utawala wa Rais Assad kuwaua watu zaidi ya elfu moja nchini Syria mwezi uliopita. |
6 | Russische Reporter behaupten dagegen, “alles sei gut” in Damaskus. | Wakati huo huo, vyombo vya habari vya Urusi vinasema, “hali ni shwari” mjini Damascus. |
7 | Iranische Medien berichten, dass chemische Angriffe von “Rebellen” durchgeführt worden seien, um den Druck in Richtung einer internationalen Intervention zu erhöhen. | Vyombo vya Habari vya Iran vinadai shambulio la kemikali lilifanywa na “waasi” katika juhudi za kutaka kuongeza shinikizo la kimataifa kuingilia kati. |
8 | Während die Regierung der USA ein militärisches Eingreifen in Syrien abwägt, appellierte der russische Präsident Putin durch die Zeitung New York Times an das amerikanische Volk, ihre Waffen aus dem von Krieg erschütterten Land rauszuhalten. | Wakati serikali ya Marekani ifikiri kuishambulia Syria kijeshi, Rais wa Urusi akiwa New York amewasihi watu wa Marekani kufutilia mbali mpango wao wa kuipiga nchi hiyo ambayo tayari imeshaharibiwa mno na vita. |
9 | Videos, die auf Einsätze iranischen Militärs auf syrischem Boden hindeuten, verbreiteten sich über soziale Medien wie ein Lauffeuer. | Video zinazoonyesha dalili ya hatua za kijeshi zinazochukuliwa na Iran nchini Syria zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii. |
10 | Die Teilnehmer des Hangouts waren unter anderem die GV Syrien-Autorin Leila Nachawati (die ebenfalls Gründerin von Syria Untold ist, einem Storytelling-Projekt im Internet, das sich dem gewaltfreien, syrischen Aufstand widmet), RuNet Echo-Redakteur Kevin Rothrock, der über die Kolumnen [in der New York Times] von Putin und Mc Cain sprach und darüber, wie sie im russischen Internet wahrgenommen wurden, unsere MENA-Redakteurin Amira Al Hussaini, die das Thema der Bürger- und Massenmedien und ihrer Berichterstattung zu Syrien innerhalb des Nahen Ostens und Nordafrika anschnitt, unsere Redaktionsleiterin Solana Larsen, die sich zu der Rolle der Bürgermedien angesichts der Darstellung Syriens in den Massenmedien äußerte, unsere AdvocacyRedakteurin Ellery Biddle, die darüber sprach, wie die Rufe nach einer Intervention der USA von den US-amerikanischen Netzbürgern gedeutet werden und unser Geschäftsführer Ivan Sigal, der seine Meinung dazu äußerte, warum die Berichterstattung zu Syrien so ist, wie sie ist und zwar weltweit. | Washiriki wa mazungumzo yetu hayo ya mtandaoni walikuwa ni pamoja na mwandishi wa Gv Syria, Leila Nachawati, Mwanzilishi wa Syria Untold, mradi wa kupashana habari mtandaoni uliojikita kwenye mapinduzi ya amani yanayofanywa na wananchi wa Syria; Mhariri wetu wa RuNet Echo Kevin Rothrock aliyezungumza kuhusu Putin na Mc Cain OpEds na namna wanavyotazamwa na mitandao ya Urusi; Amira Al Hussaini, Mhariri wetu wa Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, aliyegusia habari zilizikuwa zinaandikwa na vyombo vya habari vya kiraia na vyombo vikuu vya habari ndani ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini; Solana Larsen, Mhariri Mtendaji alizungumzia kuhusu wajibu wa vyombo vya habari vya kiraia katika taswira inayojengwa na vyombo vikuu vya habari kuhusu Syria, Ellery Biddle Mhariri wa Utetezi aliyezungumza namna wito wa kuiomba Marekani kuingilia kati mgogoro huo inavyotafsiriwa na raia wa Marekani mtandaoni na Ivan Sigal Mkurugenzi Mtendaji aliyetoa maoni yake kuhusu namna habari za Syria zinavyoumbwa kuwa vile zilivyo duniani kote. |
11 | Hintergrundinformationen zur internationalen Berichterstattung über die Syrienkrise, siehe unsere Seite für die Sonderberichte [en]. | Kupata habari za kimataifa zilizojikita kwenye Mgogoro wa Syria, unaweza kupitia ukurasa wetu maalumu. |